Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 19: Ninashukuru kwa ajili ya Macho Yangu


Somo la 19

Ninashukuru kwa ajili ya Macho Yangu

Madhumuni

Ni kumsaidia kila mtoto kuthamini macho yake na kile yanachoweza kufanya.

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze Yohana 9:1–7 na 3 Nefi 11:1-17.

  2. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Biblia na Kitabu cha Mormoni

    2. Kigurudumu cha uzi chenye tundu kubwa na kamba ya kiatu au kipande cha kamba. (Kama una darasa kubwa, ukipenda unaweza kuwaletea zaidi ya kitu kimoja ya vitu hivi.)

    3. Shali au kitambaa cha kufunga ili mtu asione.

    4. Picha 1-43, Yesu Akimponya Kipofu (Picha za Sanaa za Injili 213; 62145); picha 1-44, Yesu Akifundisha katika Nchi za Magharibi (Picha za Sanaa za Injili 316; 62380);

  3. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zo zote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Taarifa kwa mwalimu: Kuwa mwangalifu kwa hisia za watoto wo wote katika darasa lako ambao wana ulemavu wa kimwili. Zingatia mambo ambayo miili yao inaweza kufanya, wali si ulemavu wao.

Shughuli za Kujifunza

Mwalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Waonyeshe watoto jinsi ilivyo rahisi kutunga gidamu au uzi katika kigurudumu cha uzi huku macho yao yakiwa wazi. Kisha fumba macho yako na jaribu kutunga gidamu katika kigurudumu cha uzi. Mpe kila mtoto nafasi ya kujaribu.

Macho yetu ni baraka kwetu

Elezea kwamba tuna macho ili tuweze kusoma na kujifunza, kufanya kazi na kucheza, na kuona dunia maridadi.

Jadili na watoto jinsi maisha yao yangekuwa tofauti kama hawengeweza kuona.

  • Ungewezaje kula chakula?

  • Ungewezaje kujua ni nguo gani za kuvaa?

  • Ungewezaje kujua njia zako hapo nyumbani?

Wimbo

Wasaidie watoto kuimba au kusema maneno “Two Little Eyes” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 268).

Macho mawili madogo ambayo hupepesa, pepesa, pepesa,

Macho mawili madogo ambayo huona;

Kichwa na mabega, magoti na vidole;

Na vitu vingi zaidi vinifanyavyo mimi.

Tra la la la la la,

Macho mawili madogo ambayo huona,

Macho mawili madogo ambayo hupepesa, pepesa, pepesa,

Na vitu vingi zaidi vinifanyavyo mimi.

(Kutoka Merrily We Sing, © 1948, 1975 na Pioneer Music Press, Inc. [a division of Jackman Music]. Imetumika kwa Idhini.)

Shughuli

Acha watoto waangalie dirishani (au picha maridadi) na wajifanye ndio mara ya kwanza wameweza kuviona. Waalike waelezee kuhusu kile walichokiona. Zungumza kuhusu rangi na maumbo. Wasaidie watoto kutambua ni baraka iliyoje kuweza kuona.

  • Ni nini baadhi ya vitu upendavyo kuviona?

Elezea kwamba baadhi ya watu macho yao hayawezi kuona vizuri. Watu hawa huvaa miwani au lenzi za kubandika ili kuwasaidia waweze kuona. Baadhi ya watu ni vipofu na hawawezi kuona kitu.

Shughuli

Jadili jinsi watu vipofu wanaweza kujifundisha kutembea sehemu mbali mbali wenyewe kwa msaada wa mbwa kiongozi au fimbo. Mfunge kitambaa usoni mmoja wa watoto na ujifanye wewe ni mbwa kiongozi. Nyoosha mkono wako kwa yule mtoto ili akushike kama vile mnyororo wa mbwa. Mwongoze mtoto chumbani. Acha watoto wachukue zamu ya kuwa mtu kipofu au mbwa kiongozi.

Hadithi

Onyesha picha 1-43, Yesu Akimponya Kipofu, na usimulie hadithi ya Yesu akimponya mtu huyo kipofu, kama inavyopatikana katika Yohana 9:1–7.

  • Yesu alifanya nini na udongo? (Ona Yohana 9:6.)

  • Ni nini kilichotokea wakati yule mtu kipofu aliponawa birikani? (Ona Yohana 9:7.)

  • Je, unafikiri yule mtu kipofu alijisikiaje wakati alipoweza kuona?

Ninamshukuru Baba wa mbinguni kwa ajili ya macho yangu

Shughuli

Acha watoto wasimame na kurudia mstari ufuatao pamoja nawe, wakionyesha sehemu za mwili zinapotajwa:

Ninashukuru kwa ajili ya Macho Yangu

Ninashukuru kwa ajili ya macho yangu,

Masikio yangu, mdomo wangu na pua;

Ninashukuru kwa ajili ya viganja vyangu na mikono yangu.

Miguu yangu na vidole vyangu

(Imetoholewa kutoka kwenye mstari wa Beverly Spencer.)

Hadithi

Pitisha picha 1-75, Yesu Akifundisha katika Ulimwengu wa Magharibi, na umuombe kila mtoto asimulie kuhusu kitu kimoja anachokiona katika picha hii. Simulia hadithi ya Yesu matembezini katika Ulimwengu wa Magharibi, kama inavyopatikana katika 3 Nefi 11:1–17.

Elezea kwamba tunaweza tusimwone Yesu kimwili kama watu wa Nefi, lakini tuonapo ulimwengu maridadi, tunaweza kukumbuka upendo Wake kwetu.

Ushuhuda

Waelezee watoto shukrani zako kwa ajili ya macho yako. Simulia jinsi viumbe maridadi ambavyo unaviona kila siku vinakukumbusha upendo wa Yesu na Baba wa Mbinguni kwako. Wakumbushe watoto kumshukuru Baba wa Mbinguni kwa ajili ya macho yao.

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo.

  1. Waalike watoto watazamane kwa makini machoni, kope, mifuniko ya macho, nyusi na kope. Elezea kwamba vifuniko, nyusi na kope zetu husaidia kuzuia uchafu, vumbi na jasho kuingia machoni mwetu.

  2. Kabla ya darasa, tumia chombo chenye ncha kama pini kutoboa mashimo katika kipande cha karatasi cha duara na mraba. Darasani, wafunge watoto kitambaa usoni mmoja kwa wakati na uwaulize wao waguse matundu kwenye karatasi na waseme ni maumbo gani. Elezea kwamba hii ni kama breli, ambayo ndivyo wasomavyo watu vipofu.

  3. Ukitumia mifuko ya karatasi, tengeneza macho ambayo yanafunguka na kufumba kwa kila mtoto (ona kielelezo hapo chini). Andika kila mfuko wa karatasi nashukuru kwa ajili ya macho yangu. Acha watoto wapake rangi macho yao na wachore nywele kwenye mifuko yao ya karatasi. Ukitumia macho ya mfuko wa karatasi, igiza pamoja na watoto nyakati ambapo tunafunga na kufumbua macho yetu, kama vile tunapoamka, au tunapolala, tunapoomba, na tunaposhtuka.

  4. Kama inawezakana wapeleke watoto kwa matembezi ya asili huko nje. Waambie wakunje mikono yao na wawe kimya sana wanapotembea, ili weweze kuzingatia kutumia macho yao. Wanaporudi darasani, waombe wachukue zamu kuelezea kile walichokiona.

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Imbeni au semeni maneno ya “Popcorn Popping” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto uk. 242). Ekezea kwamba kuchanua kwa mwaprikoti huonekana kama bisi.

    • Kama mkitazama nje kupitia dirishani, kama isemwavyo katika wimbo, mtaweza kuona bisi zikitokeza kwenye mwapricoti. Unatakiwa kufanya nini ukitazama nje dirishani?

    Acha watoto watazame nje dirishani, au watembeze nje kwa dakika chache. Rudini darasani na warejee kile walichokiona.

    • Je, mlitumia nini kuona vitu hivi? (Macho.)

    Elezea kwamba tunapswa kumshukuru Baba wa Mbinguni kwa ajili ya macho yetu.

  2. Wasaidie watoto wasimame na kusema maneno yafuatayo, wakitumia vitendo kama inavyooneshwa na maneno:

    Gusa macho yako,

    Gusa pua lako,

    Gusa masikio yako,

    Gusa vidole vyako,

    Nyosha mikono yako,

    Juu juu sana,

    Hata juu sana,

    Kuelekea angani,

    Weka mikono yako,

    Kwenye nywele zako;

    Keti chini kimya kimya,

    Kwenye kiti chako.

  3. Waonyeshe watoto chombo kidogo. Elezea kwamba utakiweka mahali fulani chumbani, na watatumia macho yao kukitafuta. Waombe watoto wafunge macho yao, na uweke chombo hicho mahali kinapoonekana lakini pasipo wazi. Acha watoto wafungue macho yao na watafute chombo hicho bila kutembea au kufanya kelele. Waambie wakunje mikono yao wanapokipata chombo hicho. Wakumbushe watoto kuwa sharti watulie na kuwaacha wale wengine watafute chombo hicho kwa macho yao. Rudia mara nyingi kama inavyohitajika.

Picha
nyuso za mfuko wa karatasi.

Chapisha