2023
Tatizo la Kushiriki
Machi 2023


“Tatizo la Kushiriki,” Rafiki, Machi. 2023, 36–37.

Tatizo la Kushiriki

“Kushiriki ni njia ya kuwaonyesha watu kuwa unajali kuhusu wao”

Picha
Akina kaka wakishiriki bisi na sushi

Tafuna, tafuna, tafuna. Andrew akameza bisi zake na kuchota zingine mkono tele.

Kaka yake mkubwa, Caleb, akajiinamia chini kwenye kochi pembeni yake. “Hujambo, naweza kupata kidogo?”

Andrew hakutoa macho yake kutoka kwenye TV. “Hapana.

“Aa, jamani. Unaweza kunigawia.”

Caleb akalifikia bakuli, lakini Andrew akaliondosha mbali.

“Hapana! Nimekwishakwambia mapema. Usiulize tena!”

“Vema.” Caleb akasimama na kuondoka chumbani humo.

Siku iliyofuata, Andrew alikwenda jikoni. Caleb alikuwa akitengeneza sushi pamoja na wali, mwani na nguruwe ya kopo.

Andrew akapata hamu ya chakula hicho. “Ninaweza kupata kidogo?”

“Hapana,” Caleb alisema.

Hiyo ilimfanya Andrew akasirike sana. Alikimbia kushuka ngazi haraka kumwambia Baba.

“Kwa nini Caleb anakuwa mchoyo sana?” aliuliza.

Baba alikunja sura. “Niliona jana kwamba wewe hukushiriki bisi zako. Kwa nini Caleb apaswe kushiriki na wewe baada ya wewe kutoshiriki na yeye?”

“Kwa sababu yeye ni kaka yangu!” Andrew alisema.

“Basi kwa nini wewe hukushiriki na yeye?”

“Katu yeye hajawahi kushiriki na mimi hata! Zaidi ya hayo, nilitengeneza kwa ajili yangu tu, siyo na yeye,” Andrew alisema. Lakini alihisi vibaya kidogo. Pengine ulikuwa uchoyo wake wa kutonigawia.

“Je, ulijua kwamba nchini Korea, kushiriki ni kitu muhimu sana? Baba aliuliza. Familia ya Andrew ilikuwa inatokea Korea. “Kushiriki ni njia ya kuwaonyesha watu kuwa unajali kuhusu wao. Hivyo kutokushiriki, ni kama kusema kwamba wewe hujali kuhusu wao.”

“Lakini mimi najali kuhusu Caleb.”

Andrwe alikifikiria kuhusu kile ambacho Yesu angekifanya. Yeye akakumbuka jinsi Yesu anavyompenda kila mtu—hata wale ambao sio wakarimu Kwake.

“Nadhani nitakwenda kushiriki na Caleb kesho na nione itakavyokuwa,” alimwambia Baba.

Baba akatabasamu. “Nafikiri hilo ni wazo zuri.”

Andrew alipokwenda kitandani usiku ule, alifikiria kuhusu vitu vingine vizuri ambavyo angeweza kufanya kwa ajili ya Caleb. Alikuwa na shauku ya kuanza kushiriki!

Asubuhi iliyofuata, Andrew aliamka na kukutana na mshangao. Caleb alikuwa ametengeneza kifungua kinywa kwa ajili yake tu!

“Baba aliongea na mimi kuhusu kushiriki,” Caleb alisema. “Ninataka kufanya vizuri. Kwa hiyo nimetengeneza hii kwa ajili yako.”

“Asante.” Andrew alisema. “Na mimi nataka kufanya vizuri pia!”

Baadaye siku hiyo, Andrew na Caleb waliangalia filamu. Andrew alimwacha Caleb achague filamu. Kisha akatengeneza bisi kwa ajili ya Caleb tu! Alitazama ndani ya bakuli. Ilikuwa kama bisi zinasema, “UNILE MIMI!” Lakini Andrew hakuchukua hata moja. Akampa Caleb lile bakuli na kusema, “Hii yote ni yako. Samahani sikushiriki nawe kabla.”

Andrew alishiriki na Caleb wiki yote. Alimwachia Caleb asome vitabu vyake. Alimwachia Caleb atumie kalamu zake za kuwekea alama maandishi. Aliwachia Caleb achezee wanasesere wake awapendao. Hata alimpa Caleb zamu ya ziada walipokuwa wakicheza mchezo.

Kadiri Andrew alivyokuwa akishiriki na Caleb, ndivyo Caleb alivyoshiriki zaidi pamoja naye. Punde wakawa wakitendeana mambo mazuri wakati wote. Andrew alijua kwamba Baba wa Mbinguni alikuwa akimsaidia yeye kushiriki na kaka yake. Andrew hakuwa mkamilifu kama Yesu, bali yeye alikuwa akijaribu kuwa zaidi kama Yeye kila siku.

Hadithi hii ilitokea huko Marekani.

Picha
PDF ya hadithi

Kielelezo na Adam Howling

Chapisha