Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 27: Tunaweza Kuomba Kama Familia


Somo la 27

Tunaweza Kuomba Kama Familia

Madhumuni

Ni kumsaidia kila mtoto kuelewa kwamba maombi ya familia ya kila mara husaidia familia kuhisi kuwa karibu na Baba wa Mbinguni na kila mmoja.

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze Alma 34:19–27 na 3 Nefi 18:17–21. Ona pia Kanuni za Injili (31110), sura ya 8.

  2. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Kitabu cha Mormoni

    2. Mkato 1-26, baba; mkato 1-27, mama; mkato 1-28, msichana mdogo; mkato 1-29, mvulana umri wa mmisionari (mikato kama hiyo pia inaweza kupatikana katika Mikato ya Vielelezo vya Picha ya Msingi seti 1).

    3. Picha 1-10, Maombi ya Familia (62275); picha 1-15, Kubariki Chakula; picha 1-44, Yesu Akifundisha katika Ulimwengu wa Magharibi (Picha za Sanaa za Injili 316; 62380).

  3. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zo zote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Shughuli za Kujifunza

Mwalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Waulize watoto wasimulie kuhusu kitu ambacho wao hufanya pamoja na familia zao. Mpe kila mtoto nafasi ya kueleza. Onyesha picha 1-10, Maombi ya Familia.

  • Familia hii inafanya nini?

Elezea kwamba tunapoomba kama familia, tunafanya kitu ambacho Baba wa Mbinguni na Yesu wanataka tufanye. Kuomba kama familia kunaitwa maombi ya familia.

Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanatutaka tuombe pamoja na familia zetu

Hadithi

Onyesha picha 1-44, Yesu Anafundisha katika Ulimwengu wa Magharibi. Simulia kuhusu Yesu Kristo alipowatembelea Wanefi na kuwaamuru wao kuomba, kama ilivyoelezwa katika 3 Nefi 18:17–22. Waonyeshe watoto Kitabu cha Mormoni na usome 3 Nefi 18:21 kwa sauti. Wasaidie watoto kuelewa kwamba Yesu anataka sisi tuombe pamoja na familia zetu. Kama vile tu watoto Wakinefi walibarikiwa kupitia maombi ya familia, vivyo hivyo tunaweza kubarikiwa kupitia maombi ya familia.

Tunaweza kuwa na maombi ya familia kila siku

Elezea kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu wanataka tuombe pamoja na familia zetu kila asubuhi na kila usiku. Kwa kawaida baba au mtu aliye na majukumu ya familia anaweza kumchagua mtu yeyote aombe. Mtu yeyote katika familia anaweza kutoa maombi ya familia.

  • Tunaweza kuomba na familia zetu wakati gani?

  • Ni nani anayeweza kuomba?

Wimbo

Imbeni au semeni maneno ya “Family Prayer” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 189).

Acha tukusanyike katika duara.

Na tupige magoti katika maombi ya familia

Kumshukuru Baba yetu wa Mbinguni

Kwa ajili baraka tunazopata wote.

  • Tunasema nini katika maombi ya familia?

Elezea kwamba tunasema maneno yale yale ya ukarimu katika maombi ya familia jinsi hiyo hiyo tunavyosema katika maombi binafsi asubuhi na usiku. Lakini katika maombi ya familia tunasema mambo ambayo yanahusu familia yote, wala si yetu wenyewe tu.

Wimbo

Rejea mambo ambayo sisi husema tunapoomba kwa kuimba au kusema maneno ya mistari miwili ya kwanza ya “I Pray in Faith” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 14).

Mimi huanza kwa kusema “Baba Mpendwa wa Mbinguni”;

Namshukuru kwa ajili ya baraka anazotoa;

Kisha kwa unyenyekevu naomba vitu ambavyo ninahitaji,

Katika jina la Yesu Kristo, Amina.

(© 1987 by Janice Kapp Perry. Imetumika kwa Idhini.)

  • Tunasema nini mwanzoni mwa maombi?

  • Tunasema nini mwishoni mwa maombi?

  • Kila mtu mwingine anapaswa kufanya nini wakati maombi yanapotolewa.

Elezea kwamba kwa kusema “amina” mwishoni mwa maombi humaanisha tunakubaliana na kile kilichosemwa katika maombi.

Onyesha picha 1-15, Kubariki Chakula. Elezea kwamba sisi pia tuaomba kama familia tunapoomba baraka kwa ajili ya chakula chetu.

  • Tunafanya nini tunapoomba baraka kwa ajili ya chakula? (Tunamshukuru Baba wa Mbinguni kwa chakula na tunamwomba akibariki.)

  • Ni nani hutoa moambi ili kumwomba Baba wa Mbinguni akibariki chakula?

Wimbo

Imba aya ya pili ya “I Pray in Faith” tena.

Tunapokea baraka nyingi kwa kuomba pamoja kama familia

Hadithi

Ukitumia mkato 1-26, hadi 1-29, simulia hadithi kuhusu familia inayoomba pamoja kwa ajili a mwanafamilia ambaye anahudumu katika misheni. Unaweza kutaka kutumia mawazo yafuatayo:

Catherine alikuwa msichana mdogo. Aliipenda familia yake na alijua ilikuwa inampenda. Wakati fulani Paul kaka yake mkubwa alimsimulia kutoka kwenye Biblia na Kitabu cha Mormoni. Paul alikuwa anajifunza vitabu hivi kwa sababu alikuwa anataka kwenda misheni na kuwaambia watu wengine juu ya vitabu hivyo.

Siku moja Paul alipokea barua. Alipofungua ile barua, alichangamka. “Mimi naenda misheni” alisema. Wiki chache baadaye, Paul alikuwa tayari kwenda. Kabla ya kuondoka, familia ilipiga magoti katika maombi ya familia. Babake Catherine alimshukuru Baba wa Mbinguni kwa ajili ya baraka nyingi familia yao ilipata na kwa nafasi ya Paul ya kwenda misheni. Alimuomba Baba wa Mbinguni kumbariki Paul, na kumlinda, na kumsaidia yeye awe mmisionari mwema. Maombi yalimfanya Catherine afurahi moyoni. Alijua kwamba Baba wa Mbinguni angemsaidia Paul katika misheni yake. Catherine na familia yake walimwombea Paul kila siku alipokuwa katika misheni yake.

Elezea kwamba familia zinaweza kuomba pamoja kwa ajili ya mtu ambaye ni mgonjwa, kwa msaada wa shida katika familia, kwa ajili mmisionari ambaye anahitaji msaada wa Baba wa Mbinguni, na kwa ajili ya sababu zingine nyingi. Elezea kwamba tunaweza kuomba kwa ajili cho chote ambacho ni muhimu kwetu. Tumia Alma 34:19–27 ili kuwsaidia watoto kuelewa jinsi ya kuomba.

Soma 3 Nefi 18:21 kwa sauti tena. Wakumbushe watoto kwamba Yesu aliahidi tutabarikiwa kama tutafanya maombi ya familia.

Ushuhuda

Toa ushuhuda wako juu ya maombi ya familia. Ukitaka unaweza kuzungumza kuhusu wakati ambapo maombi ya familia yaliimarisha familia yako mwenyewe.

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo.

  1. Fanya mstari wa shughuli ufuatao pamoja na watoto:

    Huyu ni mama yangu, ambaye hunisaidia kucheza (inua kidole cha kwanza);

    Huyu ni baba yangu, ambaye hufanya kazi siku nzima (Inua kidole cha pili).

    Huyu ni kaka yangu, mwenye nguvu na mrefu (inua kidole cha tatu);

    Huyu ni dada yangu, ambaye anapenda kucheza mpira (inua kidole cha nne).

    Na huyu ni mimi; nina furaha kusema (onyesha kidole gumba)

    Kwa Pamoja familia yetu hupiga magoti kuomba (funga ngumi).

  2. Rusha au peana kitu laini kama vile kijifuko cha maharagwe au mpira kwa watoto, mmoja mmoja. Baada ya watoto kishika chombo, waulize wataje jina la kitu wanachoweza kumshukuru Baba wa Mbinguni kwa ajili yake wakati wanapoomba maombi ya familia. Baada ya kila mtoto kupata zamu, rudia shughuli hii, watoto wakitaja mambo wanayoweza kumshukuru Baba wa Mbinguni kwa ajili yake wanapoomba maombi ya familia.

  3. Mpe kila mtoto kipande cha karatasi na krayoni au penseli. Acha watoto wachore picha inayoonyesha familia yao ikiomba. Andika kila picha Nina furaha familia yangu inapoomba pamoja.

  4. Imbeni au semeni maneno ya “A Song of Thanks” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 20) au “A Prayer Song” (Kitabu cha Nyimbo cha Watoto, uk.22).

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Wasaidie watoto kurudia aya hii, mstari kwa mstari:

    Tunampenda Baba wa Mbinguni.

    Tunamshukuru tunapoomba.

    Baba wa Mbinguni anatupenda;

    Yeye husikia maneno tunayosema.

  2. Simulia hadithi ya familia ikiomba pamoja na kupokea msaada uliohitajika. Kwa mfano, familia inaweza kupotea njia na kisha wakaipata; wanaweza kupoteza kitu fulani na kisha kukipata; mtu fulani katika familia anaweza kuwa anaumwa na kisha kujisikia vyema. Pendekeza kwamba hata zaidi ya kuomba kwa ajili ya msaada, familia zinapaswa kutoa maombi ya shukrani baada ya kupokea msaada waliohitaji. Wakumbushe watoto kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu hufurahia tunapowashukuru kwa ajili ya baraka wanazotupa.

  3. Imbeni au semeni maneno ya aya ya kwanza na ya tatu ya “Thanks to Our Father” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 20).

Chapisha