Scripture Stories
Alma na Korihori


“Alma na Korihori,” Hadithi za Kitabu cha Mormoni (2023)

Alma 30

Alma na Korihori

Imani kwamba Mungu kweli yupo

Picha
Korihori anatabasamu na anazungumza na mtu wakitembea pamoja kwenye njia yenye shughuli nyingi

Mtu mmoja aliyeitwa Korihori alikuja kwenye nchi ya Zarahemla. Aliwaambia watu kwamba Mungu na Yesu Kristo hawapo.

Alma 30:6, 12, 37–38, 45

Picha
Korihori anatabasamu na anatoa ishara kwa mtoto mwenye huzuni

Korihori aliwaambia watu wangeweza tu kujua kitu kama wangekiona. Aliwadhihaki watu ambao waliamini katika Yesu.

Alma 30:13–16

Picha
Korihori anatabasamu na anazungumza na umati wa watu

Korihori aliwaambia watu hawakuhitaji amri za Mungu. Alisema watu wangeweza kufanya cho chote walichotaka. Watu wengi walimwamini yeye. Waliamua kufanya mambo mabaya.

Alma 30:17–18

Picha
Korihori amefungwa kwa kamba na anatolewa nje ya mji na askari

Korihori alijaribu kuwafundisha Waanti-Nefi-Lehi, lakini hawakumuamini. Walimfunga kamba na kumpeleka mbali. Alienda nchi ya Gidioni badala yake. Watu huko pia walimfunga kamba. Walimpeleka kwa Alma.

Alma 30:19–29

Picha
Korihori anatabasamu na anampa ishara Alma

Korihori alimwambia Alma kwamba hakuna Mungu. Alisema Alma na makuhani wengine walikuwa wanadanganya watu. Korihori alisema walikuwa wanawafanya watu wafuate tamaduni za kipumbavu. Alisema pia walikuwa wanatwaa fedha kutoka kwa watu. Alma alijua hii haikuwa kweli. Aliamini katika Mungu na Yesu.

Alma 30:30–40

Picha
Alma anazungumza na umati wa watu wakati Korihori akiwa ameketi chini huko nyuma akiwa amekunja mikono

Alma alisema manabii na kila kitu ulimwenguni huwasadia watu kujua kwamba yuko Mungu. Korihori alitaka ushahidi zaidi. Alma alisema angempa Korihori ushahidi. Alisema kwamba Mungu angemfanya Korihori asiweze kuzungumza. Punde Alma aliposema hivi, Korihori hakuweza kuzungumza.

Alma 30:41–50

Picha
Korihori anaonekana kuwa na huzuni na ananyoosha kwa kidole kwenye kipande cha karatasi kilicho na maandishi wakati umati wa watu ukiondoka na kumwacha

Korihori aliandika kwamba alijua Mungu yupo. Daima amekuwa akijua hivyo. Aliandika kwamba ibilisi alikuwa amemdanganya. Ibilisi alimwambia Korihori kufundisha uongo juu ya Mungu na Yesu. Wakati watu walipojua ukweli huu kuhusu Korihori, hawakuamini mafundisho yake. Walitubu na kuanza kumfuata Yesu tena.

Alma 30:52–53, 57–58

Chapisha