Scripture Stories
Waanti‑Nefi­Lehi


“Waanti‑Nefi­Lehi,” Hadithi za Kitabu cha Mormoni (2023)

Alma 23–27

Waanti‑Nefi­Lehi

Watu ambao walichagua kuwapenda maadui zao

Picha
Amoni anawafundisha watu chini ya mti

Walamani wengi walijifunza kuhusu Mungu kutoka kwa Amoni na kaka zake. Walamani hawa walikuwa na imani imara katika Bwana na walifuata amri za Mungu. Wao walitaka jina jipya, kwa hiyo walijiita Waanti-Nefi Lehi badala ya Walamani.

Alma 23:3–7, 16–17

Picha
Familia zikimsikiliza Amoni akifundisha

Waanti‑Nefi­Lehi walibadilika kwa sababu ya imani yao katika Mungu. Walitubu mambo mabaya waliyokuwa wamezoea kufanya. Walijua Mungu aliwapenda na amewasamehe.

Alma 24:8–14

Picha
Waanti-Nefi-Lehi wanatupa silaha zao kwenye shimo la wazi

Walamani walikasirika sana na wallijiandaa kuwashambulia Waanti-Nefi-Lehi. Badala ya kupigana, Waanti‑Nefi­Lehi waliweka ahadi na Mungu. Walisema kamwe hawangewaumiza watu tena. Kwa kuonyesha hili, walizika silaha zao. Wao walichagua kuwapenda maadui zao badala ya kuwaumiza au kuwaua.

Alma 24:1–19; 26:31– 34

Picha
Walamani waliokasirika wanashika silaha

Walamani ambao hawakuamini katika Mungu waliwashambulia Waanti-Nefi-Lehi.

Alma 24:20

Picha
Waanti‑Nefi­Lehi wawili wamepiga magoti katika sala

Waanti-Nefi Lehi walikuwa na imani kwamba kama wangeuawa, wangeishi tena na Mungu. Walishika ahadi yao na Mungu na hawakupigana na wale Walamani.

Alma 24:16, 21

Picha
Walamani wanaacha kushambulia

Badala ya kupigana, Waanti-Nefi Lehi walisali. Wakati Walamani walipoona hili, wengi wao waliacha kuwashambulia. Walijisikia vibaya kuwaua watu. Walamani hao pia walichagua kamwe kutowaumiza watu tena. Walijiunga na Waanti-Nefi Lehi.

Alma 24:21–27; 25:13–16

Picha
Amoni na Waanti-Nefi Lehi wanasafiri

Kadiri muda ulivyosonga, watu zaidi walishambulia. Amoni na kaka zake walihuzunika Waanti-Nefi Lehi walikuwa wanateseka. Walimuomba mfalme awapeleke watu wake kuishi na Wanefi. Mfalme alisema wangeenda kama Bwana aliwataka wao wafanye hivyo. Amoni alisali. Bwana alisema wanapaswa kwenda na kwamba Yeye atawalinda wawe salama.

Alma 27:2–15

Picha
Wanefi wanawasalimia watu wa Waanti-Nefi–Lehi

Wanefi waliwapa Waanti-Nefi Lehi ardhi ya kuishi na kuwalinda. Kama shukrani, Waanti-Nefi Lehi waliwapa Wanefi chakula. Waanti-Nefi Lehi walikuwa na imani kuu na walimpenda Mungu. Walikuwa waaminifu kwa kila mmoja na walishika ahadi yao kamwe wasipigane. Walikuwa waaminifu maisha yao yote.

Alma 27:20–30

Chapisha