Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 28: Naweza kuwa na Staha


Somo la 28

Mimi Naweza Kuwa Mtiifu

Madhumuni

Ni kuimarisha hamu ya kila mtoto kumtii Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo na kuwatii wazazi wake.

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze Yohana 14:15; na Waefeso 6:1. Ona pia Kanuni za Injili (31110), sura ya 31.

  2. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Maandiko.

    2. Picha 1-5, Familia na Mtoto (62307); picha 1-8, Kupitishwa kwa Sakramenti (62021); picha 1-9, Sala za Asubuhi (62310); picha 1-46, Watoto Wakimpa Mama Maua; picha 1-55, Mahubiri Mlimani (Sanaa ya Picha za Injili 212; 62166); picha 1-56 Watu Watatu Katika Tunuu Yenye Mto Mkali (Sanaa ya Picha za Injili 212; 62093).

  3. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zo zote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Shughuli za Kujifunza

Mwalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Kwa upole waombe watoto wafanye vitendo kadhaa, kama vile kusimama, kugeuka, nyoosha mikono juu, gusa vidole vya miguu, keti chini. Washukuru kwa kufanya vile ulivyowaomba wafanye. Elezea kwamba wamekuwa watiifu. Walitii maelekezo yako.

Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanatutaka tuwatii wazazi wetu

Onyesha picha 1-5, Familia na Mtoto Mchanga.

  • Picha hii inaonyesha nini?

Mwonyeshe mtoto mchanga katika picha na uzungumze kuhusu jinsi kila mmoja wetu alivyokuja duniani kama mtoto mchanga. Wakumbushe watoto kwamba kwa sababu watoto wachanga ni wadogo sana na hawajiwezi wanahitaji mtu mzima na mkubwa wa kuwatunza.

  • Ni nani alikutunza ulipokuwa mtoto mchanga?

  • Ni nani anayekutunza sasa?

Waelezee watoto kwamba watu ambao wanatutunza, kama vile wazazi na wana familia wengine, wanawapenda na wanataka wao wawe salama na wenye furaha.

  • Wazazi wako walikufundisha usifanye nini?

Zungumza kuhusu mambo ambayo watoto wanataka kufanya ambayo yanaweza kuwaumiza au kuwafanya wasiwe na furaha, kama vile kucheza mtaani, kugusa jiko moto, kuchukua kisu chenye makali, kukimbia kwenye mteremko wa kilima kikali, kupigana na kaka na dada zako.

  • Kwa nini wazazi wako hawataki wewe ufanye mambo haya?

Zungumzia kuhusu mambo ambayo watoto wanaweza kufanya kwa usalama na furaha, kama vile kucheza na wanasesere, kutembelea sehemu na familia zao, na kuwa wakarimu kwa kaka na dada zao.

  • Kwa nini wazazi wenu wanawaacha mfanye mambo haya?

  • Kwa nini mnapaswa kuwatii wazazi wenu?

Elezea kwamba wazazi wetu wanatupenda na wataka tufanye mambo ambayo ni salama na ya furaha.

Shughuli

Acha watoto wasimame na kufanya mstari wa kitendo ufuatao:

Miguu yangu inapenda kukimbia (kimbia kwa utulivu mahali pamoja).

Mikono yangu inapenda kucheza (chezesha mikono).

Lakini Mama [au Baba] asemapo, “Njoo” (onyesha kwa mkno),

Mimi hutii upesi.

  • Je, unajisikiaje unapowatii wazazi wako na kuja wanapokuita?

  • Je, Unajisikiaje unapofanya mambo ambayo wazazi wako wanakuambia ufanye?

Elezea kuwa tunapowatii wazazi wetu, tunaweza kujisikia furaha. Wazazi wetu pia wanakuwa na furaha tunapowatii.

Waambie watoto kwamba Baba wa Mbinguni anatutaka tuwatii wazazi. Wasomee na uwaelezee watoto Mafundisho na Maagano 6:1 .

Wimbo

Imbeni au semeni maneno ya “Quickly I’ll Obey” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 197).

Mama anaponiita,

Upesi nitatii.

Nataka kufanya kile kilicho chema.

Siku zote na kila siku.

Baba yangu anaponiita,

Upesi nitatii.

Nataka kufanya kile kilicho chema.

Siku zote na kila siku.

Baba wa Mbinguni ananipenda.

Hunibariki kila siku.

Nataka kufanya kile kilicho chema.

Siku zote na kila siku.

Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanatutaka tutii amri

Onyesha picha 1-55, Mahubiri Mlimani.

  • Ni nani aliye katika picha hii?

Elezea kwamba Yesu alipokuwa duniani, aliwafundisha watu kile ambacho Baba wa Mbinguni alikuwa anataka tufanye. Mafundisho haya huitwa amri. Inua maandiko. Waambie watoto kwamba amri zimeandikwa katika maandiko.

Shughuli

Fungua Biblia na usome Yohana 14:15. Elezea kwamba Yesu alisema maneno haya. Elezea kwamba kushika humaanisha kutii. Acha watoto warudie maandiko pamoja nawe mara kadhaa.

  • Ni zipi baadhi ya amri za Baba wa Mbinguni na Yesu wanazotaka tuzitii?

Ukitumia picha zifuatazo, zungumzia kuhusu baadhi ya amri ambazo watoto wanaweza kutii.

  • Picha 1-5, Familia na Mtoto Mchanga—tuwapende wazazi wetu

  • Picha 1-8, Kupitisha Sakramenti—kuhudhuria mikutano ya Kanisa

  • Picha 1-9, Sala za Asubuhi—omba dua kwa Baba wa Mbinguni.

  • Picha 1-46, Watoto Wakimpa Mama Maua—kuwa mkarimu kwa wengine

  • Baba wa Mbinguni hufanya nini tunapotiii amri Zake?

Baba wa Mbinguni hutubariki tunapokuwa watiifu

Hadithi

Kwa kifupi simulia hadithi ya Shadraki, Meshaki, na Abednego, kama inavyopatikana katika Danieli 3. Onyesha picha 1-56, Watu Watatu katika Tanuri Inayowaka, wakati unaofaa. Elezea kwamba mojawapo ya amri za Baba wa Mbinguni ni kwamba tuombe kwake pekee. Hautakiwi kusali kwa watu wengine, au mfano, ambayo ni kama sanamu. Elezea kwamba Shadraki, Meshaki, na Abedinego walijua amri za Baba wa Mbinguni na walitaka kuzitii. Baba wa Mbinguni aliwalinda hawa wanaume watatu kutokana na moto kwa sababu walimtii. Moto haukuwateketeza.

  • Kwa nini Shadraka, Meshaki, na Abedinego hawakudhuriwa na moto?

  • Je unafikiri Shadraka, Meshaki, na Abedinego walijisikiaje wakati Baba wa Mbinguni aliwalinda kutokana na moto?

Ushuhuda

Elezea hisia zako kuhusu umuhimu wa kuwatii wazazi wetu na Baba wa Mbinguni na Yesu. Waambie watoto ni namna gani kutii amri hutusaidia kuwa na furaha.

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo.

  1. Imbeni au semeni maneno ya “Keep the Commandments” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 146) au “I Have Two Little Hands” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 272).

  2. Acha kila mtoto achukue zamu kuwapa darasa maelekezo fulani, kama vile “simama” na “weka mikono kichwani.” Acha watoto wengine watii maelekezo hayo.

  3. Ukitumia ufito wa kuvulia samaki kutoka somo la 11 na uandae samaki fulani wa karatasi ambao juu yake umeandika maelekezo rahisi, kama vile “kunja mikono yako” “rudia ‘Yesu alisema, Kama unanipenda, zishike amri zangu,’” “tembea kwa utulivu chumbani humu,” “tabasamu kwa watoto wengine,” na “saidia darasa kuimba ‘I Am a Child of God.’” Mpe kila mtoto nafasi ya kushika samaki wa karatasi na atii maelekezo yaliyoandikwa kwenye samaki.

  4. Rejea hadithi ya Nuhu, ukisisitiza kwamba Nuhu na familia yake waliokolewa kutokana na gharika kwa sababu walitii amri.

  5. Mpe kila mtoto kipande cha karatasi kilichochorwa uso wa furaha na kuandikwa na maneno Nina furaha ninapotii. Waache watoto wachore nyuso zao.

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Wasaidie watoto kufanya vitendo vya mchezo ufuatao wa vidole:

    Vidole vidogo vyenye shughuli (kunja ngumi),

    Ni nani atatusaidia kutii?

    “Mimi nita.” “Mimi nita.” “Mimi nita.” “Mimi nita.” “Mimi nita” (nyosha kidole kwa kila “Mimi nita” mpaka vidole vyote vimefunguka),

    Vidole vidogo vyenye shughuli vinasema.

  2. Lete vitu kadhaa ambavyo vinatoa ulinzi, kama vile viatu, kofia, na glavu. Waulize watoto ni ulinzi wa aina gani kila kitu hutoa (kwa mfano, viatu hulinda miguu yetu, kofia hulinda vichwa vyetu kutokana na baridi au macho yetu kutokana na jua). Waambie watoto kwamba tunapowatii wazazi wetu, tutalindwa pia. Zungumza kuhusu baadhi ya sheria na jinsi zinavyoweza kutulinda.

  3. Inua mikono yako na uwaonyeshe watoto jinsi ya kutembeza vidole. Acha watoto wainue mikono yao, watembeze vidole, na wafungue na kufunga mikono yao. Elezea kwamba tunaweza kutembeza mikono yetu na vidole vyetu wenyewe, wala si mtu mwingine. Elezea kwamba tunaweza kufanya mikono yetu itii mtu anapotuomba tufanya kitu fulani. Kufanya hivi hutufurahisha moyoni.

  4. Wasaidie watoto kufanya vitendo vya mstari wa shughuli huku ukisema maneno:

    Mimi Napenda Mikono Yangu

    Mimi napenda mikono yangu; ni yangu (nua mikono na uitazame).

    Inashughulika na husaidia mpaka mwisho wa siku (fanya igizo la mikono ikifanya kazi.

    Inaweza kujikunja kimya kimya (kunja mikono) au piga makofi kwa nguvu (makofi)!

    Inapofanya kile kilicho sahihi, hunifurahisha!

Chapisha