Scripture Stories
Kijakazi Mnefi


“Kijakazi Mnefi,” Hadithi za Kitabu cha Mormoni (2023)

Alma 50

Kijakazi Mnefi

Anasaidia kulinda watu wake

Picha
Moriantoni anashikilia tochi na anazungumza na umati wa watu, na kijakazi akiwa karibu

Kijakazi alimfanyia kazi kiongozi Mnefi aliyeitwa Moriantoni. Moriantoni alikuwa anasababisha vurugu miongozi mwa watu. Alikishambulia kikundi cha Wanefi na kujaribu kutwaa nchi yao. Kisha alipanga kusafiri kwenda kaskazini pamoja na watu wake ili kutwaa nchi huko.

Alma 50:25–30

Picha
kijakazi anakimbia kutoka kwa Moriantoni usiku

Siku moja, Moriantoni alimkasirikia kijakazi. Alimtendea vibaya sana na kumuumiza. Kijakazi alitoroka na kukimbilia kwenye kambi ya Kapteni Moroni. Alimwambia Moroni kuhusu mambo mabaya ambayo Moriantoni alifanya. Moroni alimwamini kijakai huyo.

Alma 50:30–31

Picha
kijakazi anaonyesha kwenye ramani na anazungumza na Kapteni Moroni

Kijakazi yule pia alisema kwamba Moriantoni alitaka kuondoka na kutwaa nchi iliyokuwa huko kaskazini. Moroni alipata hofu. Wanefi wangeweza kuwa katika hatari kama Moriantoni angetwaa nchi iliyopo kaskazini. Hiyo ingeweza kusababisha watu kupoteza uhuru wao.

Alma 50:31–32

Picha
Kijakazi anamtazama Moroni na jeshi

Moroni alituma jeshi kumzuia Moriantoni. Watu wa Moriantoni walipigana na jeshi na wakashindwa. Waliahidi kudumisha amani na kurudi katika nchi yao. Kwa sababu kijakazi alimuonya Moroni, miji ya Wanefi ilibakia kuwa salama.

Alma 50:33, 35–36

Chapisha