2023
Halo kutoka Kiribati
Machi 2023


Halo kutoka Kiribati Rafiki, Jan. 2023, 18–19.

Halo kutoka Kiribati!

Jifunze kuhusu watoto wa Baba wa Mbinguni ulimwenguni kote.

Kiribati (kee-ruh-bas) ni nchi ya kisiwa katika Bahari ya Pasifiki. Takribani watu 120,000 wanaishi huko.

visiwa 33

Picha
Kisiwa chenye miti ya minazi

Vielelezo na Robyn Brimley

Kiribati ni visiwa vidogo vidogo vilivyo enea kwenye zaidi ya maili za mraba milioni 1.4 (kilometa 3.52) za bahari! Mahali pake kwenye sayari ya dunia inaiweka katika zoni ya kwanza ya wakati yenye kuona mwangaza wa jua la kila siku.

Fuko Nzuri za Bahari

Picha
Dunia inaonyesha jua linachomoza

Kiribati imejaa fuko zenye mchanga mwingi na miti ya minazi. Ni hali ya joto mwaka mzima.

Mifano Mizuri

Picha
Familia pamoja na wazazi , watoto na babu na bibi

Takribani asilimia 20 ya watu ni waumini wa Kanisa. Wao ni mfano mzuri kwa wengine wanaoishi kisiwani humo.

Kwenda Kuvua Samaki!

Picha
Mvulana ameshikilia samaki na wavu

Kwa vile bahari imewazunguka pande zote, watu huko Kiribati wanakula vyakula vingi vya baharini. Nazi, wali na maboga pia ni maarufu

Hekalu Lipo Njiani

Picha
Kielelezo cha hekalu la Kiribati

Mwaka 2020, Rais Russell M. Nelson alitangaza kwamba hekalu litajengwa huko Kiribati! Hivi ndivyo litakavyoonekana.

Chapisha