Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 5: Yesu Kristo ni Mwana wa Baba wa Mbinguni


Somo la 5

Yesu Kristo ni Mwana wa Baba wa Mbinguni

Madhumuni

Ni kumsaidia kila mtoto kujua kuwa Yesu Kristo ni Mwana wa Baba wa Mbinguni.

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze Mathayo 3:13–17 na Luka 1:26–35; 2:1–7, 41–52. Tazama pia Kanuni za Injili (31110), sura ya 3.

  2. Kwa idhini ya rais wako wa Msingi, mwalike baba wa mmoja wa watoto aje darasani na kuzungumza kuhusu mtoto wake alipokuwa mtoto mchanga. Muombe alete picha na mwanasesere kipenzi, kama inawezekana. Mhimize yeye aelezee upendo wake kwa mtoto wake.

  3. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Biblia.

    2. Picha 1-16, Kuzaliwa kwa Kristo (Sanaa ya Picha za Injili 201; 62495); picha 1-17, Mvulana Yesu Hekaluni (Sanaa ya Picha za Injili 205; 62500); Picha 1-18, Yohana Mbatizaji Akimbatiza Yesu; (Sanaa ya Picha za Injili 208; 62133).

  4. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zo zote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Taarifa kwa mwalimu: Unapozungumza kuhusu akina baba katika somo hili, uwe mwangalifu kwa hisia za watoto katika darasa lako ambao hawana baba nyumbani mwao. Sisitiza kwamba sisi wote tuna Baba wa Mbinguni ambaye anatupenda. Ikiwa baadhi ya watoto katika darasa lako wana baba wa kambo, elezea kwamba baba wa kambo pia wanatupenda na wanatujali sisi.

Shughuli za Kujifunza

Mwalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Waulize watoto kama wanajua mgeni ni nani. Muombe mtoto wa mgeni amtambulishe mgeni kwa darasa. Acha baba awasimulie watoto kuhusu mtoto wake. Acha kila mtoto aseme kitu fulani kuhusu baba yake, kama vile rangi ya nywele au kazi yake.

Yesu Kristo ni mwana wa Baba wa Mbinguni

Waambie watoto kwamba kila mmoja wao ana baba wawili: baba wa duniani na Baba wa Mbinguni. Baba wa duniani ni baba wa miili yetu. Baba wa Mbinguni ni baba wa roho zilizo ndani ya miili yetu. Yesu ana baba mmoja tu, kwa sababu Baba wa Mbinguni ndiye baba wa roho, na wa mwili wake. Hiyo ndiyo sababu Yesu anaitwa Mwana wa Mungu.

Hadithi

Onyesha picha 1-16, Kuzaliwa kwa Kristo, na usimulie hadithi ya kuzaliwa kwa Yesu, kama inavyopatikana katika Luka 1:26–35 na Luka 2:1–7. Sisitiza kwamba malaika alimwambia Mariamu kwamba angekuwa mama wa Mwana wa Mungu. Rejea kwenye picha unapouliza maswali yafuatayo:

  • Mama wa Yesu ni nani?

  • Jina lake ni nani? Tazama Luka 1:27.)

  • Mtu aliye katika picha hii ni nani? (Ona Luka 1:27.)

  • Baba wa Yesu ni nani? (Baba wa Mbinguni. Yusufu alikuwa mtu mwema aliyechaguliwa na Baba wa Mbinguni kumtunza Mariamu na Yesu.)

Wimbo

Wasaidie watoto kuimba au kusema maneno “Away in a Manger” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, p. 42). Tunga mwendo wa mikono unaofaa kuendana na maneno.

Mbali horini, kwake hakuna pa kulala.

Mdogo Bwana Yesu Kristo kalala usingizi mwanana;

Nyota za mbinguni zatazama alipolala,

Mdogo Bwana Yesu Kristo kalalia nyasi kavu.

Yesu anampenda Baba wa Mbinguni na anamtii yeye

Hadithi

Onyesha picha 1-17, Mvulana Yesu Hekaluni, na usimulie hadithi ya Yesu hekaluni, kama inavyopatikana katika Luka 2:41–52. Sisitiza kwamba Yesu alienda hekaluni kwa sababu alimpenda Baba wa Mbinguni na alitaka kuwafundisha watu juu Yake.

  • Je! Yesu anafanya nini hekaluni? (Ona Luka 2:46.)

Shughuli

Acha watoto wasimame na kufanya mstari wa shughuli ufuatao mara kadhaa:

Kijana Yesu alienda hekaluni (tembea hapo hapo)

Kabla hajakuwa na nguvu na urefu (nyoosha mikono juu)

Kufanya kazi ya Baba yake (inua mikono)

Kwa sababu anatupenda sisi wote (jikumbatie mwenyewe).

Hadithi

Onyesha picha 1-18, Yohana Mbatizaji Akimbatiza Yesu, na usimulie hadithi ya ubatizo wa Yesu, kama inavyopatikana katika Luka 3:13–17. Elezea kwamba Yesu alibatizwa kwa sababu alimpenda Baba wa Mbinguni na alitaka kumtii yeye. Yesu pia alitaka kuweka mfano mzuri kwetu. Soma kwa sauti mstari wa 17 (ukianzia Huyu ni Mwanangu Mpendwa), na uelezee kwamba haya ni maneno ya Baba wa Mbinguni. Baba wa Mbinguni alipendezwa kwamba Yesu alibatizwa.

  • Je, umeshuhudia mtu akibatizwa?

Elezea kwamba njia moja ambayo watoto wanaweza kuwa watiifu kwa Baba wa Mbinguni na kumwonyesha yeye kuwa wanampenda ni kwa kubatizwa wanapokuwa na umri wa miaka minane.

Ushuhuda

Toa ushuhuda wako kwamba Yesu ni mwana wa Baba wa Mbinguni. Elezea upendo wako kwa Yesu na shukrani unayohsi kwa ajili yake.

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo.

  1. Weka picha tatu kutoka kwa somo hili, zikitazama chini kwenye paja lako au mezani. Mwalike mtoto achague mojawapo ya picha hizi, ionyeshe kwa darasa, na usimulie hadithi inayoonyeshwa katika picha hiyo. Fanya vivyo hivyo kwa zile picha zingine mbili.

  2. Acha watoto waimbe au kusema maneno ya mstari wa kwanza wa “Tell Me the Stories of Jesus” (Kitabu cha Nyimbo cha Watoto, uk. 57).

  3. Acha watoto wafanye igizo la hadithi ya kuzaliwa kwa Yesu, mkitumia vitu rahisi kama vile mwansesere, shali, na skafu.

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Onyesha picha 1-16, Kuzaliwa kwa Yesu, na waulize watoto huyu mtoto mchanga ni nani. Wasimulie kuhusu kuzaliwa kwa Yesu.

    Elezea kwamba Yesu si mtoto mchanga bado. Sasa ni mtu mzima, na yeye ni msaidizi muhimu sana wa Baba wa Mbinguni. Onyesha picha1-3, Yesu ndiye Kristo, na uwaelezee watoto kwamba Yesu anatupenda na hutusaidia kwa njia nyingi.

  2. Wasaidie watoto kuimba au kusema maneno yafuatayo kwa tuni ya “Once There Was a Snowman” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 249). Wakitumia vitendo vya kuchuchumaa kwa mstari wa kwanza na vitendo vya kujinyoosha kwa mstari wa pili.

    Wakati mmoja nilikuwa mtoto mchanga, mchanga, mchanga,

    Wakati mmoja nilikuwa mtoto mchanga, mdogo, mdogo, mdogo.

    Sasa ninakua mkubwa, mkubwa, mkubwa,

    Sasa ninakuwa mkubwa, mrefu, mrefu, mrefu!

  3. Zungumza na wazazi wa washiriki wa darasa lako mapema ili upate picha za washiriki wa darasa lako wakiwa watoto wachanga au wanasesere wadogo ambao walizoea kucheza nao. Onyesha vitu hivi kwa darasa. Mtambue mtoto mchanga katika kila picha au mmiliki wa kila mwanasesere. Elezea kwamba walipokuwa watoto wachanga walikuwa wanaonekana kama vile picha hizi na walicheza na wanasesere .

Chapisha