Scripture Stories
Teankumu


“Teankumu,” Hadithi za Kitabu cha Mormoni (2023)

Alma 51–52

Teankumu

Kuwalinda watu Wake

Picha
Teankumu anazungumza na Kapteni Moroni kwenye kambi

Teankumu alikuwa kiongozi katika jeshi la Kapteni Moroni. Alikuwa anajaribu kuiweka miji ya Wanefi kuwa salama dhidi ya Walamani.

Alma 50:35; 52:19

Picha
Amalikia na askari wa Walamani wakiwa na silaha

Amalikia alikuwa Mnefi ambaye alikuja kuwa mfalme wa Walamani. Yeye alitaka pia kuwatawala Wanefi. Alitaka kuwashambulia Wanefi na kutwaa miji mingi.

Alma 47:1, 35; 48:1–4; 51:23–28

Picha
Jeshi la Wanefi likitembea

Jeshi la Teankumu lilienda kuzuia jeshi la Amalikia lisishambulie miji ya Wanefi.

Alma 51:28–30

Picha
majeshi yalikabiliana wakati wa machweo ya jua

Majeshi yalipigana kwa siku nzima. Teankumu na jeshi lake walipigana kwa nguvu na ujuzi zaidi kuliko jeshi la Amalikia. Lakini hakuna jeshi lililoshinda. Wakati giza lilipoingia, majeshi yote yaliacha kupigana ili kwamba wangeweza kupumzika.

Alma 51:31—32

Picha
Teankumu anaketi mbele ya moto wa kambi

Lakini Teankumu hakupumzika. Yeye na watumishi wake kwa siri walienda kwenye kambi ya Amalikia.

Alma 51:33

Picha
Teankumu anasimama kwenye mbalamwezi katika hema la Amalikia

Teankumu alinyemelea hadi ndani ya hema la Amalikia. Alimuua Amalikia kabla ya Amalikia hajaweza kuamka. Kisha Teankumu alienda kwenye kambi yake na kuwaambia askari wake wawe tayari kwa ajili ya kupigana.

Alma 51:33–36

Picha
Walamani wanaamka na wanaonekana kuogopa

Wakati Walamani walipoamka, waligundua kwamba Amalikia alikuwa amekufa. Waliona pia kwamba Teankumu na jeshi lake walikuwa tayari kupigana nao.

Alma 52:1

Picha
Walamani wanalikimbia jeshi la Teankumu

Walamani waliogopa na wakakimbilia. Mpango wa Teankumu ulikuwa umewafanya Walamani kuwa na uoga sana kushambulia miji zaidi ya Wanefi. Teankumu sasa alikuwa na muda wa kuifanya miji ya Wanefi kuwa salama. Alifanya bidii kuwalinda watu wake. Aliweza kuiweka miji mingi ya Wanefi kuwa salama.

Alma 52:2–10

Chapisha