Scripture Stories
Kapteni Moroni na Zerahemna


“Kapteni Moroni na Zerahemna,” Hadithi za Kitabu cha Mormoni (2023)

Alma 43–44

Kapteni Moroni na Zerahemna

Vita na ahadi ya kuishi kwa amani

Picha
Zerahemna anaongoza majeshi yake

Zerahemna alikuwa kiongozi wa majeshi ya Walamani. Alitaka kuwatawala Wanefi na kuwafanya wawatumikie watu wake. Zerahemna aliongoza majeshi yake kuwashambulia Wanefi.

Alma 43:3–8

Picha
Jeshi la Wanefi linatazama jeshi la Walamani

Wanefi walitaka kulinda nyumba zao, familia zao na dini yao. Walijua wasingeweza kumwabudu Bwana kama Walamani wangewatawala. Wanefi walichagua kupigana na maadui zao.

Alma 43:9–10, 14–15

Picha
Moroni anatazama mbele na mawingu yakiwa nyuma

Mtu aliyeitwa Moroni alikuwa kapteni wa majeshi ya Wanefi. Moroni alihakikisha majeshi yake yalikuwa tayari kupigana.

Alma 43:16–17

Picha
Kapteni Moroni na askari wa Wanefi tayari kupigana

Askari wa Moroni walileta silaha, na Moroni aliwapa deraya imara na ngao za kuwalinda.

Alma 43:18–19

Picha
Walamani wanatazama jeshi la Wanefi na wanaonekana kuogopa

Moroni alienda na majeshi yake kupigana na Walamani. Lakini wakati Walamani waliwaona Wanefi wako na silaha na ngao, walikuwa na uoga wa kupigana. Walamani walikuwa tu na mavazi mepesi na hawakuwa na silaha ya kuwalinda.

Alma 43:19–21

Picha
Askari Walamani wanakimbilia msituni

Walamani waliondoka. Walijaribu kuingia kisiri kwenye nchi tofauti ya Wanefi. Walifikiria Moroni hangejua pale walikwenda.

Alma 43:22

Picha
Wapelelezi Wanefi waliwatazama askari Walamani wakitoroka

Lakini punde Walamani walipoondoka, Moroni aliwatuma wapelelezi kuwafuata.

Alma 43:23

Picha
Askari Mnefi anamsikiliza Alma

Kisha Moroni alituma ujumbe kwa nabii Alma. Alimtaka Alma amuulize Bwana kile Walamani walikuwa wanapanga kufanya. Bwana alimwambia Alma kwamba Walamani walikuwa wanapanga kushambulia nchi hafifu iliyoitwa Manti. Moroni alimsikiliza Alma. Aliongoza majeshi yake kupigana dhidi ya Walamani.

Alma 43:23–33

Picha
Askari Walamani na Wanefi wakipigana

Majeshi yalipigana Walamani walikuwa na nguvu sana na walikuwa na hasira sana. Wanefi wakawa wanawaogopa Walamani na walikuwa wanataka kutoroka. Lakini Moroni aliwakumbusha wao juu ya familia zao na imani yao, hivyo waliendelea kupigana.

Alma 43:34–37, 43–48

Picha
Moroni ananyanyua mkono kusitisha mapigano

Wanefi walisali kwa Bwana kwa ajili ya msaada. Bwana alijibu sala zao na akawapa nguvu nyingi. Sasa Walamani wakawa wanaogopa. Walikuwa wamenaswa kwenye mtego na hawakuweza kutoroka. Wakati Moroni alipoona kwamba Walamani wanaogopa, aliwaambia askari wake na kusitisha mapigano. Moroni hakutaka kuwaua Walamani.

Alma 43:49–53; 44:1–2

Picha
Moroni anaongea na Walamani

Moroni alimwambia Zerahemna kwamba Walamani wangeenda zao kama wangeahidi kutopigana na Wanefi tena. Zerahemna alikasirika na kujaribu kuendelea kupigana, lakini hangeweza kuwashinda askari wa Moroni. Kisha Zerahemna na majeshi yake wakaahidi kuishi kwa amani, na Moroni akawaacha waende zao.

Alma 44:1–20

Chapisha