2010–2019
Mtegemee Yesu Kristo.
Mkutano Mkuu wa Aprili 2019


Mtegemee Yesu Kristo.

Tukimtegemea Yesu Kristo, Yeye atatusaidia kuishi maagano yetu na kukuza miito yetu kama wazee katika Israeli.

Wakati Yesu akitembea katika mtaa karibu na Kapenaumu1 pamoja na kundi kubwa la watu waliomzunguka, mwanamke aliyekuwa akiteseka kwa hali mbaya kwa miaka kumi na miwili alijinyoosha na kugusa pindo la vazi lake. Mara moja aliponywa.2

Maandiko yanaandika kwamba Yesu, akitambua “kwamba [nguvu zimemtoka].”3 “aligeuka katika msongamano”4 na “akatazama … kumwona yule ambaye amefanya kitu hiki.”5 “Yule mwanamke, alipoona ya kwamba hawezi kusitirika,”6 “akaanguka mbele yake, akamweleza kweli yote.”7

Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya: enenda zako kwa amani.”8

Yesu Kristo alimwokoa mwanamke. Alikuwa ameponywa kimwili, lakini wakati Yesu alipogeuka kumwangalia, alitangaza imani yake kwa Yesu na Yesu aliponya moyo wake.9 Alisema naye kwa upendo, alimhakikishia juu ya kukubaliwa, na alimbariki kwa amani Yake.10

Akina kaka, kama wenye ukuhani mtakatifu, tunashiriki katika kazi ya wakovu. Katika mwaka uliopita, Bwana emeweka uongozi wa kazi hii kwa uaminifu juu ya mabega ya wazee katika Israeli.11 Tunalo jukumu kutoka kwa Bwana—kufanya kazi na dada zetu, tunatakiwa kutumikia katika njia takatifu zaidi, kuongeza kasi ya kukusanya Israeli katika pande zote za pazia, kuweka imara nyumba zetu kama mahali pa madhabahu ya imani na kujifunza injili, na kuandaa ulimwengu kwa Ujio wa Pili wa Yesu Kristo.12

Kama katika vitu vyote, Mwokozi ametuonesha njia: tunahitaji kumtegemea na kumtumikia Yesu Kristo kama Yeye alivyo mtegemea na kumtumikia Baba Yake.13 Mwokozi alilisema kwa njia hii kwa Nabii Joseph:

“Nitegemeeni katika kila wazo; msitie shaka, msiogope.

Tazama majeraha yaliyoko yaliotobolewa ubavuni mwangu, na pia alama za misumari katika mikono na miguu yangu; kuweni waaminifu, zishikeni amri zangu, na mtaurithi ufalme wa mbinguni.”14

Katika ulimwengu kabla ya maisha ya duniani, Yesu alimwahidi Baba Yake kwamba angefanya mapenzi ya Baba Yake na kuwa Mwokozi na Mkombozi wetu. Wakati Baba yake alipouliza, “Nimtume Nani?”15 Yesu alijibu:

“Niko hapa, nitume mimi.”16

“Baba, mapenzi yako yafanyike, na utukufu uwe wako milele.”17

Katika maisha yake yote ya duniani Yesu aliishi ahadi hiyo. Kwa unyenyekevu, upole, na upendo, Alifundisha mafundisho ya Baba Yake na alifanya kazi ya Baba Yake kwa nguvu na mamlaka Baba Yake aliyompa.18

Yesu aliutoa moyo wake kwa Baba yake. Alisema:

“Nampenda Baba.”19

“Ninafanya siku zote vitu hivyo ambavyo vinampendeza Yeye.”20

“Nilikuja … sio kufanya mapenzi yangu, bali mapenzi ya [Baba ambaye] alinituma mimi.“21

Katika mateso yake huko Gethsemane, aliomba, “Hata hivyo sio mapenzi yangu, bali yako yatimizwe.”22

Wakati Bwana anapowaita wazee katika Israeli “nitegemeeni katika kila wazo” na “Tazama majeraha” katika mwili Wake uliofufuka, ni mwito wa kukataa dhambi na ulimwengu na kumgeukia Yeye na kumpenda na kumtii. Ni mwito wa kufundisha mafundisho Yake na kufanya Kazi yake katika njia Yake. Kwa hivyo, ni wito wa kumwamini Yeye kikamilifu, kuacha mapenzi yetu na kutoa mioyo yetu Kwake, na kupitia nguvu Yake ya kukomboa kuwa kama Yeye.23

Akina kaka, kama tutamtegemea Yesu Kristo, Yeye atatubariki tuwe Wazee Wake katika Israeli—wanyenyekevu, wapole, watiifu, waliojawa na upendo Wake.34 Na tutaleta shangwe na baraka za injili Yake na Kanisa Lake katika familia zetu na kwa kaka na dada zetu pande zote za pazia.

Rais Russell M. Nelson, ametuita kumtegemea Yesu Kristo katika njia hii: “Hakuna kitu rahisi au kinachotokea chenyewe kuhusu kuwa wafuasi wenye nguvu namna hiyo. Fokasi yetu lazima ikazwe kwa Mwokozi na injili Yake. Ni vigumu kiakili kujitahidi kumtegemea Yeye katika kila wazo. Lakini tunapofanya hivyo, mashaka yetu na hofu hutoweka.”25

Kaza ni neno kuu. Inamaanisha kufungwa imara, kuvutia na kushika kikamilifu.26 Tunakaza fokasi yetu kwa Yesu Kristo na injili yake kwa kuishi maagano yetu.

Wakati tunapoishi maagano yetu, yanaathiri kila kitu tunachosema na kufanya. Tunaishi maisha ya agano27 yaliyojaa matendo rahisi, ya kila siku ya imani ambayo inayotuelekeza sisi kwa Yesu Kristo: sala kutoka moyoni katika Jina lake, tukisherehekea kwenye neno Lake , tukimgeukia Yeye kutubu thambi zetu, tukishika amri Zake , kushiriki sakrament na kuitunza Sabato Yake takatifu, tukiabudu katika hekalu Lake takatifu mara nyingi kadiri tunavyoweza, na kutumia ukuhani Wake mtakatifu kuhudumia watoto wa Mungu.

Vitendo hivi vya kimaagano hufungua mioyo yetu na akili kwenye nguvu ya ukombozi ya Mwokozi na ushawishi wa utakaso wa Roho Mtakatifu. Mstari juu ya mstari, Mwokozi anabadili asili yetu hasa, tunaongoka kwa kina Kwake, na maagano yetu huwa hai katika mioyo yetu.28

Ahadi tunazofanya kwa Baba yetu wa Mbinguni zinakuwa kujitolea kuliko imara kama mwamba, nia zetu za dhati. Ahadi za Baba wa Mbinnguni kwetu zinatujaza na shukrani na furaha.29 Maagano yetu yanakoma kuwa sheria tunazozifuata na kuwa kanuni za upendo ambazo zinatutia moyo na kutuongoza na kukaza fokasi yetu kwa Yesu kristo.30

Vitendo hivi vya dhati vinapatikana kwa wote, vijana na wazee. Ninyi wavulana wenye ukuhani mtakatifu wa Haruni, kila kitu nilichosema usiku huu kinawahusu nyinyi. Namshukuru Mungu kwa ajili yenu. Mnafanya ibada takatifu na maagano yanayopatikana kwa mamilioni ya Watakatifu wa siku za Mwisho kila wiki. Mnapoandaa, kubariki, au kupitisha sakramenti; kuhudumu; kubatizwa katika hekalu; mnapomualika rafiki kwenye shughuli; au kumuokoa muumini wa akidi yenu, mnafanya kazi ya wokovu. Ninyi pia mnaweza kumtegemea Yesu Kristo na kuishi maagano yenu kila siku. Ninawaahidi kwamba kama mtafanya hivyo, mtakuwa watumishi wa kuaminika wa Bwana sasa na, katika siku zijazo, wazee wenye nguvu katika Israeli.

Akina kaka, Ninajua kwamba haya yote yanaweza kuonekana yanakatisha tamaa. Lakini tafadhali kumbukeni maneno haya ya mwokozi: “Siko peke yangu, kwa sababu Baba yupo pamoja nami.”31 Hivyo ndivyo ilivyo kwetu. Hatuko peke yetu. Bwana Yesu Kristo na Baba yetu wa Mbinguni wanatupenda, na Wako pamoja nasi.32 Kwa sababu Yesu alimtegemea Baba Yake na akakamilisha dhabihu kuu ya upatanisho, tunaweza kumtegemea Yesu Kristo kwa imani kwamba Atatusaidia.

Hakuna kati yetu aliye mkamilifu. Wakati mwingine tunakwama. Tunavurugwa mawazo au kukatishwa tamaa. Tunajikwaa. Lakini kama tutamtegemea Yesu Kristo kwa moyo wa toba, Yeye atatuinia, kutuosha kutoka dhambi, kutusamehe, na kuponya mioyo yetu. Yeye ni mwenye subira na mpole; upendo wake wa ukombozi kamwe hauna mwisho na haushindwi.33 Atatusaidia kuishi maagano yetu na kukuza miito yetu kama wazee katika Israeli.

Na Baba atatubariki kwa vitu vyote vinavyohitajika kukamilisha azma Zake: “vitu … vyote vilivyo mbinguni na duniani, maisha na nuru, Roho na nguvu, iliyotumwa mbele kwa mapenzi ya Baba kupitia Yesu Kristo, Mwanaye.”34

Wakati nuru takatifu na nguvu vinatiririka kwenye maisha yetu vitu vitatu vya kimiujiza vinatokea:

Kwanza, tunaweza kuona! Kupitia ufunuo tunaanza kuona kama Yesu alivyomwona mwanamke: kupita mwonekano wa nje mpaka moyoni.35 Tunapoona kama Yesu anavyoona, Anatubariki kuwapenda wale tunaowatumikia kwa upendo Wake. Kwa usaidizi wake, wale tunaowahudumia watamwona Mwokozi na kuhisi upendo Wake.36

Pili, tuna nguvu za ukuhani! Tuna mamlaka na nguvu ya kutenda katika jina la Yesu Kristo “kubariki, kuongoza, kulinda, kuimarisha, na kuwaponya wengine na kuleta miujiza kwa wale [tunao] wapenda na kuweka ndoa [zetu] na familia salama.”37

Tatu,Yesu Kristo huenda pamoja nasi Kule tuendako, Yeye anakwenda. Wakati tunapofundisha, Yeye hufundisha. Wakati tunapofariji, Yeye hufariji Wakati tunapobariki,Yeye hubariki.38

Akina kaka, je, hatuna sababu ya kufurahia? Tunayo! Tunao ukuhani mtakatifu wa Mungu. Tunapomtegemea Yesu Kristo, kuishi maagano yetu, na kukaza fokasi yetu kwake, tutajumuika na dada zetu na kutumikia katika njia takatifu zaidi, kukusanya Israeli iliyotawanyika kutoka pande zote mbili za pazia, kuimarisha na kuunganisha familia zetu, na kuandaa ulimwengu kwa Ujio wa Pili wa Bwana Yesu Kristo. Itatokea. Nashuhudia hivyo.

Ninafunga kwa sala hii kutoka moyoni mwangu, kwamba sisi sote, kila mmoja, atamtegemea Yesu Kristo katika kila wazo. Usitie shaka.  Usiogope. Katika Jina la Yesu Kristo, amina.

Muhtasari

  1. James E. Talmage anamweka Yesu “jirani na Kapenaumu” wakati uponyaji wake ulopotakea (ona Yesu Kristo [1916], 313).

  2. Ona Luka 8:43–44; ona pia Mathayo 9:20–21; Marko 5:25–29.

  3. Luka 8:46.

  4. Marko 5:30.

  5. Marko 5:32.

  6. Luka 8:47.

  7. Marko 5:33.

  8. Luka 8:48.

  9. James E. Talmage aliandika kwamba cha thamani kuu kwa mwanamke kuliko uponyaji wa kimwili kilikuwa uthibitisho kwamba Mwokozi aliridhia matamanio ya moyo wake na kwamba imani yake ilikubaliwa na Yeye (ona Jesus the Christ, 318). Yesu alimponya kimwili na kiroho na alimfungulia njia ya wokovu.

  10. Ni cha kufundisha kwamba Jairo, mkuu wa sinagogi, alikuwa na Yesu wakati uponyaji huu ulipotokea. Yesu alikuwa njiani kwenda nyumbani kwa Jairo, ambako angemwinua binti wa Jairo kutoka kifo. Mwanamke ambaye Yesu alimponya alikuwa kwa vyovyote ametupwa nje ya sinagogi kwa sababu mateso yake. Wakati Yesu alipomponya, pia Aliweka wazi kwa wote waliokuwepo pale, ikiwa ni pamoja na Jairo, kwamba alikuwa binti mpendwa, mwanamke mwenye imani, na mzima katika mwili na roho.

  11. Ona D. Todd Christofferson, “Akidi ya Wazee” (Liahona, Mei 2018, 55–58) kwa ajili ya majadiliano ya marekebisho kuanzisha akidi moja ya ukuhani wa Melkizedeki katika kata. Lengo la badiliko hilo lilielezwa kwa njia hii katika sehemu ya Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara ya mtandao wa Kuhudumu: “kuwa na akidi moja ya Ukuhani wa Melkidezeki katika kata kunawaunganisha wenye ukuhani kukamilisha vipengele vyote vya kazi ya wokovu, ikiwa ni pamoja na hekalu na kazi ya historia ya familia ambazo awali zilisimamiwa na kiongozi wa kikundi cha makuhani wakuu” (“Huku ndiko Kuhudumu: Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara,” 8, ministering.ChurchofJesusChrist.org).

    Mabadiliko yanayofuatia yamemuweka kiongozi wa misheni wa kata na kiongozi mpya wa hekalu na historia ya familia katika kata chini ya maelekezoya urais wa akidi ya wazee. Kwa kuhudumia familia ambazo tayari ziko chini ya maelekezo ya urais, marekebisho haya yameweka uongozi wa kazi ya ukombozi katika akidi za wazee, zikisaidiwa na Muungano wa Usaidizi wa Akina Mama. Bila shaka, askofu anashikilia funguo za kazi ya wokovu katika kata, lakini ananaibisha majukumu na mamlaka kwa ajili ya kazi hiyo kwa rais wa akidi ya wazee ili kwamba askofu aweze kutumia muda mwingi kuhudumia familia yake mwenyewe, kuwaimarisha vijana, na kuhudumu kama mwamuzi katika Israeli

  12. Ona Russell M. Nelson, “Acha Tusonge Mbele,” Liahona , mei 2018, 118–19; Russell M. Nelson, “Kuwa Mtakatifu wa Siku za Mwisho wa Mfano,” Liahona, Nov. 2018, 113–14; Quentin L. Cook, “Uongofu wa Kina na wa Kudumu kwa Baba wa Mbinguni na Bwana Yesu Kristo,” Liahona, Nov. 2018, 8–12.

  13. Baba alimtuma Yesu Kristo ulimwenguni (ona Yohana 17:18).

  14. Mafundisho na Maagano 6:36–37.

  15. Ibrahimu 3:27.

  16. Ibrahimu 3:27.

  17. Musa 4:2

  18. Kuna marejeleo mengi katika maandiko ambayo yanaandika maelezo Yesu aliyosema kuhusu kufanya kazi ya Baba Yake na kufundisha mafundisho ya Baba Yake. Ona, kwa mfano, Yohana 5:19 (Yesu anafanya kile anachoona Baba akifanya); Yohana 5:36 (Baba alimpa mwanaye kazi ya kufanya); Yohana 8:26 (Yesu alifundisha kile alichopokea kutoka kwa Baba Yake); Yohana 14:28 (Yesu alitangaza, “Baba Yangu ni mkuu kuliko mimi”); 3 Nephi 11:32 (mafundisho Yake ni mafundisho Baba Yake aliyompa).

  19. Yohana 14:31.

  20. Yohana 8:29.

  21. Yohana 6:38; ona pia Yohana 5:30.

  22. Luka 22:42.

  23. Neno tegemea katika kifungu hiki (ona Mafundisho na Maagano 6:36–37) lina maana ambazo zinafanana na wito wa Bwana: kukabiliana (au kugeukia); kuelekeza umakini wa mtu kwenye; kutegemea; kutafuta kwa ajili ya; kungojea kwa matumaini; kuwa katika akili zetu kama mwisho; kutegemea au kutumainia (ona “tegemea,” Merriam-Webster.com).

  24. Ona Mafundisho na Maagano 121:41–42. Sifa kama za Kristo zilizotajwa katika maandiko ni karama za Roho ambazo zinakuja kupitia huruma na rehema ya Yesu Kristo. Ndivyo vinavyofanya wazee katika Israeli kuwa wazee Wake .

  25. Russell M, Nelson, “Kuvutia Nguvu ya Yesu Kristo kwenye Maisha Yetu,” Liahona, Mei 2017, 41.

  26. Ona merriam-webster.com, “kaza.”

  27. Kwa ajili ya mjadala juu ya suala la maisha ya agano, ona Donald L. Hallstrom, “Kuishi maisha ya agano,” Ensign, Juni 2013, 46–49. Makala hii ilirekebishwa kutoka mazungumzo marefu yaliyotolewa BYU– Idaho mwezi mei ya mwaka 2011. Kwa toleo refu, ona Donald L. Hallstrom, “Maisha ya Agano” (Ibada ya Chuo Kikuu cha Brigham Young–Idaho, Mei 10, 2011), byui.edu.

  28. Ona Yeremia 31:31–33, ambapo Bwana anatangaza kwamba atafanya agano jipya na nyumba ya Israeli lililoandikwa katika mioyo yao. Mfano wa maagano yaliyoandikwa katika mioyo yetu, au maagano ambayo yanakuja hai katika mioyo yetu, yanapatikana pia katika maandiko ya Paulo (ona 2 Wakorintho 3:3; Waebrania 8:10). Kwa majadiliano ya uongofu na moyo, ona DavidA. Bednar, “Kuongoka kwa Bwana,” Liahona Nov. 2012, 106–9.

  29. Sala ya sakramenti juu ya mkate inaelezea kwa uzuri asili ya uhusiano wa agano letu na Baba yetu wa Mbinguni. Katika mpango wa Baba wa wokovu, tunafanya maagano na Baba wa Mbinguni, lakini malengo ya maagano yanaeleweka na tunastahili kwa ajili ya baraka zilizoahidiwa kupitia Bwana Yesu Kristo; Yeye ni mpatanishi. Katika ibada ya sakramenti, tunashuhudia kwa Baba (kama matokeo, kufanya agano na Yeye upya) kwamba tupo tayari kujichukulia juu yetu jina la Yesu kristo, daima kumkumbuka Yeye, na kutii amri Zake, ambazo ametupa, ili daima Roho Wake (Roho Mtakatifu) apate kuwa pamoja nasi.

    Karama katika ahadi za Baba zinakuja kupitia nguvu ya kukomboa na kuimarisha ya Yesu Kristo. Kwa mfano, kama Rais Russell M. Nelson alivyofundisha,Yesu Kristo ni “chanzo cha furaha yote” (ona “Furaha na Kunusurika Kiroho,” Liahona Nov. 2016,82). Hivyo, kukaza kwa uimara fokasi yetu kwa Yesu Kristo kunaleta furaha ndani ya maisha yetu bila kujali hali zetu.

  30. Rais Ezra Taft Benson alinasa athari ya badiliko hili katika mtazamo na mwelekeo wa mazingira aliposema, “Wakati utii unapokoma kukera na kuwa uhitaji wetu, katika muda ule Mungu atatujalia nguvu” (katika Donald l. Staheli, “Utii—Changamoto Kuu ya Maisha,” Ensign, mei 1998, 82).

  31. Yohana 16:32.

  32. Kwa nyongeza ya majadiliano ya ukweli wa Baba na wa Mwana kuhusu kwa ajili ya, shauku katika, upendo kwa ajili, na kujihusisha katika maisha yetu, ona Jeffrey R, Holland, “Ukuu wa Mungu,” Liahona, Nov. 2003, 70–73; Henry B. Eyring, “Tembea Nami,” Liahona, May 2017, 82–85. Ona pia Mathayo 18:20; 28:20; Mafundisho na Maagano 6:32; 29:5; 38:7; 61:36; 84:88.

  33. Ona Warumi 08:35–39; 1 Wakorintho 13:1–8; Moroni 7:46–47.

  34. Mafundisho na Maagano 50:27. Fahamu kwamba Bwana hutoa kwa wote walio tawazwa na kupeleka ahadi hii ambayo inahusiana na, na imewekewa mipaka na, jukumu maalumu alilopewa:

    “Huyo ndiye ameteuliwa kuwa mkuu, bila kujali kuwa yeye ni mdogo na mtumishi wa wote.

    “Kwa hiyo, yeye ni mmiliki wa vitu vyote; kwani vitu vyote viko chini yake, kote mbinguni na duniani, uzima na nuru, Roho na nguvu, ametumwa kwa mapenzi ya Baba kupitia Mwana wake, Yesu Kristo..

    “Lakini hakuna mwanadamu aliye mmiliki wa vitu vyote isipokuwa yule aliye takaswa na kuoshwa dhambi zote.

    “Na kama umetakaswa na kuoshwa kutokana na dhambi zote, utaomba kitu chochote utakacho katika jina la Yesu nalo litafanyika” (Mafundisho na Maagano 50:26–29).

  35. Ona 1 Samweli 16:7; 1 Wakorintho 2:14. Kwa mfano wa baraka hii ya kuona kama Yesu anavyoona, ona maelezo ya Rais Henry B. Eyring ya uzoefu wake kama askofu wa kijana aliyefanya uhalifu. Bwana alisema kwa aliyekuwa Askofu Eyring, “Nitakuruhusu umwone kama mimi ninavyomuona” (“Tembea Nami,” 84).

  36. Hii ni ahadi na agizo Mwokozi alilowapa watu kwenye hekalu pale Bountiful. Aliwaamuru kuishi hivyo ili kwamba nuru Yake na mfano Wake vingekuwa ndani yao, ili kwamba wangeweza Kumwinua juu kama nuru kwa ulimwengu katika maisha yao na katika mialiko yao kwa wengine kuja Kwake. Kama wafuasi Wake wangeishi hivyo na kualika hivyo, wengine wangemhisi na kumwona Yeye katika watumishi wa Bwana. (Ona 3 Nefi 18:24–25.)

  37. Ona Russell M. Nelson, “Gharama ya Nguvu za Ukuhani,” Liahona, Mei 2016, 68.

  38. Ona Mafundisho na Maagano 84:88.

Chapisha