Mkutano Mkuu
Stahimili Siku katika Kristo
Mkutano mkuu wa Oktoba 2023


Stahimili Siku katika Kristo

Yesu Kristo hufanya iwezekane kwa ajili yetu “kustahimilli siku.”

Ilikuwa ni siku iliyojaa mifano mahsusi na ya moja kwa moja, maswali magumu na mafundisho mazito. Baada ya kutoa karipio kali kwa wale ambao walikuwa kama “makaburi yaliyopakwa chokaa, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa mifupa ya wafu, na uchafu wote,”1 Yesu alifundisha mifano mitatu zaidi kuhusu maandalizi ya kiroho na ufuasi. Mojawapo ya hii ilikuwa mfano wa wanawali kumi.

“Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofananishwa na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana harusi.

“Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara.

“Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao:

“Bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao.

“Hata bwana harusi alipokawia, wote wakalala usingizi.

“Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana harusi; tokeni mwende kumlaki.

“Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.

“Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.

“Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.

“Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana harusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye harusini; mlango ukafungwa.

“Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.”2

“Akajibu akasema, Amin, nawaambia, hamkunijua ninyi.”3

Kesheni kwa sababu hamjui siku wala saa wakati Mwana wa Adamu atakapokuja.”4

Rais Dallin H. Oaks aliuliza maswali yafuatayo ya kuchochoea mawazo kuhusiana na kuja kwa Bwana harusi:5 “Ingekuwaje kama siku ya ujio Wake ni kesho? Kama tungejua kwamba tungekutana na Bwana kesho—kupitia kifo chetu katika umri mdogo au kupitia ujio Wake usiotarajiwa —je tungefanya nini leo?”6

Nimejifunza kutokana na uzoefu binafsi kwamba maandalizi ya kiroho kwa ajili ya ujio wa Bwana si tu muhimu bali ndiyo njia pekee ya kupata amani na furaha.

Ilikuwa siku ya majira ya kiangazi kikavu niliposikia kwa mara ya kwanza maneno “Wewe una saratani.” Mimi pamoja na mume wangu tulipigwa na butwaa! Tulipokuwa tukirudi nyumbani, kimya kimya tukifikiria habari hizo, moyo wangu uliwageukia wana wetu watatu.

Akilini mwangu nilimuuliza Baba wa Mbinguni, “Je, nitakufa?”

Roho Mtakatifu alininong’oneza, “Kila kitu kitakuwa SAWA.”

Kisha nikauliza, “Je, nitaishi?

Tena, jibu likaja: “Kila kitu kitakuwa SAWA.”

Nilikanganyikiwa. Kwa nini nilipokea jibu lile lile ikiwa ningeishi au ningekufa?

Kisha ghafla kila kiungo cha mwili wangu kilijawa na amani kamili pale nilipokumbushwa: Hatukuhitaji kuharakisha kwenda nyumbani na kuwafundisha watoto wetu jinsi ya kusali. Walijua jinsi ya kupokea majibu na faraja kutoka kwenye sala. Hatukuhitaji kuharakisha kwenda nyumbani na kuwafundisha wao kuhusu maandiko au maneno ya manabii walio hai. Maneno hayo tayari yalikuwa chanzo cha kawaida cha nguvu na uelewa. Hatukuhitaji kuharakisha kwenda nyumbani na kuwafundisaha wao kuhusu toba, Ufufuo, Urejesho, mpango wa wokovu, familia za milele au hata mafundisho ya Yesu Krisro.

Kwa wakati huo kila somo la jioni ya familia nyumbani, kikao cha kujifunza maandiko, sala ya imani iliyotolewa, baraka zilizotolewa, ushuhuda uliotolewa, agano lililofanywa na kutunzwa, nyumba ya Bwana iliyohudhuriwa na siku ya Sabato iliyotunzwa vilikuwa na maana—ee, ni jinsi gani kila kimoja kilikuwa na maana! Hatukuwa tena na muda wa kutia mafuta kwenye taa zetu. Tulihitaji kila tone moja, na tulilihitaji papo hapo!

Kwa sababu ya Yesu Kristo na injili Yake iliyorejeshwa, kama ningekufa, familia yangu ingefarijiwa, ingeimarishwa na siku moja kurejeshwa. Kama ningeishi, ningepata nguvu kuu sana hapa duniani ili kusaidia kunifariji, kunihimili na kuniponya. Mwisho, kwa sababu ya Yesu Kristo, kila kitu kinaweza kuwa SAWA.

Tunajifunza kutoka kwenye mafunzo makini ya Mafundisho na Maagano neno “SAWA” linachomaanisha:

“Na siku ile, wakati nitakapokuja katika utukufu wangu, ndipo mfano utakapotimia ambao nilisema juu ya wanawali kumi.

Kwani wale walio na hekima na kupokea ukweli, na kumchukua Roho Mtakatifu kuwa kiongozi wao, na hawajadanganyika—amini ninawaambia, hawatakatiliwa chini na kutupwa katika moto, bali watastahimili siku ile.”7

Yesu Kristo hufanya iwezekane kwa ajili yetu “kustahimilli siku.” Kustahimili siku haimaanishi kuongezea kwenye orodha inayoongezeka ya vitu vya kufanya. Fikiria kuhusu lenzi ya kukuzia. Dhumuni lake hasa si tu kufanya vitu vionekane kuwa vikubwa. Pia inaweza kukusanya mwanga na kuufanya kuwa na nguvu zaidi. Tunahitaji tu, kufokasi juhudi zetu na kuwa wakusanyaji wa Nuru ya Yesu Kristo. Tunahitaji uzoefu mtakatifu zaidi na wa ufunuo.

Huko kaskazini magharibi Ya Israeli, kuna safu ya mlima wa kupendeza na mara nyingi unajulikana kama “mlima wa kijani kibichi.” Mlima Carmel8 ni wa kijani mwaka mzima kutokana na matone madogo ya umande kwa sehemu kubwa. Kulishwa hufanyika kila siku. Kama vile “umande wa Carmel,9 tunapotafuta kulisha nafsi zetu “vitu vinavyohusu utakatifu,”10 “vitu vidogo na rahisi,”11 shuhuda zetu na shuhuda za watoto wetu zitakuwa hai!

Sasa, unaweza kuwa unafikiria, “Lakini Dada Wright, hauijui familia yangu. Sisi tunahangaika kweli na wala hatuko hivi.” Uko sahihi. Mimi siijui familia yako. Lakini Mungu kwa upendo usio na kikomo, rehema, nguvu, maarifa na utukufu anaijua.

Maswali unayoweza kuwa unauliza ni maswali ya moyo ambao unauma katika kina cha nafsi yako. Maswali kama hayo yanapatikana katika maandiko matakatifu:

“Mwalimu, si kitu kwako kuwa [familia yangu] tunaangamia?”12

“Tumaini langu li wapi?”13

“[Nifanye] nini, ili hili wingu la giza liweze kuondolewa kwamba lisinifunike [mimi]?”14

“Bali hekima itapatikana wapi? Na mahali pa ufahamu ni wapi?”15

“Inawezekanaje kwamba [mimi] nishikilie kila kitu kizuri?”16

“Bwana, ungetaka nifanye nini?”17

Na kisha kwa uzuri sana yaja majibu:

“Je, unaziamini nguvu za wokovu za Kristo?”18

“Je, Bwana amewaamuru wowote wasipokee wema wake?”19

“Mnaamini kwamba [Yeye] anaweza kufanya hili?”20

“Je! unawaamini manabii?”21

“Je, mnaweka imani yenu ya ukombozi kwa yule aliyewaumba?”22

“Je, mhukumu ulimwengu wote atakosa kutenda haki?”23

Rafiki zangu wapendwa, sisi hatuwezi kugawa mafuta yetu, lakini tunaweza kushiriki nuru Yake. Mafuta katika taa zetu hayatatusaidia tu “kustahimili siku” bali yanaweza pia kuwa njia ya kuangaza njia ambayo inawaongoza wale tunaowapenda hadi kwa Mwokozi, ambaye anasimama tayari “kwa mikono wazi kuwapokea” wao.24

“Bwana asema hivi; Zuia sauti yako, usilie, na macho yako yasitoke machozi; Maana kazi yako itapata thawabu, … nao watakuja tena kutoka nchi ya adui.

“Tena liko tumaini kwa siku zako za mwisho, asema Bwana; na watoto wako watarejea hata mpaka wao wenyewe.”25

Yesu Kristo ndiye “tumaini kwa siku zako za mwisho.” Hakuna chochote tulichonacho, au tusichonacho, kilicho mbali na mfiko Wake usio na mwisho na dhabihu Yake ya milele. Yeye ndiye sababu ya kwa nini kamwe si mwisho wa hadithi yetu.26 Kwa hivyo sisi, “lazima tusonge mbele tukiwa na imani imara katika Kristo, tukiwa na mngʼaro mkamilifu wa tumaini, na upendo kwa Mungu na wanadamu wote. Kwa hivyo, kama [sisi] tutasonga mbele, tukila na kusherekea neno la Kristo, na tuvumilie hadi mwisho, tazama, hivi ndivyo asema Baba: [Sisi] tutapokea uzima wa milele.”27

Uzima wa milele ni shangwe ya milele. Shangwe katika maisha haya, sasa hivi—si kwa sababu ya changamoto za siku yetu bali kwa sababu ya msaada wa Bwana ili kujifunza kutoka kwazo na hatimaye kuzishinda—na shangwe isiyo na kifani katika maisha yajayo. Machozi yatakauka, mioyo iliyovunjika itaponywa, kile kilichopotea kitapatikana, wasiwasi utaondolewa, familia zitarejeshwa tena na vyote vile Baba aliavyonavyo vitakuwa vyetu.28

Mtegemee Yesu Kristo na uishi29 ndiyo ushuhuda wangu katika jina lililotukuzwa na takatifu la mpendwa “Mchungaji na Askofu wa nafsi [zetu],”30 Yesu Kristo, amina.

Muhtasari

  1. Mathayo 23:27.

  2. Mathayo 25:1–11.

  3. Tafsiri ya Joseph Smith, Mathayo 25:11 (katika Mathayo 25:12, tanbihi a).

  4. Mathayo 25:13.

  5. Mzee James E. Talmage alifundisha: “Bwana harusi ni Bwana Yesu; karamu ya ndoa inaashiria ujio Wake katika utukufu, ili kulipokea Yeye Mwenyewe Kanisa hapa ulimwenguni kama bibi harusi Wake. Wanawali wanaashiria wale ambao wanakiri imani katika Kristo, na ambao, kwa hivyo, kwa ujasiri wanatarajia kujumuishwa kuwa miongoni mwa washiriki waliobarikiwa katika karamu. Taa zilizowashwa, ambazo kila mwanamwali alibeba, ni dhihirisho la nje la imani na desturi ya Ukristo; na katika akiba ya mafuta ya wale wenye busara tunaweza kuona nguvu ya kiroho na wingi ambao bidii na kujitolea katika huduma ya Bwana pekee inaweza kuleta” (Jesus the Christ [1916], 578).

  6. Dallin H. Oaks, “Maandalizi kwa ajili ya Ujio wa Pili,” Liahona, Mei 2004, 9.

  7. Mafundisho na Maagano 45:56–57; msisitizo umeongezwa.

  8. “Kuanguka kwa umande hutoa kiasi kidogo cha maji hata wakati wa majira ya joto, na ni muhimu kwa ajili ya mimea ya majira ya joto kama vile matikiti maji. Kadiri eneo linavyokuwa karibu na bahari, kuna uwezekano mwingi wa kuanguka kwa umande katika usiku usio na upepo wakati udongo unapokuwa baridi sana kushinda hewa ambayo hugusa uso wake. Kwa ujumla, Nyanda za Pwani zinakuwa na umande zaidi kushinda maeneo ya bara; Mlima Carmel ni maarufu kwa hili, ambao una wastani wa usiku wa siku 250 za umande kwa mwaka” (Efraim Orni and Elisha Efrat, Geography of Israel, 4th rev. ed. [1971], 147).

  9. Mafundisho na Maagano 128:19.

  10. Mosia 23:18.

  11. Alma 37:6.

  12. Marko 4:38.

  13. Ayubu 17:15.

  14. Helamani 5:40.

  15. Ayubu 28:12.

  16. Moroni 7:20.

  17. Matendo ya Mitume 9:6.

  18. Alma 15:6

  19. 2 Nefi 26:28.

  20. Mathayo 9:28.

  21. Matendo ya Mitume 26:27.

  22. Alma 5:15.

  23. Mwanzo 18:25.

  24. Mormoni 6:17.

  25. Yeremia 31:16–17; msisitizo umeongezwa.

  26. Ona Camille N. Johnson, “Mwalike Kristo Aiandike Hadithi YakoLiahona, Nov. 2021, 82: “Acha dhiki na shida ambavyo ni sehemu ya kila hadithi nzuri viwe ni sehemu ya kukuleta karibu, na kuwa zaidi kama Yesu Kristo.”

  27. 2 Nefi 31:20.

  28. Ona Mafundisho na Maagano 84:38.

  29. Ona Alma 37:47.

  30. 1 Petro 2:25.

Chapisha