Mkutano Mkuu
Ndani ya Kina cha Mioyo Yetu
Mkutano mkuu wa Aprili 2020


Ndani ya Kina cha Mioyo Yetu

Bwana anajaribu kutusaidia—sisi sote—kupata injili Yake ndani ya kina cha mioyo yetu.

Akina dada na akina kaka, tunaishi katika wakati wa kupendeza sana hivi sasa. Tunaposherehekea mwanzo wa Urejesho, inafaa pia kusherehekea Urejesho unaoendelea ambao tunaushuhudia. Ninafurahia pamoja na wewe kuishi katika siku hii.1 Bwana anaendelea kuweka yote pamoja, kupitia manabii Wake, yote ambayo yanahitajika kutusaidia kujiandaa kumpokea Yeye.2

Mojawapo ya vitu hivyo vinavyohitajika ni mpango mpya wa Watoto na Vijana. Wengi wenu mnajua mkazo wa programu hii kwenye kuweka malengo, nembo mpya za kuwa sehemu ya, na mikutano ya Kwa Nguvu ya Vijana. Lakini hatupaswi kuruhusu hayo yazibe mtazamo wetu juu ya kanuni ambazo kwazo programu hii imejengwa na malengo yake: kusaidia kupata injili ya Yesu Kristo ndani ya kina cha mioyo ya watoto na vijana wetu.3

Ninaamini tunapofahamu kanuni hizi kwa uwazi zaidi, tutaona hii kama zaidi ya programu ya washiriki wa miaka 8 hadi 18. Tutaona jinsi Bwana anavyojaribu kutusaidia—sisi sote—kupata injili Yake kwa kina ndani ya mioyo yetu. Ninaomba Roho Mtakatifu atusaidie kujifunza pamoja.

Mahusiano—“Kuwa pamoja Nao”4

Kanuni ya kwanza ni mahusiano. Kwa sababu wao ni sehemu ya asili ya Kanisa la Yesu Kristo, wakati mwingine tunasahau umuhimu wa mahusiano katika safari yetu endelevu kwa Kristo. Hatutegemewi kupata au kutembea njia ya agano peke yake. Tunahitaji upendo na msaada kutoka kwa wazazi, wanafamilia wengine, marafiki, na viongozi ambao pia wako kwenye njia.

Aina hizi za mahusiano huchukua muda. Muda wa kuwa pamoja. Muda wa kucheka, kucheza, kujifunza na kutumikia pamoja. Muda wa kuthamini masilahi na changamoto za kila mmoja. Muda wa kuwa wawazi na waaminifu kwa kila mmoja pale tunapojitahidi kuwa bora pamoja. Mahusiano haya ni moja ya malengo ya kukusanyika kama familia, akidi, madarasa, na mikutano. Haya ni msingi wa huduma madhubuti.5

Mzee Dale G. Renlund alitupa ufunguo wa kukuza mahusiano haya wakati aliposema: “Ili kuwatumikia wengine vizuri lazima tuwaone … kupitia macho ya Baba wa Mbingu. Ni hapo tu ndipo tunaweza kuelewa thamani halisi ya nafsi. Ni hapo tu ndipo tunaweza kuhisi upendo alionao Baba wa Mbinguni kwa watoto Wake wote.”6

Kuwaona wenzetu kama vile Mungu anavyowaona ni kipawa. Ninawaalika kila mmoja wetu kutafuta kipawa hiki. Wakati macho yetu yamefunguliwa kuona,7 tutaweza pia kuwasaidia wengine kujiona kama Mungu anavyowaona.8 Rais Henry B. Eyring alisisitiza nguvu ya hili wakati aliposema: “Kilicho muhimu zaidi ni nini [wengine] wanachojifunza kutoka [kwako] juu ya wao ni nani hasa na kile hasa wanachoweza kuwa. Nadhani kwamba hawatajifunza mengi kuhusu hilo kutoka kwenye mihadhara. Watakipata kutokana na hisia za wewe ni nani, unadhani wao ni akina nani, na kile unachodhani wanaweza kuwa.”9 Kuwasaidia wengine kuelewa utambulisho wao wa kweli na lengo lao halisi ni moja ya zawadi kubwa tunazoweza kutoa.10 Kuwaona wengine na sisi wenyewe vile Mungu anavyotuona huunganisha mioyo yetu “kwa pamoja katika umoja na katika upendo.”11

Kwa nguvu za ulimwengu zinazoongezeka kila wakati kutuvuta, tunahitaji nguvu inayotokana na mahusiano ya upendo. Kwa hivyo tunapopanga shughuli, mikutano, na mikusanyiko mingine, hebu tukumbuke kusudi kuu la mikusanyiko hii ni kujenga mahusiano ambayo hutuimarisha na kusaidia kupata injili ya Yesu Kristo ndani ya kina cha mioyo yetu.12

Ufunuo, Haki ya kujiamulia, na Toba—“Waunganishe na Mbingu”13

Kwa kweli, haitoshi tu kufungwa pamoja. Kuna vikundi na mashirika mengi ambayo yanafikia umoja kupitia sababu tofauti. Walakini umoja tunaotafuta ni kuwa wamoja katika Kristo, kujiunganisha sisi pamoja na Yeye.14 Ili kuunganisha mioyo yetu na mbingu, tunahitaji uzoefu binafsi wa kiroho, kama vile Mzee Andersen alivyotoka kutuzungumzia hilo kwa ushawishi.15 Uzoefu huo huja wakati Roho Mtakatifu anapopeleka neno na upendo wa Mungu kwenye akili na mioyo yetu.16

Ufunuo huu unakuja kupitia maandiko, hasa Kitabu cha Mormoni; kupitia maneno yenye msukumo wa Kiungu kutoka kwa manabii walio hai na wafuasi wengine waaminifu; na kupitia sauti ndogo, tulivu.17 Maneno haya ni zaidi ya wino kwenye ukurasa, mawimbi ya sauti kwenye masikio yetu, mawazo katika akili zetu, au hisia katika mioyo yetu. Neno la Mungu ni nguvu ya kiroho.18 Ni ukweli na nuru.19 Ni jinsi tunavyomsikia! Neno linaanzisha na kuongeza imani yetu kwa Kristo na linachochea ndani yetu hamu ya kuwa kama Mwokozi—ambayo ni, kutubu na kutembea njia ya agano.20

Aprili mwaka jana, Rais Russell M. Nelson alitusaidia kuelewa jukumu kuu la toba katika safari hii iliyofunuliwa.21 Alisema: “Tunapochagua kutubu, tunachagua kubadilika! Tunamruhusu Mwokozi kutubadilisha kuwa toleo bora zaidi la sisi wenyewe. … Tunachagua kuwa zaidi kama Yesu Kristo!”22 Mchakato huu wa badiliko, unaochochewa na neno la Mungu, ndivyo jinsi tunavyoungana na mbingu.

Msingi wa mwaliko wa Rais Nelson wa kutubu ni kanuni ya haki ya kujiamulia. Tunapaswa kuchagua toba sisi wenyewe. Injili haiwezi kulazimishwa kuingia kwenye mioyo yetu. Kama Mzee Renlund alivyosema, “Lengo la Baba yetu wa Mbinguni katika malezi sio kuwafanya watoto Wake wafanye yaliyo sahihi; ni kufanya watoto wake wachague kufanya yaliyo sahihi.”23

Katika programu iliyobadilishwa na watoto na Vijana, kulikuwa na mahitaji tofauti zaidi ya 500 ya kukamilisha ili kupokea utambulisho mbali mbali.24 Leo, kimsingi kuna moja. Ni mwaliko wa kuchagua kuwa zaidi kama Mwokozi. Tunafanya hivi kwa kupokea neno la Mungu kupitia Roho Mtakatifu na kumruhusu Kristo atubadilishe kuwa “toleo bora zaidi la sisi wenyewe.”

Hii ni zaidi ya mazoezi ya kuweka malengo au kujiboresha. Malengo ni nyenzo tu ambayo hutusaidia kuungana na mbingu kupitia ufunuo, haki ya kujiamulia, na toba—kuja kwa Kristo na kupokea injili yake kwa kina ndani ya mioyo yetu.23

Ushiriki na Dhabihu—“Waruhusu Wao Waongoze”25

Mwishowe, ili kupata injili ya Yesu Kristo ndani ya kina cha mioyo yetu, tunahitaji kujihusisha nayo—kutoa muda wetu na talanta zetu kwa ajili yake, kutoa dhabihu kwa ajili yake.26 Sote tunataka kuishi maisha ya maana, na hii ni kweli hasa kwa kizazi kinachoinukia. Wanatamani kusudi.

Injili ya Yesu Kristo ndilo kusudi kuu zaidi ulimwenguni. Rais Ezra Taft Benson alisema: “Tumeamriwa na Mungu kuchukua injili hii kwa ulimwengu wote. Hilo ndilo kusudi ambalo lazima lituunganishe leo. Injili tu ndiyo itaokoa ulimwengu kutokana na janga la kujiangamiza wenyewe. Injili tu ndiyo itawaunganisha wanaume [na wanawake] wa kila kabila na mataifa kwa amani. Injili tu ndiyo italeta furaha, shangwe na wokovu kwa familia ya binadamu.”27

Mzee David A. Bednar aliahidi, “Tunapowawezesha vijana kwa kuwaalika na kuwaruhusu kuchukua hatua, Kanisa litasonga mbele kwa njia za kimiujiza.”28 Mara nyingi hatujawaalika na kuwaruhusu vijana kujitolea kwa kusudi hili kuu la Kristo. Mzee Neal A. Maxwell alisema, “Ikiwa vijana [wetu] wamelemewa na [kazi ya Mungu], wana uwezekano mkubwa wa kulemewa na ulimwengu.”29

Programu ya Watoto na Vijana inafokasi kwenye kuwawezesha vijana. Wanachagua malengo yao wenyewe. Urais wa akidi na madarsa huwekwa katika majukumu yao sahihi. Baraza la vijana la kata, kama vile baraza la kata, linafokasi kwenye kazi ya wokovu na kuinuliwa.30 Na akidi na madarasa huanza mikutano yao kwa kushauriana juu ya jinsi ya kufanya kazi ambayo Mungu amewapa.31

Rais Nelson aliwaambia vijana wa Kanisa: “Ukichagua, ikiwa unataka, … unaweza kuwa sehemu kubwa ya kitu kikubwa, kitu kizuri, kitu adhimu! … Wewe ni miongoni mwa bora zaidi ambao Bwana amewahi kuwaleta kwenye ulimwengu huu. Una uwezo wa kuwa nadhifu na mwenye busara na una athari zaidi juu ya ulimwengu kuliko kizazi chochote kilichopita!”32 Katika hafla nyingine, Rais Nelson aliwaambia vijana: “Nina ujasiri kamili kwenu. Ninawapenda na Bwana pia anawapenda. Sisi ni watu Wake, tuliojiunga pamoja katika kazi Yake takatifu.”33 Vijana, je! Mnaweza kuhisi imani ambayo Rais Nelson anayo kwenu na jinsi gani mlivyo muhimu katika kazi hii?

Wazazi na viongozi watu wazima, ninawaombeni muwaone vijana kama Rais Nelson anavyowaona. Wakati vijana wanapohisi upendo wako na imani yako, unapowahimiza na kuwafundisha jinsi ya kuongoza—na kisha kutoka kwenye njia yao—watakushangaza kwa ufahamu wao, uwezo wao, na kujitolea kwao kwenye injili.34 Watasikia furaha ya kuchagua kujihusisha na kujitolea kwa ajili ya kusudi la Kristo. Injili Yake itaingia ndani ya kina cha mioyo yao, na kazi itasonga mbele kwa njia za kimiujiza.

Ahadi na Ushuhuda

Ninaahidi, tunapofokasi kwenye kanuni hizi—mahusiano, ufunuo, haki ya kujiamulia, toba, na dhabihu—injili ya Yesu Kristo itazama ndani ya kina cha mioyo yetu sote. Tutaona Urejesho ukisonga mbele hadi kwenye kusudi lake la mwisho, ukombozi wa Israeli na kuanzishwa kwa Sayuni,35 ambapo Kristo atatawala kama Mfalme wa wafalme.

Ninashuhudia kwamba Mungu anaendelea kufanya vitu vyote muhimu kuandaa watu wake kwa ajili ya siku hiyo. Na tuuone mkono wake katika kazi hii tukufu pale sote tunapojitahidi “kuja kwa Kristo, na kufanywa kamili ndani yake.”36 Katika Jina la Yesu Kristo, amina.

Muhtasari

  1. Ona Mafundisho na Maagano 45:12. Rais Nelson alisema: “Fikiria tu juu ya shangwe na umuhimu wake wote: kila nabii akianza na Adamu ameona siku yetu. Na kila nabii ameongea kuhusu siku yetu , wakati Israeli itakapokusanywa na ulimwengu kutayarishwa kwa Ujio wa Pili wa Mwokozi. Fikiria hilo! Kati ya watu wote ambao wamewahi kuishi katika sayari ya dunia, sisi ni moja ya wale tunaopata nafasi ya kushiriki katika tukio hili la mwisho, la mkusanyiko mkuu. Ni ya kupendeza kiasi gani!” (“Hope of Israel” [worldwide youth devotional, June 3, 2018], HopeofIsrael.ChurchofJesusChrist.org).

    Mzee Jeffrey R. Holland alifundisha:

    “Ni wakati wa kuvutia kiasi gani kuwa hai!

    “Injili ya Yesu Kristo ni uhakika mkuu, usalama zaidi, inayopatikana zaidi, na ukweli wenye tunu kubwa duniani na mbinguni, kwa muda na katika umilele. Hakuna chochote—si chochote, si yeyote, si ushawishi wowote—utazuia Kanisa hili kutimiza kazi yake na kutambua takdiri yake iliyotangazwa tangu kabla ya msingi wa ulimwengu. … Hakuna sababu ya kuogopa au kuwa na wasiwasi kuhusu wakati ujao.

    “Tofauti na nyakati zingine kabla yetu, kipindi hiki cha maongozi ya Mungu hakitapitia ukengeufu wa kitaasisi; hakitaona upotevu wa funguo za ukuhani; hakitateseka kukosekana kwa ufunuo kutoka kwenye sauti ya Mwenyezi Mungu. … Ni wakati wa kusisimua kuwa hai!

    “… Ikiwa hujagundua, nina ujasiri kuhusu siku za mwisho. … Amini. Inuka. Kuwa mwaminifu. Na tumia vizuri siku ambayo ndani yake tunaishi!” (Facebook post, Mei 27, 2015; ona pia “Usiogope, Amini Tu” [address to Church Educational System Religious Educators, Feb. 6, 2015], broadcasts.lds.org).

  2. Ona Yohana 1:12.

  3. Muda mfupi baada ya kuitwa kama Urais Mkuu wa Wavulana, Rais Henry B. Eyring alijadili nasi changamoto za kipekee na fursa ambazo vijana wa Kanisa hili wanakabiliana nazo leo. Alitushauri kufokasi kwenye vitu vile ambavyo vitasaidia kufikisha injili ya Yesu Kristo ndani ya kina cha mioyo yao. Ushauri huo umekuwa alama kwetu kama Urais wa Wavulana.

  4. Ona “Be with Them,” ChurchofJesusChrist.org/callings/aaronic-priesthood-quorums/my-calling/leader-instruction/be-with-them.

  5. Ona Mosia 18:25; Moroni 6:5.

  6. Dale G. Renlund, “kupitia Macho ya Mungu,” Liahona, Nov. 2015, 94; ona pia Musa 1:4–6.

    Rais Thomas S. Monson alifundisha: “Tuna jukumu la kuwaona wengine si kama jinsi walivyo lakini kama wanavyoweza kuwa. Ninawasihi muwafikirie kwa njia hii” (“Waone Wengine jinsi Wanavyoweza Kuwa,” Liahona, Nov. 2012, 70).

    Mzee Neal A. Maxwell alifundisha: “Mara nyingi, mwonekano wa nje wa kijana usiolandana na viwango vya Kanisa, au maswali yake yanayoonekana kama ya kupinga, au mashaka yake yaliyoonyeshwa humfanya abandikwe jina haraka. Matokeo yanaweza kuwa umbali na, wakati mwingine, kutokuwa na maelewano. Upendo wa kweli haupendi kubandika majina!” (“Kwa Kizazi Kinachoinukia,” Ensign, Apr. 1985, 9).

  7. Ona 2 Wafalme 6:17.

  8. Stephen L. Richards, kama mshiriki wa Urais wa Kwanza, alisema: “The highest type of discernment is that which perceives in others and uncovers for them their better natures, the good inherent within them” (in Conference Report, Apr. 1950, 162; in David A. Bednar, “Quick to Observe,” Ensign, Des. 2006, 35; Liahona, Dec. 2006, 19). Ona pia 2 Wafalme 6:17.

  9. Henry B. Eyring, “Teaching Is a Moral Act” (address at Brigham Young University, Aug. 27, 1991), 3, speeches.byu.edu; msisitizo umeongezwa; ona pia Henry B. Eyring, “Help Them Aim High,” Liahona, Nov. 2012, 60–67.

  10. Ona Musa 1:3–6.

  11. Mosia 18:21; ona pia Musa 7:18.

  12. “Vijana ambao wana uhusiano madhubuti, na mzuri na familia inayoshiriki kikamilifu [Watakatifu-wa Siku za Mwisho], marafiki, na viongozi, ambao huwasaidia kukuza mahusiano na Baba yao wa Mbinguni, wana uwezekano mkubwa wa kuendelea kushiriki kikamilifu. Vipengele maalum vya programu—kama vile mtaala wa Jumapili, programu ya shughuli za [Wavulana], matarajio ya mafanikio binafsi … yanaweza kuwa na athari kidogo bila ya mahusiano hayo. … Swali muhimu sio jinsi vipengele maalum vya programu vinavyotekelezwa, lakini ni jinsi gani vinachangia kwenye mahusiano mazuri ambayo huimarisha utambulisho wa kidini wa wavulana [Watakatifu wa Siku za Mwisho] ” (“Be with Them,” ChurchofJesusChrist.org/callings/aaronic-priesthood-quorums/my-calling/leader-instruction/be-with-them).

  13. Ona “Connect Them with Heaven,” ChurchofJesusChrist.org/callings/aaronic-priesthood-quorums/my-calling/leader-instruction/connect-them-with-heaven.

  14. Ona Yohana 15:1–5; 17:11; Wafilipi 4:13; 1 Yohana 2:6; Yakobo 1:7; Omni 1:26; Moroni 10:32.

  15. Maandiko yamejaa mifano ya hili; hapa ni miwili tu: 1 Nefi 2:16; Enoshi 1:1–4.

  16. Ona Luka 24:32; 2 Nefi 33:1–2; Yakobo 3:2; Moroni 8:26; Mafundisho na Maagano 8:2–3.

  17. Ona 2 Timotheo 3:15–16; Mafundisho na Maagano 68:3–4; 88:66; 113:10.

  18. Ona 1 Wathesalonike1:5; Alma 26:13; 31:5; Helamani 3:29; 5:17; Mafundisho na Maagano 21:4–6; 42:61; 43:8–10; 50:17–22; 68:4.

  19. Ona Yohana 6:63; 17:17; Alma 5:7; Mafundisho na Maagano 84:43–45; 88:66; 93:36.

  20. Ona Yohana 15:3; 1 Petro 1:23; Mosia 1:5; Alma 5:7, 11–13; 32:28, 41–42; 36:26; 62:45; Helamani 14:13.

  21. Ona 2 Nefi 31:19–21; 32:3, 5.

  22. Russell M. Nelson, “Tunaweza Kufanya Vizuri Zaidi na Kuwa Wazuri Zaidi,” Liahona, Mei 2019, 67.

  23. Dale G. Renlund, “Chagueni Hivi Leo,” Liahona, Nov. 2018, 104.

  24. Idadi hii ni pamoja na mahitaji ya programu ya Skauti, ambayo hadi hivi karibuni ilikuwa sehemu ya programu ya shughuli za Kanisa kwa vijana na wavulana, hasa huko Marekani na Canada. Katika maeneo ambayo hayakuhusika katika Skauti, idadi ya mahitaji ilikuwa zaidi ya 200. Kwa kuongezea, programu mbali mbali za shughuli za wavulana, wasichana, vijana wa kiume, na mabinti wadogo ziliundwa tofauti, ikifanya uzoefu wote kuwa mgumu zaidi kwa familia.

  25. Ona “Let Them Lead,” ChurchofJesusChrist.org/callings/aaronic-priesthood-quorums/my-calling/leader-instruction/let-them-lead.

  26. Ona Omni 1:26; 3 Nefi 9:20; 12:19; Mafundisho na Maagano 64:34. “Dini ambayo haihitaji dhabihu ya vitu vyote haina nguvu ya kutosha kuzaa imani muhimu katika maisha na wokovu.” (Mihadhara ya Imani [1985], 69).

  27. Ezra Taft Benson, The Teachings of Ezra Taft Benson (1988), 167; katika Preach My Gospel: A Guide to Missionary Service (2019), 13; ona pia Russell M. Nelson, “Hope of Israel,” HopeofIsrael.ChurchofJesusChrist.org.

  28. Mkutano na Mzee David A. Bednar; ona pia “2020 Temple and Family History Leadership Instruction,” Feb. 27, 2020, ChurchofJesusChrist.org/family-history.

  29. Neal A. Maxwell, “Kwa Kizazi Kinachoinukia,”, 11. Mzee Maxwell aliendelea: “Kwa kweli, ni idadi kiasi gani ya urais wa akidi za mashemasi na waalimu inajumuisha zaidi tu ya kumwita mtu asali au kupitisha sakramenti? Ndugu, hizi ni roho maalum, na zinaweza kufanya mambo ya maana ikiwa zitapewa nafasi!”

  30. Ona General Handbook: Serving in The Church of Jesus Christ of Latter-day Saints, 2.2, ChurchofJesusChrist.org.

  31. Nyenzo kadhaa zinapatikana katika Maktaba ya Injili ili kuwasaidia vijana kuongoza, ikiwa ni pamoja na “Nyenzo za Urais wa Akidi na Darasa,” “Kutumia Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Ukuhani wa Haruni na Madarasa ya Wasichana,” na katika nyenzo za wasichana na akidi za Ukuhani wa Haruni katika “Miito ya Kata au Tawi.”

  32. Russell M. Nelson, “Hope of Israel,” HopeofIsrael.ChurchofJesusChrist.org. Wakati wa ibada hiyo hiyo, Rais Nelson alisema: “Baba Yetu wa Mbinguni amehifadhi wengi wa roho zake wazuri—labda, naweza kusema, timu Yake bora zaidi—kwa ajili ya awamu hii ya mwisho. Roho hizo nzuri—wachezaji hao bora, hao mashujaa—ni wewe!”

  33. Russell M. Nelson, maneno ya ufunguzi katika “Watoto na Vijana: Tukio la Uso kwa Uso na Mzee Gerrit W. Gong,” Nov. 17, 2019, broadcasts.ChurchofJesusChrist.org.

  34. Rais Nelson alisema “Tunahitaji kuwaruhusu vijana waongoze, hasa wale ambao wameitwa na wametengwa ili kutumika darasani na kuhudumu kwenye akidi za urais. Mamlaka ya Ukuhani yatakuwa yamegawiwa kwao. Watajifunza jinsi ya kupata msukumo katika kuongoza darasa au akidi yao” (katika “Children and Youth Introductory Video Presentation,” Sept. 29, 2019, ChurchofJesusChrist.org).

    Mzee Quentin L. Cook alisema, “Vijana wetu wanaombwa kuchukua majukumu zaidi binafsi katika umri mdogo—bila wazazi na viongozi kufanya kile ambacho vijana wanaweza kufanya wao wenyewe” (“Marekebisho ya Kuimarisha Vijana,” Liahona, Nov. 2019, 40).

  35. Rais George Q. Cannon alifundisha: “Mungu amehifadhi roho kwa ajili ya kipindi hiki cha maongozi ya Mungu ambazo zina ujasiri na ari ya kukabiliana na ulimwengu, na nguvu zote za mwovu, zinazoonekana na zisizoonekana, kutangaza injili na kuendeleza ukweli na kuanzisha na kuijenga Sayuni ya Mungu wetu bila kuhofia matokeo. Amezileta roho hizi katika kizazi hiki ili kuuweka msingi wa Sayuni usishindwe kamwe, na kuinua uzao ambao utakuwa wa haki, na ambao utamuheshimu Mungu, na kumuheshimu Yeye kwa ukuu, na kuwa watiifu Kwake katika hali zozote” (“Remarks,” Deseret News, Mei 31, 1866, 203); ona pia Teachings of Presidents of the Church: Joseph Smith (2007), 186.

  36. Moroni 10:32.

Chapisha