Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 9: Ninashukuru kwa ajili ya Maji


Somo la 9

Ninashukuru kwa ajili ya Maji

Madhumuni

Ni kumsaidia kila mtoto kuwa na shukrani kwa Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo kwa ajili ya maji.

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze Mwanzo 1:9–10; Kutoka 17:1-6; na Mathayo 3:13–17.

  2. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Biblia.

    2. Kama inawezekana, tumia picha za aina mbalimbali ya maji, kama maziwa, mito, na bahari.

    3. Picha 1-8, Kupitisha Sakramenti (62021); picha 1-11, Mvulana Akibatizwa (60018); picha 1-18 Yohana Mbatizaji Akimbatiza Yesu (Sanaa za picha za Injili 208; 62133).

  3. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zo zote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Shughuli za Kujifunza

Mwalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Uliza mtoto aje mbele ya darasa. Mnong’onezee sikioni shughuli ambayo inatumia maji, kupiga mswaki, kunawa mikono, au kunyunyiza mimea maji. Acha mtoto aigize shughuli huku watoto wengine wabahatishe ni nini anachofanya. (Unaweza kuhitaji kuwaonyesha watoto jinsi ya kuigiza kila hali.) Acha kila mtoto apate zamu kuigiza shughuli.

Waambie kwamba kila shughuli ambayo imeigizwa inahitaji ya maji. Waambie watoto kwamba tunapaswa kuwa na shukrani kwa Baba wa Mbinguni na Yesu kwa kutupa maji.

Maji ilikuwa sehemu ya Uumbaji

Soma kwa sauti na uelezee Mwanzo 1:9–10.

  • Kwa nini maji ni muhimu sana kwetu?

  • Tunapataje maji yetu?

Wasaidie watoto kuelewa kwamba maji hutoka katika vyanzo vingi, ikijumuisha maziwa, mito, bahari, mvua, na theluji. Elezea kwamba theluji na barafu ni maji yaliyoganda. Onyesha picha za maji ulizopata na uzungumze kuhusu mahali ambapo maji yanatoka katika eneo lako.

Waambie watoto kwamba wewe una shukrani kwamba maji ni sehemu ya mpango wa Baba wa Mbinguni.

Wimbo

Imbeni au semeni maneno “Fun to Do” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, p. 253). Kwa mistari hii, acha watoto waseme njia wanazotumia maji, kama vile kuosha nguo, kuoga, au kupiga mswaki meno yao. Buni vitendo kwa ajili ya wimbo kama inavyopendezwa na maneno.

Kuosha nguo ni furaha,

Yafurahisha kutenda, kutenda, kutenda,

Kuosha nguo ni furaha,

Kutenda, kutenda, kutenda!

(© 1963 by D. C. Heath and Company. Imechapishwa tena kwa Idhini.)

Tunahitaji maji kufanya mambo mengi

  • Kwa nini tunahitaji maji? Maji hutumiwa kwa ajili gani?

Elezea kwamba vitu vingi vyenye uhai, ikijumuisha watu, wanyama, mimea, vinahitaji maji ili kuishi. Kama inawezekana, mpe kila mtoto kikombe kidogo cha maji ya kunywa. Zungumza kuhusu jinsi miili yetu haiwezi kuishi bila maji.

  • Ni kwa namna gani wanyama na mimea hupata maji inayohitaji.

Elezea kwamba sisi pia tunahitaji maji kufanya mambo mengine, kama vile kuoshea na kupikia.

Yesu alimpa Musa na Waisraeli maji huko jangwani

Hadithi

Simulia hadithi ya Musa akipata maji kutoka kwenye mwamba, kama inavyopatikana katika Kutoka 17:1–6. Elezea kwamba watu walikuwa jangwani penye joto na pakavu. Hapakuwa na maji ya kunywa.

  • Ni nini kingetokea kama Waisraeli hawangepata maji?

  • Je, umeshawahi kuwa na kiu sana? Je, unajisikiaje kupata kinywaji cha maji baridi unapokuwa na kiu?

Maji ni muhimu katika Kanisa

Hadithi

Onyesha picha 1-18, Yohana Mbatizaji Akimbatiza Yesu. Simulia hadithi ya ubatizo wa Yesu, kama inavyopatikana katika Mathayo 3:13–17.

  • Yesu Kristo alibatiziwa wapi?

  • Yesu Kristo alibatizwa vipi?

Onyesha picha 1-11, Mvulana Akibatizwa.

  • Tunabatiziwa wapi tunapofika umri wa miaka minane?

  • Je, umeshuhudia mtu akibatizwa?

Waruhusu watoto wazungumze kuhusu kile kilichotendeka wakati walipomwona mtu akibatizwa. Elezea kwamba ni lazima tuwe na maji ili kubatizwa?

Onyesha picha 1-8, Kupitisha Sakramenti

  • Ni kwa namna gani tunatumia maji katika mkutano wa sakramenti?

Elezea shukrani zako kwa ajili ya maji ambayo kwayo tunaweza kubatizwa na kupokea sakramenti.

Ushuhuda

Toa ushuhuda wako juu ya mpango wa Baba wa Mbinguni na upendo wake kwetu katika kutupa maji. Waambie watoto jinsi wewe unamshukuru Baba wa Mbinguni na Yesu kwa ajili ya kipawa hiki cha ajabu.

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo.

  1. Karirini mstari ufuatao pamoja na watoto mara kadhaa, mkifanya vitendo kama inavyoelezwa:

    Matone ya Mvua

    Wakati maua yana kiu.

    Na majani yamekauka (fungua mikono na uinyoshe juu kabisa),

    Matone madogo ya furaha

    Yanatiririka kutoka angani (lete mikono chini, uiviringe).

    Katika vyote hunyunyiza (chezesha vidole upande upande).

    Katika siku zake za furaha,

    Mpaka uangavu wa joto la jua (weka mikono juu ya kichwa na fanya duara).

    Huyafukuzilie mbali (ficha vidole nyuma).

  2. Wasaidie watoto kuimba ua kusema maneno ya “Rain Is Falling All Around” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 241) au “’Give,’ Said Little Children” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk.236).

  3. Acha mtoto achore picha ya maji, kama vile ziwa, mto, au matone. Andika kwenye karatasi ya kila mtoto Ninashukuru kwa ajili ya Maji.

  4. Acha watoto waseme kuhusu au wafanye igizo la njia ambazo wanaweza kucheza na maji, kama vile kuogelea, kuteleza barafuni, kutegengeza mtu wa theluji, au kurukaruka ndani ya vidimbwi.

  5. Wasaidie watoto kuelewa kwamba maji hutusaidia kusafisha vitu. Acha watoto wafanye igizo la shughuli za kusafisha wakitumia maji, kama vile kuosha nguo au kunawa mikono.

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Fanya shughuli zote au baadhi ya zifuatazo ili kuwasaidia watoto kujifunza njia tofauti za kutumia maji:

    1. Mpe kila mtoto kiasi kidogo cha maji ya kunywa. Watoto wanapokunywa maji, elezea kwamba maji ni sehemu ya mpango wa Baba wa Mbinguni kwa ulimwengu. Tunaweza kunywa maji tunapokuwa na kiu.

    2. Weka maji kidogo katika bakuli na umsaidie kila mtoto kunawa mikono yake. Wakumbushe watoto kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu walitupangia sisi tuwe na maji. Elezea kwamba tunaweza kutumia maji kuosha vitu.

    3. Kama inawezakana wapeleke watoto nje na uache kila mmoja wao anyunyize mmea maji. Au lete mmea darasani na umruhusu kila mtoto kunyunyiza maji kidogo kwenye mmea. Elezea kwamba mimea pia inahitaji maji kukua.

  2. Fanya vitendo vifuatavyo huku watoto wakijifanya kuwa mvua inanyesha—pole pole kwanza, na kisha kidogo kidogo ikinyesha sana.

    1. Gusisha ncha za vidole pamoja.

    2. Gusisha mikono pamoja.

    3. Gusisha magoti, yakibadilishana na mikono.

    4. Gonga gonga kwa miguu.

Chapisha