Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 32: Ninashukuru kwa Chakula na Mavazi


Somo la 32

Ninashukuru kwa Chakula na Mavazi

Madhumuni

Ni kumsaidia kila mtoto kuona na kuonyesha shukrani kwa ajili ya chakula na mavazi.

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze Mwanzo 1:11–12 na 1 Wafalme 17:8–16.

  2. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Biblia.

    2. Matunda au mboga zikiwa na mbegu ndani yake.

    3. Kijifuko cha maharagwe au kitu kingine laini.

    4. Mkato 1-5, samaki; picha mkato 1-7, nguruwe; mkato 1-8, kondoo; makato 1-22, kuku (picha mikato kama hiyo pia inaweza kupatikana katika Mikato ya Vielelezo vya Picha za Watoto wa Msingi seti 4); au tafuta picha za wanyama watoao chakula na mavazi katika eneo lako.

    5. Picha 1-15, Kubariki Chakula; picha 1-50, Naweza Kujivika.

  3. Fanya maandalizi yaliyo muhimu kwa ajili ya Shughuli yo yote yenye Kuboresha unayotaka kutumia.

Shughuli za Kujifunza

Mwalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Toa maelekezo yafuatayo, mkijaza maeneo yaliyo wazi kwa vyakula vya kawaida vya kifungua kinywa :

Kama unapenda kula. kwa kifungua kinywa, nyoosha mkono.

Kama unapenda kula. kwa kifungua kinywa, nyoosha mkono mwingine.

Kama unapenda kula. kwa kifungua kinywa, simama.

Endelea na matendo mengine mpaka utaje karibu aina moja ya chakula ambacho kila mtoto hupenda. Kisha sema, “Kama unayo shukrani kwa Baba wa Mbinguni kwa ajili ya chakula unachokula, keti chini na ukunje mikono yako.”

Tunatumia mimea na wanyama kwa chakula

  • Ni aina gani nyingine ya vyakula unavyopenda kula?

  • Tunapata wapi chakula chetu?

  • Ni nani aliumba mimea na wanyama ambao kwao tunapata chakula?

Zungumza juu ya baadhi ya vyakula unavyokula na pale vinakotoka. Elezea kwamba sisi tunapata vyakula vingi kutokana na mimea.

Mega au kata tunda au mboga uliyoleta na uonyeshe mbegu.

  • Hizi ni nini?

  • Kwa nini matunda yana mbegu?

Elezea kwamba Baba wa Mbinguni alipanga mimea iwe na mbegu ili mbegu ziweze kuota kuwa mimea mingi ili kutoa chakula kwa ajili yetu (ona Mwanzo 1:11–12). Unapopanda mmea kama vile tunda au mboga hukua, na mbegu zaidi hutokea.

Shughuli

Fanya mstari wa shughuli ufuatao pamoja na watoto:

Mbegu Zimezikwa Kina Kirefu

Mbegu zimezikwa kina kirefu (inama na uguse sakafu kwa mikono).

Zimelala ardhini (weka mkono mmoja juu ya mwngine , viganja pamoja).

Jua la manjano hung’ara sana (weka mikono juu ya kichwa na ufanya duara).

Matone ya mvua ni mepesi sana (chezeshachezesha vidole kwenda chini

Upepo mwanana unapiga (yumbisha mikono juu ya kichwa).

Mbegu ndogo zinaanza kukua (viringa vidole sakafuni kuja juu).

  • Je, umeshawahi kusaidia kupanda mbegu?

  • Ulipanda nini?

  • Ni vyakula gani tunapata kutokana na mimea?

Wasaidie watoto wafikirie juu ya matunda mbali mbali, mboga, na nafaka. Elezea kwamba mkate na chakula cha nafaka hutengenezwa kwa kutumia nafaka. Waambie watoto jinsi ulivyo na shukrani kwa Baba wa Mbinguni kwa ajili ya matunda, mboga, na nafaka.

Onyesha mbegu tena.

  • Je, hizi mbegu zinahitaji nini ili kukua?

Hadithi

Simulia hadithi ya Eliya na mjane wa Sarepta, kama inavyopatikana katika 1 Wafalme 17:8–16. Wasaidie watoto kuelewa kwamba hakukuwa na chakula kingi kwa sababu ya ukosefu wa mvua. Bila mvua iletayo maji, hakuna chakula kitakachokua.

  • Utajisikiaje ikiwa huna chakula cha kula?

  • Je, huyu mjane alibarikiwa vipi kwa kumpa Eliya kile chakula kidogo alichokuwa nacho. (Ona 1 Wafalme 17:15–16.)

Elezea kwamba sio vyakula vyetu vyote hutokana na mimea.

  • Tunapata maziwa kutoka wapi?

  • Tunapata mayai kutoka wapi?

  • Tunapata nyama kutoka wapi?

Zungumzia jinsi baadhi ya vyakula hutokana na wanyama. Ukitumia mikato au picha zifaazo, jadili wanyama ambao wanaotumika kwa chakula katika eneo lako.

Tunatumia mimea na wanyama kwa mavazi

Sema kwamba chakula sio kitu pekee tunachopata kutokana na mimea na wanyama. Onyesha picha 1-50, Naweza Kujivika.

  • Huyu mvulana anafanya nini?

  • Je, wewe unavaa nini wakati unapojivika?

Shughuli

Acha watoto wafanye igizo la kujivika nguo kama vile shati, gauni, viatu, koti na kofia.

  • Kwa nini tunahitaji nguo? (Kufunika miili yetu, kukinga miili yetu, kutupa joto wakati wa baridi.)

  • Nguo zinatengezwa na nini?

Kama watoto wanaweza kutaja baadhi ya vifaa vinavyotumika kutengeneza nguo, uliza kama wanajua hivi vifaa vinatoka wapi. Elezea kwamba tunapata vifaa vya kutengeneza nguo na viatu kutokana na mimea na wanyama. Waambie watoto ni mimea au wanyama gani hutoa vifaa vya kawaida vinavyotumika kwa mavazi katika eneo lako. Kwa mfano, pamba na mkonge hutoka kwenye mimea, na hariri hutoka kwenye nondo wa hariri. Manyoya hutokana na kondoo, na ngozi nyingi hutokana na ng’ombe.

Tunaweza kuwa na shukrani kwa ajili ya chakula na nguo

Shughuli

Waeleze watoto kufikiria juu ya vyakula ambavyo kwa ajili yake wao hushukuru. Rusha au mpe kila mtoto kijifuko cha maharagwe au chombo laini, na wapokezane kwa zamu. Acha kila mtoto ataje chakula ambacho yeye anashukuru kuwa nacho na ndipo akurushie kijifuko hicho cha maharagwe. Jadili chakula hicho kilichotajwa hutokana na nini kabla ya kurusha kijifuko cha maharagwe kwa mtoto anayefuata. Wakumbushe watoto kwamba kila mmea au mnyama aliumbwa na Yesu, chini ya maelekezo ya Baba wa Mbinguni.

Rudia shughuli hii, kwa kumwuliza kila mtoto ataje aina ya vazi badala ya chakula.

Onyesha picha 1-15, Kubariki Chakula.

  • Tunapaswa kumshukuru nani kwa ajili ya chakula chetu.

  • Tunapaswa kumshukuru nani kwa ajili ya mavazi yetu.

  • Tunaweza kumshukuru vipi Baba wa Mbinguni kwa vitu hivi vyote. (Njia moja ni kuvitaja katika sala za kila siku.)

Ushuhuda

Elezea shukrani zako kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu wamefanya iwezekane kwetu sisi kuwa na nguzo za kuvaa na chakula cha kula.

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo hilo.

  1. Mpe kila mtoto kipande cha karatasi kilicho na mstari uliochorwa katikati kutoka juu kwa maneno Ninashukuru kwa ajili ya: ikiandikwa kutoka juu. Acha kila mtoto achore picha ya chakula upande mmoja wa mstari na aina ya vazi upande mwingine.

  2. Wasaidie watoto kuimba au kusema maneno ya mistari miwili ya kwanza ya “Thanks to Our Father” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 20).

  3. Waache watoto wajifanye kuwa wao ni mbegu. Watoto hao wachutame kana vile wao wamepandwa ardhini, kisha wainuke pole pole jinsi jua linavyoangaza na mvua kuwanyeshea pole pole. Ukipenda unaweza kuwaacha watoto wachukue zamu kuwa jua na mvua.

  4. Leta tunda au mboga na wape watoto kiasi kidogo kuonja. Elezea aina ya mbegu na mmea ule unaozaa tunda au mboga. (Zungumza na wazazi wa watoto ili kuhakikisha hakuna mtoto yo yote anayeweza kudhurika na chakula unacholeta.)

  5. Elezea chakula kilicho maarufu kwa watoto bila kukitaja na uwaulize wabahatishe ni chakula gani unachoelezea. Kwa mfano, unaweza kusema, “Hiki chakula ni cheupe au hudhurungi kwa nje. Kina ganda. Kimelazwa kwenye kiota. Ni nini? (Yai.) Rudia mara nyingi kama upendavyo. Unaweza kuleta mfano wa kila chakula ambacho unaelezea.

  6. Leta mavazi kama vile sweta, makoti, na kofia na uache watoto wajaribu wakati unapoongea kuhusu nguo ambazo watoto wanashukuru kuwa nazo.

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Wasaidie watoto kuimba au kusema maneno ya “A Song of Thanks” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 20) au “For Health and Strength” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk.21).

  2. Acha watoto wafanye igizo la kuvaa mavazi unaposema maneno ya mstari wa shughuli ufuatao:

    Watoto, vaeni suruali zenu, vaeni suruali, vaeni suruali.

    Watoto, vaeni suruali zenu, moja, mbili, tatu.

    Watoto, vaeni skati zenu, vaeni skati, vaeni skati.

    Watoto, vaeni skati zenu, moja, mbili, tatu.

    Watoto, vaeni shati zenu, vaeni shati, vaeni shati.

    Watoto, vaeni shati zenu, moja, mbili, tatu.

    Watoto, vaeni soksi zenu, vaeni soksi, vaeni soksi.

    Watoto, vaeni soksi zenu, moja, mbili, tatu.

    Watoto, vaeni viatu vyenu, vaeni viatu, vaeni viatu.

    Watoto vaeni viatu vyenu, moja, mbili, tatu.

    Watoto sasa vaeni nguo, vaeni nguo, vaeni nguo (pigeni makofi).

    Watoto sasa vaeni nguo, acheni tucheze!

Chapisha