Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 26: Familia Zinaweza Kuwa Pamoja Milele


Somo la 26

Familia Zinaweza Kuwa Pamoja Milele

Madhumuni

Ni kumsaidia kila mtoto kuelewa kwamba mahekalu ni sehemu takatifu, ambapo familia zinaweza kuuganishwa pamoja milele, na kumhimiza kila mtoto kujiaanda kuingia hekaluni.

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze Mafundisho na Maagano 97:15–17 na 124:37–41. Ona pia Kanuni za Injili (31110), sura ya 36, na “Hekalu” katika Kamusi ya Biblia

  2. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Nakala ya Mafundisho na Maagano.

    2. Picha 1-5, Familia na Mtoto (62307); picha 1-7, Familia yenye Upendo; picha 1-54 Hekalu la Salt Lake (Sanaa za picha za injili 502; 62433); picha za mahekalu zinazopatikana (Sanaa za picha za injili 505; 62434–62448, 62566–62569, 62583–62601, 62613–62619); ukurasa wa michoro mwishoni wa somo.

  3. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zo zote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Shughuli za Kujifunza

Mwalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Onyesha picha 1-54, Hekalu la Salt Lake, na picha za mahekalu mengine kadhaa, ikijumuisha hekalu la wilaya yenu ya hekalu, kama lipo. Waruhusu watoto waseme kile wanachojua kuhusu mahekalu.

  • Je, umeshaona hekalu?

  • Je, wewe unafikiria nini unapoona hekalu?

Zungumzia kuhusu umaridadi wa mahekalu, onyeshe minara, madirisha, na milango Elezea kwamba kwenye kuta za nje za kila hekalu kuna maneno The House of the Lord. Waumini wa Kanisa huenda hekaluni kujifunza kuhusu Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo na upendo wao kwetu sisi.

Shughuli

Acha watoto wainue mikono yao juu vichwa vyao kama mnara wa hekalu. Waambie wasimame wima na kujifanya kuwa wao ni hekalu maridadi. Kisha waombe waketi chini kwa utulivu.

Hekalu ni mahali patakatifu

Elezea kwamba hekalu ni mahali patakatifu (ona M&M 97:15–17). Waombe watoto warudie neno takatifu. Hii humaanisha kwamba hekalu ni mahali maalum sana ambapo kila kitu kinatukumbusha Baba wa Mbinguni na Yesu.

Waambie watoto kwamba kama wanashika amri za Baba wa Mbinguni, wanaweza kwenda hekaluni watakapokuwa watu wakubwa. Elezea kwamba katika hekalu tunafanya ahadi maalum na Baba wa Mbinguni na Yesu za kutii amri zake. Pia tunaweza kuoana katika hekalu, na tunaweza kubatizwa kwa niaba ya watu ambao hawakubatizwa walipokuwa hai walipokuwa duniani.

Acha watoto wainue vidole vitatu na urudie vitu vitatu wanavyoweza kufanya katika hekalu watakapokuwa watu wakubwa:

“Katika hekalu tunaweza kufanya ahadi maalum na Baba wa Mbinguni.”

“Katika hekalu tunaweza kuoana.”

“Katika hekalu tunaweza kubatizwa kwa niaba ya wengine.”

Wimbo

Acha watoto wasimame na kuimba au waseme maneno ya “I Love to See the Temple” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 95), wakitumia vitendo vifuatavyo:

Mimi napenda kuona hekalu (unganisha vidole na uinue kidole cha mbele cha kila mkono kutengeneza mnara).

Mimi nitaenda huko siku moja (tembea mahali pamoja);

Kuhisi Roho Mtakatifu (weka mikono pamoja juu ya moyo),

Kusikiliza na kusali (weka mkono nyuma ya sikio, na kisha ikunje mikono).

(© 1980 by Janice Kapp Perry. Imetumika kwa Idhini.)

Elezea kwa sababu hekalu ni mahali patakatifu, sisi huvaa nguo nyeupe tunapokuwa ndani. Nguo hizo hutukumbusha kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu wanatutaka tuwe nadhifu na wasafi na kuchagua kile kilicho sahihi siku zote.

  • Ni rangi gani ya nguo mmevaa leo?

  • Mtavaa nguo rangi gani ndani ya hekalu?

Elezea kwamba kwa sababu hekalu ni mahali patakatifu, tunakuwa na staha tunapokuwa ndani. Tunanong’ona na kuongee kwa sauti ya chini. Acha watoto wanong’one, “Mimi nawapenda Baba wa Mbinguni na Yesu.” Elezea kwamba tunaweza kuhisi furaha na amani katika hekalu kwa sababu tunahisi kuwa karibu Baba wa Mbinguni na Yesu.

Hadithi

Simulia hadithi ifuatayo kuhusu Rais Lorenzo Snow kwa maneno yako mwenyewe:

Lorenzo Snow alijua kwamba karibuni angekuwa nabii wa Kanisa. Alienda hekaluni, na kuvaa nguo zake nyeupe, na akapiga magoti katika chumba maalum ili asali. Alitaka Baba wa Mbinguni amwambie kile ambacho alipaswa kufanya ili kuongoza Kanisa. Aliomba na aliomba, lakini hakupokea jibu. Rais Snow alipokuwa akiondoka kutoka chumbani pale alipokuwa anaomba, Yesu alimtokea. Yesu alikuwa amevaa joho jeupe maridadi na alionekana anang’aa sana na kumetameta kiasi kwamba Rais Snow hakuweza kumtazama kwa urahisi. Yesu alionekana kana kwamba alikuwa amesimama juu dhahabu thabiti. Yesu alimwambia Rais Snow mambo machache ambayo alikuwa amesali ili ajue (ona LeRoi C. Snow, “An Exeperience of My Father’s.” Improvement Era, Sept. 1933, p. 677).

  • Kwa nini unafikiri Rais Snow aliomba katika hekalu badala ya mahali pengine? (Kwa sababu angeweza kuhisi kuwa karibu na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo akiwa hekaluni.)

Mahekalu husaidia familia kuwa pamoja milele

Picha 1-5, Familia na Mtoto Mchanga, na picha 1-7, Familia yenye Upendo. Elezea kwamba mahekalu yanaweza kusaidia familia kuwa pamoja milele. Wakati mwanaume na mwanamke wanapooana katika hekalu na kutii amri, Baba wa Mbinguni huwaahidi wao kwamba wanaweza kuwa pamoja na watoto wao wote milele. Tunaita hii kuunganishwa kama familia?

  • Ni watu gani walio katika familia yako?

  • Unahisi vipi unapokuwa pamoja na familia yako?

  • Ni kwa namna gani familia zinaweza kuwa pamoja milele?

Waambie watoto kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu wanaipenda kila familia na wanataka kila familia kuunganishwa pamoja milele. Elezea kwamba familia ambazo hazijaunganishwa hekaluni zinaweza kujiandaa kwa kutii amri za Baba wa Mbinguni. Kisha zinaweza kwenda hekaluni kuunganishwa kama familia.

Wimbo

Wasaidie watoto kuimba au kusema maneno ya kibwagizo “Families Can Be Together Forever” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 188) mara kadhaa.

“Familia zinaweza kuwa pamoja milele

Kwa Mpango wa Baba wa Mbinguni,

Daima nataka kuwa na familia yangu.

Bwana amenionyesha jinsi ya kufanya hivyo.

Bwana amenionyesha jinsi ninaweza.

Ninaweza kujiandaa kwenda hekaluni

Wakumbushe watoto kwamba kila mtu ambaye hutii amri za Baba wa Mbinguni anaweza kwenda hekaluni. Onyesha ukurasa wa michoro uliyojumuishwa mwisho wa somo na acha watoto wajadili amri zilizoonyeshwa hapo. Elezea kwamba kutii amri hizi kutawasaidia watoto kuwa wenye kustahili kwenda hekaluni wanapokuwa wakubwa.

  • Omba.

  • Tii wazazi.

  • Pendaneni.

  • Nenda kanisani

  • Kulipa zaka.

  • Kula vyakula vizuri (kutii Neno la Hekima).

  • Kuwa mwaaminifu.

Ushuhuda

Toa ushuhuda wako juu ya umuhimu wa kuwa familia milele na kuhusu baraka za hekalu. Wakumbushe watoto kwamba kuwatii wazazi wao na kutii amri za Baba wa Mbinguni ni njia muhimu za kujiandaa kwenda hekaluni.

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo.

  1. Wasaidie watoto kuelewa kwamba milele ni muda mrefu. Unaweza kuwaambia kwamba ni muda mrefu sana kuliko ule wanaongojea siku yao ya kuzaliwa au sikukuu inayofuata; ni muda mrefu mtu mzee wanayemjua amekuwa hai; ni muda mrefu kuliko sasa hadi nyakati Adamu na Hawa walipokuwa hai. Elezea kwamba milele humaanisha kitu kisicho na mwisho.

    Wasaidie watoto kufanya vitendo vya mstari ufuatao unaposema maneno haya:

    Milele ni Muda Gani?

    Milele ni muda gani (onyesha kichwa na kidole, kana vile unafikiria)?

    Ni muda mrefu kushinda mwaka (weka ngumi kidevuni, na uweke kiwiko juu ya ule mkono mwingine).

    Ni muda mrefu kushinda wakati inachukua (weka ile ngumi ingine kidevuni, na uweke kiwiko juu ya ule mkono mwingine).

    Kwa Krismasi kufika.

    Milele ni muda gani (onyesha kichwa na kidole, kana vile unafikiria)?

    Sio muda mrefu kuishi (tikisa kidole)

    Na familia ambayo unaipenda (jikumbatie [mwenyewe).

    Kwani kamwe, haitaisha!

  2. Kwa idhini ya rais wako wa Msingi, waalike wazazi wa mtoto wa darasa lako waje kuelezea hisia zao kuhusu umuhimu wa kuunganishwa pamoja.

  3. Tengeneza nakala ya ukurasa wa michoro uliopo mwisho wa somo kwa kila mtoto. Waache watoto wapake rangi michoro hii.

  4. Kwa idhini ya rais wako wa Msingi, alika familia katika kata yako ambayo hivi karibuni ilienda hekaluni kuunganishwa kusimulia darasa kuhusu tukio hilo.

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Wasaidie watoto kufanya vitendo kwa mstari ufuatao huku ukisema maneno:

    Mimi Ni Msaidizi

    Sasa kwamba mimi ni mkubwa na mrefu (simama kwa vidole na ukinyoosha mikono juu sana).

    Nitakuwa msaidizi mzuri.

    Msaidizi wa baba (inua kidole cha kwanza juu).

    Ambaye ni mkarimu na ni mwema;

    Nitamfanyia mama yangu hivyo (inua kidole cha pili juu).

    Mambo ambayo ninapaswa.

    Msaidizi wa dada (inua kidole cha tatu juu).

    Na kaka pia (inua kidole cha nne juu).

    Msaidizi wa marafiki zangu wote wakweli (inua kidole gumba juu)

    Msaidizi wa Mungu nitajaribu kuwa.

    Kwa kuwapenda wengine jinsi anavyonipenda (kunja mikono).

    Nataka kuwa msaidizi wa wote (nyoosha mikono kabisa),

    Sasa kwamba mimi ni mkubwa na mrefu (simama vidole na ukinyoosha mikono juu sana).

  2. Wasaidie watoto kufanya vitendo vya mstari wa shughuli ufuatao huku ukisema maneno: Rudia mara nyingi kama unavyotaka.

    Fanya duara kila mtu akisimama na ukishikana mikono. Shikaneni mikono wakati wote wa shughuli.

    Sisi wote tuliishi pamoja na Baba wa Mbinguni (kila mtu aje karibu pamoja, na kuleta mikono katikati ya duara).

    Alitutuma hapa duniani ili tuishi (fungueni duara kubwa).

    Alitupatia familia za kutupenda na kufundisha (njooni karibu pamoja tena).

    Familia zetu zitatusaidia kuishi pamoja naye tena (fungueni duara kubwa).

  3. Tengeneza mchoro rahisi wa hekalu kwenye karatasi ili watoto wapake rangi.

Picha
andaa.

Ninaweza Kujiandaa Kwenda Hekaluni

Omba.

Nenda Kanisani.

Kula Vyakula Vizuri.

Pendaneni.

Tii Wazazi.

Lipa Zaka.

Kuwa Mwaaminifu.

Chapisha