Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 6: Baba wa Mbinguni na Yesu Wananipenda Mimi


Somo la 6

Baba wa Mbinguni na Yesu Wananipenda Mimi

Madhumuni

Ni kumsidia kila mtoto kuelewa kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu wanampenda kila mmoja wetu.

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze Marko 10:13–16; na Yohana 3:18; na 3 Nefi 17:11–12, 21-24.

  2. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Biblia na Kitabu cha Mormoni

    2. Kioo kidogo.

    3. Picha 1-1, Ulimwengu (62196);Picha 1-3, Yesu Kristo (Sanaa ya Picha za Injili 240; 62572); picha 1-4, Ono la Kwanza (Sanaa ya Picha za Injili 403; 62470);Picha 1-19, Kristo na Watoto (Sanaa ya Picha za Injili 216; 62467); picha 1-20, Yesu Akiwabariki Watoto Wakinefi.

  3. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zo zote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Shughuli za Kujifunza

Mwalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Msalimu kila mtoto kwa mkono. Sema jina la kila mtoto na umwambie kila mmoja kitu fulani unachokipenda juu yake yeye.

Muulize kila mtoto jina la mtu mmoja ambaye anampenda na aseme kile ambacho mtu huyo hufanya hata kumfanya yeye ahisi kuwa anapendwa.

Elezea kwamba somo hili linahusu watu wawili wanaotupenda sisi wote. Wao walitupa ulimwengu huu maridadi na injili na Kanisa.

  • Hawa watu wawili ni kina nani ambao wanampenda kila mtu? (Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.)

Hadithi

Onyesha picha 1-4, Ono la Kwanza. Acha watoto wakusaidie kusimulia hadithi ya kile kinachotendeka katika picha hii.

  • Je, unakumbuka watu walio katika picha hii ni kina nani?

  • Wanafanya nini?

Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo hutupatia baraka

Wakumbushe watoto kwamba kabla ya kuja duniani, tuliishi pamoja na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo. Wao walipanga sisi tuje duniani ili tuweze kujifunza na kukua. Wanatujua na wanatujali.

Onyesha picha 1-1, Ulimwengu.

  • Baba wa Mbinguni alimwomba Yesu aumbe nini kwa ajili yetu?

Elezea kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu waliumba dunia na kila kitu kilichopo ndani yake. Wasaidie watoto kuelewa kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu walipanga vitu vyote tunavyohitaji ili tuishi na kuwa na furaha. Vitu hivi vinatukumbusha sisi juu ya upendo wao kwetu.

  • Ni vitu gani vinakukumbusha wewe juu ya upendo wa Baba wa Mbinguni kwako? (Majibu yanaweza kujumuisha vitu kama vile familia, marafiki, Kanisa, mimea, na wanyama.)

Wimbo

Imbeni au semeni maneno ya “My Heavenly Father Loves Me” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto , 228) mkitumia vitendo vinavyoonyeshwa hapo chini. Kisha waombe watoto wasimame na kuimba wimbo pamoja nawe.

Ninaposikia (weka mikono kwenye masikio) wimbo wa ndege (fungua na ufunge vidole mfano wa mdomo wa ndege)

Au kutazama (tazama juu) kwenye anga samawati, samawati (inue mikono katika mwendo wa tao).

Wakati wowote nionapo mvua usoni mwangu (fanya mwendo wa matone ya mvua kwa vidole)

Au upepo unapovuma (mwendo wa mikono yote mbele na nyuma)

Wakati wo wote nigusapo ua waridi (jifanye unagusa au kunusa ua)

Au kutembea karibu na mti wetu wa lilaki (tembea hapo hapo),

Mimi nashukuru naishi katika ulimwengu huu maridadi

Baba wa Mbinguni aliuumba kwa ajili yangu (fungua viganja na unyoshe mikono).

Onyesha picha 1-3, Yesu Kristo.

  • Je, hiki ni nani?”

  • Baba wa Yesu ni nani?

Soma sehemu ya kwanza ya Yohana 3:16 (hata kufikia Mwana) na ueleze kwamba baraka kuu ambayo Baba wa Mbinguni ameshatupa ilikuwa ni kumleta Yesu Kristo ulimwenguni.

Yesu alionyesha upendo wake kwa watoto

Hadithi

Onyesha picha 1-19, Yesu na Watoto. Simulia hadithi ya Yesu akiwabariki watoto, kama inavyopatikana katika Marko 10:13–16.

Onyesha wazi kwamba Yesu alitumia muda mwingi kuwapenda na kuwabariki watoto licha ya kwamba baadhi ya wafuasi wake walifikiria hapaswi kujishughulisha na watoto.

  • Yesu alifanya nini wakati watoto walikuja? (Ona Marko 10:16.)

  • Unafikiri watoto walijisikiaje juu ya Yesu?

Wimbo

Pamoja na watoto imbeni au semeni maneno ya “Jesus Loved the Little Children” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, p. 59).

Yesu aliwapenda watoto wadogo,

Watoto wadogo kama mimi.

Angewabariki na kuwasaidia

Na kuwaleta magoti mwake.

Hadithi

Onyesha picha 1-20, Yesu Akiwabariki Watoto Wakinefi. Elezea kwamba baada ya Yesu kufa, aliwatembelea watu wa Amerika. Amerika ilikuwa mbali sana kutoka pale alipoishi Yesu duniani.

Simulia hadithi ya Yesu akiwabariki watoto Wakinefi, kama inavyopatikana katika 3 Nefi 17:11–12, 21–24. Elezea kwamba Yesu alimbariki kila mtoto binafsi.

  • Ni kwa jinsi gani Yesu alionyesha upendo kwa watoto?

  • Unajuaje kuwa Yesu anakupenda?

Shughuli

Kariri mstari ufuatao pamoja na watoto mara kadhaa, mkifanya vitendo vilivyoonyeshwa:

Yesu Anawapenda Watoto Wote

Yesu anawapenda watoto wote (nyosha mikono wazi);

Wadogo bado wadogo sana (tumia mikono kuashiria mtoto wa kimo cha ngoti),

Mtoto mchanga katika susu (tenegeza susu kwa mikono),

Wengine wakubwa na warefu (inua mikono juu ya kichwa).

(Ona Finger Fun for Little Folk na Thea Cannon. © 1949 na Standard Publishing Company, Cincinnati, Ohio. Imetumika kwa Idhini.)

Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanampenda kila mmoja wetu

Wasaidie watoto kuelewa jinsi kila mmoja wao alivyo muhimu kwa Baba wa Mbinguni na Yesu. Elezea kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu wanampenda kila mmoja wetu na wanatujua kwa jina.

Shughuli

Inua kioo juu na uwaache watoto waje mmoja baada ya mwingine. Kila mtoto anapokuja na kutazama katika kioo, sema, “”Huyu ni (jina mtoto), na Baba wa Mbinguni na Yesu wanampenda (jina mtoto) sana)”

Ushuhuda

Toa ushuhuda kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanaishi na kwamba wanampenda kila mmoja wetu. Shiriki hisia zako za shukrani kwa ajili ya baraka nyingi ambazo Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wamekupatia.

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo hilo.

  1. Imbeni au semeni maneno ya “Jesus Is Our Loving Friend” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 58). Mpe kila mtoto nakala za kitini cha “Jesus is Our Loving Friend,” kama inayopatikana (mwishoni wa somo) na acha watoto wapake rangi vitini vyao.

  2. Imbeni ua semeni maneno ya “Thanks to Our Father” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 5) au “I Feel My Savior’s Love” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk.74).

  3. Onyesha picha za vitu ambavyo Baba wa Mbinguni na Yesu wametupatia, kama vile hekalu, wanyama, maua, familia, chakula, nyumba, majumba ya mikutano, au maandiko. (Picha zinaweza kupatikana kutoka maktaba ya jumba la mikutano, Sanaa ya Picha za injili, au magazeti ya Kanisa. Wasaidie watoto kuelewa kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu wametupatia vitu hivi kwa sababu wanatupenda.

  4. Leta kitu, kama vile chupa ya kinywaji tupu, ambayo inaweza kuzunguka kama mshale. Wakalishe watoto chini katika duara na uweke chupa katikati ya duara. Zungusha chupa sakafuni. Wakati inamlenga mtoto, mtoto yule anapaswa kusema kitu ambacho Baba wa Mbinguni na Yesu wametupa ambacho kinaonesha upendo wao kwetu. Msaidie kila mtoto kufikiria jibu inapofika zamu yake. Baada ya mtoto kujibu, acha azungushe chupa ili imlenge mtoto mwingine.

  5. Andaa sanduku au mfuko ambao una vitu kadhaa ambavyo ni muhimu kwetu ili kuishi duniani, kama vile chakula, maji, au nguo. Elezea kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu waliipanga dunia hii kwa ajili ya sisi kuishi ndani yake. Elezea kwamba sanduku au mfuko una baadhi ya vitu ambavyo tunavihitaji ili kuishi duniani. Wape watoto vidokezo kuhusu kitu kimoja na mpaka wabahatishe ni nini. Wanapobahatisha ni nini, kitoe kutoka kwenye sanduku au mfuko. Endelea na mchezo mpaka watoto wabahatishe vitu vyote.

  6. Tengeneza beji ambayo inasema Baba wa Mbinguni na Yesu Wananipenda kwa kila mtoto ili avalie au achukue nyumbani. Unaweza kunganisha beji kwa mtoto au kuunga kamba kwenye beji na kumvisha mtoto shingoni. Unaweza kuzificha beji chini ya viti vya watoto kabla ya darasa na kuwaacha watoto wazitafute.

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Wasaidie watoto kusema maneno na kufanya vitendo vya mstari ufuatao.

    Kama wewe ni mrefu, mrefu sana (jinyoshe na mikono juu sana)

    Kuna nafasi kanisani kwa ajili yako.

    Kama wewe ni mdogo, mdogo sana (chuchumaa chini),

    Kuna nafasi kanisani kwa ajili yako.

    Mrefu (jinyoshe)

    Mdogo (chuchumaa)

    Mrefu (jinyoshe)

    Mdogo (chuchumaa)

    Baba wa Mbinguni na Yesu Wanatupenda wote.

  2. Semeni mstari ufuatao na wasaidie watoto kufanya vitendo vinavyoelezwa:

    Baba wa Mbinguni Ananijua

    Baba wa Mbinguni ananijua (jiote mwenyewe)

    Na kile mimi ninapenda kufanya.

    Yeye anajua jina langu na pale ninapoishi (tengeneza paa kwa kugusanisha vidole vya mikono yote).

    Mimi najua ananipenda, pia (pitisha mikono na uweke mikono nyuma ya mabega kama kumbatio).

    Yeye anajua kile kinachonifanya kuwa na furaha (weka vidole kwenye mdomo unao tabasamu).

    Yeye anajua kile kinachonifanya kuwa na huzuni. (weka vidole kwenye mdomo uliogueza kwenda chini).

    Mimi najua anataka kunisaidia (jionyeshe mweyewe);

    Na hiyo inanifanya nisikie furaha!

Yesu Kristo ni Rafiki Yetu Mwenye Upendo

Picha
Yesu pamoja na watoto

Chapisha