Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 22: Mimi Naweza Kufanya Mambo Mengi


Somo la 22

Mimi Naweza Kufanya Mambo Mengi

Madhumuni

Ni kumsaidia kila mtoto kuelewa kwamba kama watoto wa Baba wa Mbinguni kila mmoja sisi anaweza kufanya mambo mengi.

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze 1 Samweli 17.

  2. Wasiliana na wazazi wa kila mtoto katika darasa lako ili kujua kitu kimoja ambacho mtoto anaweza kufanya vyema au anajifunza kufanya.

  3. Andaa vipande vya karatasi vilivyo na maelekezo rahisi, kama vile kupiga makofi, kuhesabu hadi tatu, kutembea chumbani, kuruka, kuchora duara (ubaoni au kwenye kipande cha karatasi) kusimama kwa mguu mmoja, kukunja mikono, au kuonyesha kitu ambacho ni rangi ya bluu. Andaa angalao vipande vingi vya karatasi kadiri iwezekanavyo kulingana na idadi ya watoto darasani. Chukua tahadhari juu ya watoto katika darasa lako ambao wana ulemavu, na hakikisha kwamba umewajumuisha katika mambo wanayoweza kufanya.

  4. Andika jina la mtoto kwenye kipande tofauti cha karatasi tofauti.

  5. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Biblia.

    2. Ufito mdogo wa kuvulia samaki (kwa hiari; ona somo la 11).

    3. Chombo cha kuweka majina (kwa hiari).

    4. Picha 1-5, Familia na Mtoto (62307); picha 1-10, Sala ya Familia (62275); picha 1-38, Watoto Wakicheza na Mpira; picha 1-50, Naweza Kujivisha Nguo; picha 1-51, Familia Ikifanya Kazi Pamoja (62313); picha 1-52, Daudi Anamuua Goliathi (Sanaa ya Picha za Injili 212; 62073).

  6. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zo zote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Kwa taarifa ya mwalimu: Kuwa msikivu kwa hisia za watoto wo wote katika darasa lako ambao wana ulemavu wa kimwili. Zingatia mambo ambayo miili yao inaweza kufanya, siyo ulemavu wao.

Shughuli za Kujifunza

Mwalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Kunja vipande vya karatasi vilivyo na majina ya watoto na uviweka katika chombo au sakafuni. Acha kila mtoto atumie ufito wa kuvua samaki na akitumia mikono yake kuchukua kipande kimoja cha karatasi. Mwombe mtoto ambaye jina lake limevulia aje kusimama karibu nawe. Liambie darasa kitu fulani mtoto huyu anachoweza kufanya vyema au anajifunza. Rudia mpaka kila mtoto apate zamu ya kuchagua jina na umesema kitu fulani kuhusu kila mtoto. Wapongeze watoto kwa kile wanachoweza kufanya na wanachojifunza kufanya.

Miili yetu inaweza kufanya mambo mengi

Wimbo

Imba “I Am a Child of God” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 2), pamoja na watoto.

Mimi ni mtoto wa Mungu,

Kanileta hapa,

Kanipa makao mema

Na wazazi wema

Niongoze, kaa nami,

Unifundishe,

Unionyeshe njia,

Ya kujia kwako.

  • Baba wa roho yako ni nani?

  • Ni nani aliyekutuma wewe hapa duniani ili kupata mwili?

Rejea pamoja na watoto kwamba Baba wa Mbinguni alipanga sisi tuje duniani ili tupate miili. Elezea kwamba yeye anatutaka sisi tujifunze mambo mengi kwa miili yetu na anatutaka tutumie miili yetu kwa njia sahihi ili tuweze kuwa kama yeye.

  • Unaweza kufanya nini na mikono yako? miguu yako? mdomo wako? macho yako?

Onyesha picha 1-5, Familia na Mtoto Mchanga.

  • Unafikiri mtoto mchanga huyu anaweza kufanya nini?

Uliza maswali yafuatayo au yanayofanana nayo ili kuonyesha mambo maagapi watoto wamejifunza kufanya tangu walipokuwa watoto wachanga.

  • Mtoto mchanga anaweza kutembea?

  • Mtoto mchanga anaweza kuzungumza?

  • Mtoto mchanga anaweza kujilisha?

  • Mtoto mchanga anaweza kujivisha?

  • Mtoto mchanga anaweza kujipindua?

  • Mtoto mchanga anaweza kuimba wimbo?

  • Mtoto mchanga anaweza kuendesha baiskeli ya magurudumu matatu?

Elezea kwamba watoto wanakua na kwamba watajifunza kufanya mambo mengi zaidi. Moja kwa wakati, onyesha picha 1-10, 1-38, 1-50, na 1-51. Acha mtoto mmoja ainue picha huku watoto wengine wakielezea kile kinachotendeka katika picha hiyo. Baada ya watoto kujibu, wapongeze wao kwa mambo waliyotambua kwamba miili yao inaweza kufanya.

Shughuli

Acha kila mtoto achague kipande kilicho na maelekezo yaliyoandikwa juu yake. Soma maelekezo kwa sauti na uache mtoto mmoja afanye kile yanachosema. Acha kila mtoto apate zamu moja.

  • Je, unajifunza kufanya nini sasa?

  • Unataka kujifunza nini ili kikifanya utakapokuwa mkubwa?

Waambie watoto jinsi ulivyo na shukrani kwa Baba wa Mbinguni kwamba tuna miili ambayo inaweza kufanya mambo mengi.

Baba wa Mbinguni anaweza kutusaidia kufanya mambo mengi

Waambie watoto kwamba wakati mwingine tunaombwa kufanya mambo ambayo ni magumu.

  • Ni nini ambacho umeshajaribu kufanya ambacho ni kigumu?

  • Ni nani anaweza kutusadia kufanya mambo haya? (Wazazi, kaka na dada na walimu.)

  • Kwa nani tunaweza kuomba msaada tunapokuwa tunatakiwa kufanya jambo gumu? (Baba wa Mbinguni.)

Elezea kwamba Yesu Kristo anaweza kutusaidia wakati mambo yanapokuwa magumu.

Hadithi

Onyesha picha 1-52, Daudi Anamuua Goliathi, na usimulie hadithi ya Daudi na Goliathi, kama inavyopatikana katika 1 Samweli 17. Elezea kwamba Yesu alimsaidia Daudi kufanya jambo gumu.

Ushuhuda

Elezea jinsi ulivyo na shukrani kwa Baba wa Mbinguni kwa mwili wako na mambo mengi unayoweza kufanya. Watie moyo watoto kumwomba Baba wa Mbinguni awasaidie wao kutumia miili yao ili kufanya mambo mema.

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo.

  1. Pamoja na watoto, imbeni ”Do As I’m Doing” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto uk. 276), au “Fun to Do” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto uk. 253) na mkifanya vitendo viinavyofaa. Acha watoto wapendekeze vitendo kwa mistari ya nyongeza.

  2. Wape watoto karatasi na krayoni, na uache kila mtoto achore picha ya kitu kimoja au vingi anavyoweza kufanya. Andika Mimi naweza kufanya mambo mengi kwenye kila karatasi la mtoto.

  3. Wasadie watoto kuamua juu ya kitu wanachoweza kufanya nyumbani ili kumsaidia mtu fulani, kama vile kupanga meza, kufagia sakafu, au kulisha mnyama wa nyumbani. Wakumbushe wao kuwaambia wazazi wao juu ya hilo baada ya masomo ya darasa la Msingi ili wazazi wao waweze kuwasaidia kukumbuka kufanya.

  4. Rudia baadhi ya shughuli zinazofaa katika somo la 16 hadi 20.

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Wasaidie watoto kuimba au kusema maneno yafuatayo kwa tuni ya “Once There Was a Snowman” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 249). Wakitumia vitendo vya kuchuchumaa kwa mstari wa kwanza na vitendo vya kujinyoosha kwa mstari wa pili.

    Wakati mmoja nilikuwa mtoto mchanga, mchanga, mchanga,

    Wakati mmoja nilikuwa mtoto mchanga, mdogo, mdogo, mdogo.

    Sasa ninakua mkubwa, mkubwa, mkubwa,

    Sasa ninakua mkubwa, mrefu, mrefu, mrefu!

    Waache watoto waongee kuhusu mambo ambayo wamejifunza na kufanya tangu walipokuwa watoto wachanga.

  2. Onyesha kwa kitendo kama vile kuruka, kupiga makofi, kurukaruka, na waombe watoto wataje kile ambacho wewe unafanya. Kisha acha watoto wafanye kitendo hicho hicho. Mpe kila mtoto nafasi ya kuonyesha kitendo. Waalike watoto wengine waseme ni kitendo gani na kisha wakiigize.

Chapisha