Scripture Stories
Mfalme Nuhu na Mfalme Limhi


“Mfalme Nuhu na Mfalme Nuhu,” Hadithi za Kitabu cha Mormoni (2023)

Mosia 19–22

Mfalme Nuhu na Mfalme Limhi

Kutoroka kutoka kwa Walamani

Picha
Gidioni anashikilia upanga na anasimama karibu na mnara, na Nuhu yuko mnarani na ananyoshea jeshi la Walamani kidole

Mfalme Nuhu alitawala kundi la Wanefi. Alifanya mambo mengi mabaya, na baadhi ya watu walimkasirikia sana. Mtu aliyeitwa Gidioni alipigana na Nuhu kwa upanga. Nuhu alikimbia na kupanda mnarani. Kutoka kwenye mnara, aliona jeshi la Walamani likija. Nuhu alijifanya alikuwa anawaogopa watu wake, kwa hiyo Gidioni alimwacha aishi.

Mosia 11:1–2; 19:2–8

Picha
Nuhu anakimbilia mbali, na watu wa Nuhu wanaogopa

Nuhu na watu wake wanakimbilia mbali. Lakini Walamani waliwafukuza na wakaanza kuwashambulia. Nuhu aliwaambia wanaume waache familia zao na waende pamoja naye.

Mosia 19:9–11

Picha
Limhi, Gidioni na Wanefi wengine wanakabiliana na jeshi la Walamani

Baadhi ya wanaume waliondoka na Nuhu. Lakini wengi wa wanaume walichagua kubaki pamoja na familia zao. Limhi mwana wa Nuhu pia alichagua kubaki.

Mosia 19:12, 16–17

Picha
wanawake wanasimama mbele ya Limhi na Wanefi wengine

Mabinti wengi walisimama mbele ya jeshi na kuwaomba Walamani wasiziumize familia zao. Walamani waliwasikiliza mabinti wale na wakawaacha Wanefi waishi. Badala yake, Walamani waliwateka Wanefi.

Mosia 19:13–15

Picha
Nuhu na watu wake wanakasirikiana

Wanaume ambao walikimbia walitaka kurudi kwa familia zao. Nuhu alijaribu kuwazuia, kwa hiyo walimuua. Kisha wakarudi kwa familia zao.

Mosia 19:18–22

Picha
wanaume Wanefi wanasalimia familia zao pamoja na Gidioni

Wanaume walikuwa na furaha sana kwamba familia zao zilikuwa salama. Walimwambia Gidioni kile kilichomtokea Nuhu.

Mosia 19:22–24

Picha
Limhi anawapa Walamani chakula na wanyama

Watu wanamchagua Limhi kuwa mfalme wao mpya. Limhi alimwahidi mfalme Mlamani kwamba wangewalipa Walamani nusu ya kila kitu walichomiliki. Kama malipo, mfalme wa Walamani aliahidi hangewaumiza watu wa Limhi.

Mosia 19:25–27

Picha
Limhi na mkewe wanaonekana kuhuzunika, na Wanefi wengi wameumizwa

Waliishi kwa amani kwa miaka kadhaa. Kisha Walamani wakaanza kuwatendea watu wa Limhi vibaya. Watu walitaka kuwa huru tena. Walijaribu kupigana na Walamani, lakini walishindwa. Watu walisali kwa Mungu kwa ajili ya msaada.

Mosia 19:29; 21:1–15

Picha
Limhi na Amoni wakizungumza

Siku moja, Mnefi mmoja aliyeitwa Amoni alimtembelea Limhi na watu wake. Amoni alitokea nchi iliyoitwa Zarahemla. Limhi alikuwa na furaha kumwona Amoni.

Mosia 21:22–24

Picha
Gidioni, Limhi, Amoni na Wanefi wengine wakizungumza

Amoni angewaongoza watu wa Limhi hadi Zarahemla, lakini iliwabidi watoroke kutoka kwa Walamani kwanza. Gidioni alikuwa na mpango.

Mosia 21:36; 22:1–9, 11

Picha
Walinzi Walamani walilala, na Wanefi waliondoka kutoka kwenye mji.

Usiku, Gidioni aliwapa walinzi Walamani kileo zaidi ili kuwafanya walale. Wakati walinzi wamelala, Limhi na watu wake waliutoroka mji. huo

Mosia 22:7, 10–12

Picha
Mfalme Mosia na watu wake wanamkaribisha Limhi na watu wake.

Walienda hadi Zarahemla na kuungana na Wanefi huko. Limhi na watu wake walijifunza zaidi kuhusu Mungu. Walifanya agano, au ahadi maalumu, kumtumikia Mungu na kutii amri Zake. Walibatizwa na kuwa sehemu ya Kanisa la Mungu. Walikumbuka kwamba Mungu aliwasaidia kutoroka kutoka kwa Walamani.

Mosia 21:32–35; 22:13–14; 25:16–18

Chapisha