Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 46: Kuzaliwa kwa Yesu Kristo (Krismasi)


Somo la 46

Kuzaliwa kwa Yesu Kristo (Krismasi)

Madhumuni

Ni kumsaidia kila mtoto kuhisi shukrani kwa ajili ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo.

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze Mathayo 2:1–12 na Luka 1:26–35; 2:1–20.

  2. Tafuta utondoti rahisi mchache juu ya kuzaliwa kwa watoto walio katika darasa lako, kama vile walizaliwa wapi, walikuwa na nywele za rangi gani, na waliishi wapi wiki ya kwanza ya maisha yao. Uwe mwangalifu kwa hisia za watoto wo wote walioasiliwa.

  3. Kata papi za karatasi (takribani 8” urefu na 11/2” upana) kwa ajili ya kutengeneza minyororo ya Krismasi. Kata papi za kutosha kutengeneza mnyororo mfupi kwa kila mtoto.

  4. Andika taarifa fupi ukielezea kuhusu mnyororo wa Krismasi (tazama somo) kwa wazazi wa kila mtoto, ili wamhimize mtoto wao kufanya matendo ya ukarimu.

  5. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Biblia.

    2. Mandhari madogo ya kuzaliwa kwa Yesu. Ukitaka waweza kutumia mwanasesere aliyefunikwa kwa blangeti, akiwa amelala kwenye kisanduku kidogo. Kata nyota kutoka kwenye karatasi na uitundike kwenye mandhari ya kuzaliwa kwa Yesu. Kama mandhari hayawezi kupatikana, tumia picha 1‑75, Kuzaliwa kwa Yesu Kristo (Sanaa ya Picha za Injili 200; 62116).

    3. Krayoni rangi na gundi.

    4. Picha 1‑75, Kuzaliwa kwa Yesu Kristo (Sanaa za Picha za Injili 200; 62116); picha 1‑76, Hamna Chumba katika Nyumba ya Wageni (62115); picha 1‑77 Matangazo ya Kuzaliwa kwa Kristo kwa Machungaji (Sanaa za Picha za Injili 202; 62117); picha 1‑78, Mamajusi (Sanaa za Picha za Injili 203; 62120).

  6. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zozote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Shughuli za Kujifunza

Mwaalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Acha mtoto asimame karibu nawe unaposema kuhusu utondoti unaojua kuhusu kuzaliwa kwake. Rudia kwa kila mtoto katika darasa.

Tunasherekea kuzaliwa kwa Yesu Kristo wakati wa Krisimasi

Elezea kwamba kwa vile huu msimu wa Krismasi, tunasherekea kuzaliwa kwa mtu ambaye sisi wote tunampenda.

  • Ni kuzaliwa kwa nani ambako sisi tunasherekea?

Hadithi

Simulia hadithi ya matembezi ya malaika kwa Mariamu, kama inavyopatikana katika Luka 1:26–35. Elezea kwamba malaika alimwambia Mariamu kwamba angekuwa mama wa Mwana wa Mungu.

  • Jina la Mama ya Yesu Kristo ni nani? (Ona Luka 1:27.)

  • Ni nani alikuwa baba ya Yesu? (Baba wa Mbinguni. Ona Luka 1:35.)

Elezea kwamba Yusufu hakuwa baba wa Yesu. Yeye alikuwa mtu mwema aliyechaguliwa kumlea Yesu. Malaika alimjia Yusufu katika ndoto na akamwambia kuhusu mtoto muhimu ambaye Mariamu angempata. Malaika alimwambia Yusufu kwamba ilibidi Mariamu awe mke wake.

Hadithi

Onyesha picha 1-76, Hamna chumba katika Nyumba ya Wageni, na waambie kuhusu safari ya Yusufu na Mariamu kutoka Nazareti hadi Bethlehemu, kama inavyopatikana katika Luka 2:1–7. Soma Luka 2:7 kwa sauti, ukielezea neno lolote ambalo linaweza kuwa geni kwa watoto.

Shughuli

Acha watoto wakae chini au wapige magoti mbele ya mandhari ya kuzaliwa kwa Yesu. Ukitaka unaweza kuwapatia blangeti la kukalia. Pitisha picha 1-75, Kuzaliwa kwa Yesu, na acha kila mtoto asimulie kuhusu kitu kimoja anachokiona katika picha hii.

  • Kwa nini Mariamu na Yusufu hawakulala katika nyumba ya wageni? (Ona Luka 2:7.)

  • Yesu Kristo alizaliwa wapi? (Katika zizi la ng’ombe.)

  • Ni aina gani ya kitanda ambacho Mariamu alimlaza mtoto Yesu? (Ona Luka 2:7.)

Wimbo

Wasaidie watoto kuimba au kusema maneno “Away in a Manger” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, p. 42). Tunga mwendo wa mikono unaoendana na maneno.

Mbali horini, kwake hamna pa kulala.

Mdogo Bwana Yesu kalala usingizi mwanana;

Nyota za mbinguni zatazama alipolala,

Mdogo Bwana Yesu, kalala kwenye nyasi kavu.

Hadithi

Onyesha picha 1-77, Tangazo la Kuzaliwa kwa Kristo kwa Wachungaji, na wasimulie kuhusu matembezi ya wachungaji, kama ilivyoelezewa katika Luka 2:8–20.

  • Kwa nini wachungaji walikuwa na hofu? (Ona Luka 2:9.)

  • Ni nini malaika aliwaambia wachungaji? Ona Luka 2:10–12.

  • Wachungaji walifanya nini walipomtembelea mtoto Yesu? (Ona Luka 2:17, 20.)

Hadithi

Onyesha picha 1-78, Mamajusi, na usimulie kuhusu matembezi ya mamajusi, kama ilivyoelezewa katika Mathayo 2:1–12.

Shughuli

Acha watoto wasimame na kujifanya wao wamepanda ngamia wakizunguka chumbani, wakiifuata nyota ambayo iliwaongoza wao kwa mtoto Yesu.

Baada ya safari kadhaa chumbani, acha watoto washuke kutoka kwenye ngamia wao na kuja tena kwenye mandhari ya kuzaliwa. Elezea kwamba hadi kufikia wakati mamajuzi walipompata mtoto Yesu, Yusufu alikuwa ameshapata sehemu bora ya familia kuishi na walikuwa hawaishi katika zizi la ngome. Wakumbushe watoto kwamba mamajusi walileta zawadi za dhahabu, uvumba na manemane. Acha kila mtoto aeleze kama zawadi yake ya kujifanya ni dhahabu, uvumba au manemane na kisha amzawadie mtoto Yesu.

Zawadi yetu kwa Yesu ni kuwa kama Yeye

Elezea kwamba kila Krismasi tunaposherekea kuzaliwa kwa Yesu, tunaweza kumpa zawadi. Hatuwezi kutoa dhahabu, uvumba, na manemane kama mamajusi, lakini tunaweza kutoa aina nyingine ya zawadi. Tunampatia Yesu zawadi wakati tunapojaribu kuwa kama Yeye. Tunakuwa kama Yesu wakati tunapokuwa wakarimu kwa familia na marafiki zetu.

Shughuli

Msaidie kila mtoto atengeneze mnyororo wa Krismasi ulio na viungo kadhaa. Acha watoto wapake rangi viungo vyao na kugandisha kwa gundi viungo hivyo pamoja (ona kielelezo hapo mwisho wa somo). Waambie watoto waweke minyororo yao mahali fulani nyumbani mwao pale inapoweza kuwakumbusha kufanya matendo mema kwa wengine kama zawadi kwa Yesu. Wapatie watoto changamoto ya kufanya angalao kitendo kimoja cha ukarimu kila siku hadi Krismasi.

Wasaidie watoto wafikirie aina ya matendo ya ukarimu wanayoweza kufanya. Wakumbushe kwamba wanapofanya tendo ya ukarimu, wanatoa zawadi ya nzuri kwa Yesu. Mpe kila mtoto taarifa inayoelezea kuhusu mnyororo huo kwa wazazi wake.

Ushuhuda

Elezea kwamba kuzaliwa kwa Yesu Kristo ilikuwa ni mojawapo ya mambo muhimu yaliyotendeka ulimwenguni. Onyesha upendo wako kwa Yesu na hamu yako ya kuwa kama Yeye, sio tu wakati wa Krismasi bali mwaka mzima.

Shughuli zenye Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo.

  1. Simulie tena hadithi ya kuzaliwa kwa Yesu wakati watoto wakiigiza sehemu za Yusufu, Mariamu, Mwenye nyumba ya wageni, wachungaji, na mamajusi. Tumia viwakilishi kama vile mtoto mwanasesere, blangeti dogo, na mtandio, kama vinaweza kupatikana. Mpe kila mtoto nafasi ya kushiriki. Ukitaka unaweza kurudia shughuli hii, kwa kuwaruhusu watoto wachukue nafasi tofauti.

  2. Wasaidie watoto kukata au kuchora mapambo ya nyota rahisi. Acha watoto wapake rangi mapambo yao, na kuunga kwa uzi kila nyota ili mtoto aweze kutundika mahali fulani nyumbani mwao.

  3. Jadili baadhi ya maandalizi ya kibiashara kwa ajili ya Krismasi ambayo watoto wameyaona. Wasaidie kuelewa kwamba vitu kama vile zawadi na karamu hufurahisha, lakini Krismasi hasa ni juu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo na umuhimu wa kulenga juu yake Yeye na maisha Yake.

  4. Jadili desturi za kawaida katika eneo lenu ambazo Kristo - ndiye kitovu chake ambazo wewe unapendelea au unazifahamu. Waalike watoto wazungumze kuhusu tamaduni ambazo Kristo -ndiye kitovu chake ambazo familia zao hufurahia wakati wa Krismasi.

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Acha watoto wajifanye kuwa wachungaji wanaopumzika malishoni. Wasadie kuigiza wakionyesha hofu ambayo wachungaji waliona wakati walipomwona malaika, kisha furaha waliojisikia wakati walipoelewa taarifa hizo. Wasaidie kufikiria kuwasikia malaika wakiimba na kulitazama anga maridadi la usiku na kuiona nyota ile. Wakitembea pamoja chumbani wakimtafuta mtoto. Wakipiga magoti mbele za mtoto Yesu katika hori, na kuimba wimbo wa sifa.

  2. Wasaidie watoto kufanya vitendo vya mstari ufuatao unaposema maneno haya:

    Mtoto katika hori (pembeza mikono kama vile kumbembeleza mtoto),

    Mama mwenye upendo karibu (mikono ya kupokea),

    Nyota iking’aa mbinguni (hali ya kushangaza angani),

    Mwana wa Mungu yu hapa (kupiga makofi ya shangwe)!

  3. Imba au mseme maneno “Little Jesus” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 39, au ”Jesus Said Love Everyone” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 61). Wakumbushe watoto kwamba sisi husherekea kuzaliwa kwa Yesu wakati wa Krismasi.

  4. Tengeneza karatasi za kukata za Yesu Kristo kama amefunikwa nguo. Kusanya nyasi kavu, au majani makavu na uyalete kwa watoto ili wayagundishe kuwa “hori” (karatasi ya mraba) Acha watoto wagundishe karatasi ya kukata ya mtoto Yesu juu ya kitanda cha nyasi au majani makavu.

Picha
mnyororo wa karatasi

Chapisha