Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 12: Ninashukuru kwa ajili ya Wanyama


Somo la 12

Ninashukuru kwa ajili ya Wanyama

Madhumuni

Ni kumsaidia kila mtoto kuwa na shukrani kwa Baba wa Mbinguni kwa ajili ya wanyama.

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze Mwanzo 1:24–25 na Mwanzo 6:5–8; 19.

  2. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Biblia.

    2. Mikato 1-6 hadi 1-19 (mikato inayofanana na hiyo pia inaweza kupatikana katika Mikato ya Vielelezo vya Picha vya Msingi seti ya 4, na 5).

    3. Picha 1-28, Uumbaji—Viumbe Hai (Picha za Sanaa za Injili 100; 62483); picha 1-29, Kujenga Safina (Picha za Sanaa za Injili 102; 62053);picha 1-30, Nuhu na Safina Ikiwa na Wanyama (Picha za Sanaa za Injili 103; 62305);

  3. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zo zote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Shughuli za Kujifunza

Mwalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Weka maumbo ya mikato ya wanyama sakafuni au mezani mbele ya watoto. Msaidie mtoto atwae mkato, na amtambue mnyama huyo na kuonyesha darasa. Endelea mpaka kila mtoto apate angalao zamu moja.

Baba wa Mbinguni alimtuma Yesu Kristo kuwaumba wanyama

Rejea pamoja na watoto kwamba Baba wa Mbinguni alimtuma Yesu Kristo kuumba ulimwengu wetu maridadi, ikijumuisha mchana na usiku, bahari na nchi kavu, na mimea na miti. Onyesha Biblia na uwakumbushe watoto kwamba tunaweza kusoma kuhusu Uumbaji katika kitabu hiki. Elezea kwamba Biblia inatuambia kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu waliumba wanyama wote na kuwaweka ulimwenguni.

Onyesha picha 1-28, Uumbaji—Viumbe Hai.

  • Ni nani aliumba vitu unavyoona katika picha hii?

  • Majina ya wanyama walioko katika picha ni gani?

Eleza kwamba Yesu Kristo aliumba wanyama wa kila aina ili wawe ulimwenguni. Baadhi ya wanyama huishi shambani, wengine nyumbani mwetu. Wanyama wengine huishi msituni, wengine milimani, na wengine jangwani. Wanyama wengine huishi katika sehemu za baridi duniani na wengine wanaishi katika sehemu za joto,

  • Ni wanyama gani waishio shambani?

  • Ni wanyama gani wanaoishi msituni, milimani, au jangwani?

  • Unapendelea mnyama gani?

Shughuli

Acha watoto wasimame na kujifanya wao ni wanyama wawapendao.

Wanyama hutusaidia

Elezea kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu waliwaweka wanyama duniani ili watusaidie. Tunatumia baadhi ya wanyama kama chakula, wengine hutufanyia kazi, na wengine ni wakupendeza kuwatazama au kucheza nao.

  • Je, wanyama hutusaidia vipi?

  • Ni kutoka kwa wanyama gani tunapata chakula, kama vile maziwa, mayai, au nyama?

  • Ni kutoka kwa wanyama gani tunapata bidhaa za nguo?

  • Ni wanyama gani wanapendeza kwa kufugwa?

  • Ni wanyama gani waweza kuendeshwa?

Acha watoto waongee kuhusu uzoefu waliopata kutokana na aina tofauti za wanyama.

Wanyama waliokolewa kutokana na gharika

Simulia hadithi ya Nuhu na Safina, kama inavyopatikana katika Mwanzo 6:5–8:19. Onyesha picha 1-29, Kujenga Safina, na picha 1-30, Nuhu na Safina iliyo na Wanyama. Unaweza pia kutumia maumbo ya mikato kuelezea hadithi.

  • Ni kwa namna gani Nuhu na familia yake walibarikiwa kwa kumtii Yesu?

  • Ni kwa namna gani wanyama waliokolewa?

  • Tunapoona upinde wa mvua, unatukumbusha nini?

Shughuli

Acha watoto wasimame na kufanya vitendo unapokariri mstari ufuatao:

Nuhu

Nuhu alijenga safina kubwa (nyoosha mikono kama umeipanua);

Yeye alijua cha kufanya (weka kidole upande wa uso).

Alipigilia, akakata, na akapima (fanya mwenendo kama ilivyosema)

Kama alivyokuwa ameamriwa kufanya (Itikia kwa kichwa).

Na Nuhu aliita familia yake (ashiria kwa mkono)

Watembee kuingia ndani ya mashua (tembea kwa utulivu)—

Na wanyama, wawili kwa wawili (inua vidole viwili juu).

Wakaingia ndani ili kuelea (fanya ishara kuelea kwa mikono).

Mawingu mazito yakatanda (weka mikono juuu ya kichwa),

Mvua ikanyesha (viringa vidole ukiigiza mvua)—

Na dunia yote ikafunikwa (fanya ishara ya kufagia kwa mikono),

Hapakuwepo na nchi kavu kabisa (geuza kichwa upande na upande),

Safina ilielea salama (fanya ishara kuelea kwa mikono)

Siku nyingi usiku na mchana (weka mikono upande mmoja wa uso),

Hatimaye jua lilichomoza tena (weka mikono daura juu ya kichwa)

Na likaangaza vyema na kun’gaa.

Na maji yote nyakauka kabisa (weka mikono kufuani);

Nchi kavu ikatokeza (mikono ilifunguka na ikielekea juu).

Familia na Nuhu ikashukuru (inamisha kichwa na ukunje mikono)

Kwamba Mungu daima alikuwa karibu.

(Imetoholewa kutoka kwenye mstari wa Beverly Spencer.)

Ushuhuda

Elezea hisia zako za shukrani kwa ajili ya ulimwengu maridadi ambao Yesu Kristo aliumba kulingana na mpango wa Baba wa Mbinguni. Elezea jinsi ulivyo na shukrani kwa ajili ya wanyama ambao wamewekwa duniani kwa ajili yetu kuwatumia na kuwafurahia.

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo.

  1. Cheza mchezo “Mnyama, Mnyama, Wewe ni Nani? Acha watoto watengeneze duara. Acha mtoto mmoja asimame katika ya duara na kujifanya kuwa mnyama. Watoto wengine wainue mikono yao ili kubahatisha ni mnyama gani huyu mtoto aliye katikati anamwigiza. Mtoto apobahatisha sahihi, anaingia katika duara na kumwigiza mnyama mwingine. Unaweza kutaka kila mtoto kwanza ukunong’onezee jina la mnyama ataigiza ili kuhakikisha mtoto anawelewa vyema akilini.

  2. Cheza mchezo wa “Huyu ni Mnyama Gani? Waache watoto watoe vidokezo kuhusu mnyama fulani. Vidokezo vinaweza kuashiria pale mnyama anapoishi, jinsi alivyo mkubwa, sauti anayotoa, rangi yake, na jinsi huwasaidia watu. Waambie watoto wainue mikono yao wanapofikiria wanajua ni mnyama gani unayemwongelelea. Rudia kwa wanyama tofauti mara nyingi kama upendavyo kufanya.

  3. Pamoja na watoto Imbeni au semeni maneno ya “The World Is So Big” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto , 235). Fanya vitendo kama inavyoonyeshwa chini:

    Dunia ni kubwa sana, ee, duara sana (tengenezeni duara kubwa kwa mikono),

    Na ndani yake viumbe vya Mungu hupatikana;

    Milima (weka kwa umbo la mlima juu ya kichwa)

    Mabonde (weka viganja mbele ya mwili)

    Na miti mirefu (nyoosha mikono kwa urefu)

    Wanyama wakubwa (ishara ukubwa)

    Na wanyama wadogo (ishara ya udogo)

    Dunia ni kubwa sana, ee, duara sana (tengenezeni duara kubwa kwa mikono),

    Mungu anatupenda sisi wote; baraka zetu ni nyingi (kunja mikono na ujikumbatie).

  4. Waache watoto waongee kuhusu wanyama wao wa kufugwa walio nao au wale ambao wangependa kuwa nao. Jadili na watoto jinsi tunavyopaswa kuwatendea na kuwatunza wanyama wa kufugwa.

  5. Mpe kila mtoto kipande cha karatasi na krayoni au penseli. Acha kila mtoto achore picha ya mnyama ampendaye. Andika kwenye kila picha Ninashukuru kwa ajili ya wanyama.

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Onyesha picha 1-28, Uumbaji—Viumbe Hai. Kwa maneno yako mwenyewe, simulia hadithi ya uumbaji wa wanyama (ona Mwanzo 1:24–25). Elezea shukrani zako kwa ajili ya wanyama.

  2. Chagua wanyama wachache ambao watoto wanawafahamu. Acha watoto wajifanye kuwa kila mnyama. Jadili jinsi wanyama hawa wanavyoonekana na sauti zao zinavyosikika na matumizi yao.

  3. Wasaidie watoto kuimba au kusema maneno “All Things Bright and Beautiful (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 231).

Chapisha