Scripture Stories
Ishara za Kuzaliwa kwa Yesu


“Ishara za Kuzaliwa kwa Yesu,” Hadithi za Kitabu cha Mormoni (2023)

3 Nefi 1

Ishara za Kuzaliwa kwa Yesu

Imani katika mafundisho ya nabii

Picha
mama na baba wakiwa na mtoto mchanga na watoto wanatembea mjini

Ilikuwa karibia miaka mitano tangu Samweli nabii alipowafundisha watu kuhusu ishara za kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Watu wengi waliamini na walitazamia ishara hizo. Watu wengine walisema Samweli hakuwa sahihi na wakati wa ishara hizo tayari ulikuwa umepita. Waliwadhihaki walioamini na kusema Yesu hangekuja.

Helamani 14:2–7; 3 Nefi 1:4–6

Picha
familia inaketi chini nyumbani, na baba anazungumza

Waaminio walikuwa na wasiwasi, lakini walikuwa na imani. Wao waliendelea kutazamia ishara. Ishara moja ilikuwa usiku ambao hakungekuwa na giza. Ungekuwa angavu kama vile mchana baada ya jua kutua. Usiku usio na giza ungekuwa ishara kwamba Yesu angekuwa anazaliwa siku iliyofuata katika nchi nyingine.

Helamani 14:2–4; 3 Nefi 1:7–8

Picha
familia inaogopa huku ikizomewa

Watu ambao hawakuamini walifanya mpango. Walichagua siku na kusema kwamba kama ishara haingetokea kufikia siku hiyo, waaminio wangeuawa.

3 Nefi 1:9

Picha
Nefi anaona watu wakiwa wakatili kwa familia

Mtu aliyeitwa Nefi alikuwa nabii wakati huu. Alikuwa na huzuni sana kwamba baadhi ya watu walitaka kuwaua waaminio.

3 Nefi 1:10

Picha
Nefi anapiga magoti ili kusali

Nefi aliinama chini ardhini na kusali kwa Mungu kwa ajili ya waaminio ambao walikuwa karibu kufa kwa sababu ya imani yao. Alisali siku nzima.

3 Nefi 1:11–12

Picha
Nefi anashikilia mikono yake pamoja na anasali

Kama jibu la sala yake, Nefi alisikia sauti ya Yesu. Yesu alisema ishara ingetokea usiku ule na kisha Yeye angezaliwa siku iliyofuata.

3 Nefi 1:12–14

Picha
Watu walitazama angani na kushangaa

Usiku ule kulikuwa hakuna giza ingawa jua lilikuwa limetua. Watu ambao walikuwa hawajaamini maneno ya Samweli walishangaa sana kiasi kwamba walianguka ardhini. Waliogopa kwa sababu walikuwa hawaamini. Watu ambao walikuwa wanaamini hawangeuawa.

3 Nefi 1:15–19

Picha
familia zinatazama anga samawati angavu na kushangaa

Siku iliyofuata, jua lilichomoza tena na anga likabaki kuwa angavu. Watu walijua kwamba hii ilikuwa ile siku ambayo Yesu angezaliwa.

3 Nefi 1:19

Picha
watu wanatazama angani na kuona nyota mpya

Watu waliona ishara nyingine. Nyota mpya ilichomoza angani. Ishara zote ambazo Samweli alikuwa amesema juu yake zilikuja kutokea kweli. Watu wengi zaidi waliamini katika Yesu na wakabatizwa.

Helamani 14:2–7; 3 Nefi 1:20–23

Chapisha