Scripture Stories
Abishi


“Abishi,” Hadithi za Kitabu cha Mormoni (2023)

Alma 17–19

Abishi

Aliwasaidia watu wake kuamini katika Yesu

Picha
Abishi akitembea kote kijijni

Abishi alimfanyia kazi malkia ambaye alikuwa Mlamani. Abishi alikuwa amejifunza kuhusu Yesu Kristo kutoka kwa ono la baba yake. Kwa miaka mingi, aliamini katika Yesu na alitaka kumfuata Yeye. Lakini alikuwa hajamwambia Mlamani mwingine bado.

Alma 19:16–17

Picha
Abishi akimtazama malkia, mfalme na Amoni

Siku moja, Mnefi aliyeitwa Amoni alikuja kwenye ufalme huu ili kuwafundisha Walamani kuhusu Yesu na Mungu. Malkia na mfalme waliamini kile Amoni alichofundisha. Malkia na mfalme walijua kwamba Yesu angekuja ulimwenguni na kumfanya kila mmoja ambaye aliamini katika Yeye aweze kusamehewa.

Alma 17:12–13; 18:33–36, 39–40; 19:9, 13

Picha
Abishi anaona kila mmoja akianguka ardhini

Malkia na mfalme walihisi Roho Mtakatifu na walikuwa na furaha sana kwamba walianguka ardhini. Amoni na watumishi walianguka pia. Abishi alikuwa ndiye tu aliyekuwa amesimama.

Alma 19:6, 13–16

Picha
Abishi akizungumza na watu wengi

Abishi alitaka kuwaambia watu kuhusu muujiza huu. Alitumaini watu wangeamini katika nguvu za Mungu wakati walipoona kile kilichotokea. Kwa hiyo Abishi alikimbia nyumba hadi nyumba. Aliwaambia watu waende wakaone kile Mungu amefanya kwa ajili ya malkia na mfalme.

Alma 19:17

Picha
watu wengi wanawaona watu wakiwa ardhini

Watu wengi walikuja kwenye nyumba ya malkia na mfalme. Walishangaa kwa sababu ilionekana kana kwamba malkia, mfalme na watumishi wote walikuwa wamekufa.

Alma 19:18

Picha
watu wakibishana

Watu walikanganyikiwa. Walibishana kuhusu kile kilichomtokea malkia na mfalme.

Alma 19:19–21

Picha
Abishi amepiga magoti na kushikilia mkono wa malkia

Wakati Abishi aliporudi, aliona watu wakibishana. Alikuwa na huzuni sana kwa sababu hawakuona nguvu za Mungu. Kisha alichukua mkono wa malkia, na malkia alisimama na kumsifu Yesu.

Alma 19:28–29

Picha
mfalme na malkia wanasimama pamoja na Abishi na Amoni

Malkia alishikilia mkono wa mumewe, na alisimama. Mfalme aliwaambia watu kuhusu Yesu. Kisha Amoni na watumishi wengine walisimama. Waliwaambia watu kwamba Yesu alikuwa amewabadilisha wao. Sasa walitaka kufanya mambo mema tu. Watu wengi waliwaamini wao.

Alma 19:29–36

Picha
Abishi, malkia, na mfalme wakitazama ubatizo

Kama vile Abishi alikuwa ametumaini, watu waliona nguvu za Mungu. Watu wengi waliamini katika Yesu na wakabatizwa. Walikuwa na Roho wa Mungu pamoja nao Hata walianzisha Kanisa katika nchi yao. Waliona kwamba Yesu anamsaidia kila mmoja ambaye anatubu na kuamini katika Yeye.

Alma 19:17, 31, 35–36

Chapisha