Rafiki
Mfalme Benyamini ni Nani?
Mei 2024


“Mfalme Benyamini ni Nani?” Rafiki, Mei 2024, 24–25

Jifunze kuhusu Kitabu cha Mormoni

Mfalme Benyamini ni Nani?

Picha
Mfalme Benyamini mnarani

Mfalme Benyamini alikuwa nabii wa Mungu na mfalme mwema. Aliwakusanya watu ili awafundishe. Alisimama mnarani ili watu wengi waweze kumsikia. Watu walipiga mahema kuzunguka mnara ili kusikiliza. Ilikuwa kama mkutano mkuu!

Picha
Yesu Kristo

Mfalme Benyamini aliwafundisha kwamba Yesu Kristo angezaliwa duniani. Yesu angetenda miujiza. Angeteseka na kufa kwa ajili ya dhambi za watu wote. Angekufa pia na kufufuka ili tuweze kuishi tena!

Picha
Watu wakimsikiliza Mfalme Benyamini

Mfalme Benyamini aliwaalika watu kujichukulia juu yao jina la Kristo. Hiyo ilimaanisha wafanye agano, au ahadi, kumfuata Mungu na kushika amri Zake.

Picha
Mvulana akibatizwa

Leo, tunaonyesha kwamba tuko radhi kujichukulia juu yetu jina la Kristo wakati tunapobatizwa.

Changamoto ya Maandiko

  • Baada ya watu kumsikiliza Mfalme Benyamini, ni nani ambaye walifanya agano naye? (Mosia 5:5)

  • Ni kitu gani Abinadi alimwambia Mfalme Nuhu alihitaji kufanya ili kuokolewa? (Mosia 12:33)

  • Baada ya Alma na Helamu kutoka majini, walijawa na nini? (Mosia 18:14)

Ninaweza Kusoma Kitabu cha Mormoni!

Baada ya kusoma, paka rangi sehemu ya picha. Unaweza kusoma maandiko haya yanayoenda sambamba na usomaji wa kila wiki kutoka Njoo, Unifuate.

Picha
PDF ya hadithi

Vielelezo na Simini Blocker

Chapisha