Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 36: Naweza Kuwa Mfano Mwema


Somo la 36

Naweza Kuwa Mfano Mwema

Madhumuni

Ni kumsaidia kila mtoto kuweka mfano mwema kwa wengine kwa kufuata mfano wa Yesu

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze Mathayo 4:19; Luka 19:1–10; Yohana 13:15; na 3 Nefi 17:11–24.

  2. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Biblia na Kitabu cha Mormoni.

    2. Nyayo kadhaa zilizokatwa kutoka kwenye karatasi.

    3. Picha 1-3, Yesu Kristo (Picha za Sanaa za Injili 240; 62572); Zakayo juu Mtini; picha 1-64, Yesu Akiomba Pamoja na Wanefi (62542).

  3. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zo zote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Shughuli za Kujifunza

Mwalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Imbeni au mseme maneno ya “Do As I’m Doing” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 276) pamoja na watoto. Acha watoto wafuatie vitendo vyo yvote unavyofanya, kama vile kukunja mikono, kupiga makofi, au kujifanya unapaa kama ndege.

Fanya kama ninavyofanya

Nifuate, Nifuate!

Fanya kama ninavyofanya

Nifuate, Nifuate!

Kama nikipaa juu au chini,

Kama nikienda upesi au pole pole,

Fanya kama ninavyofanya

Nifuate, Nifuate!

Fanya kama ninavyofanya

Nifuate, Nifuate.

(© 1963 by D. C. Heath and Company. Umepigwa chapa tena kwa Idhini.)

Waelezee watoto kwamba walipofanya vitendo vile ulivyofanya, walikuwa wanafuata mfano wako. Tunapofuata mfano wa mtu, tunafanya kile wanachofanya. Waambie watoto kwamba Yesu alisema, “Nifuate” (ona Mathayo 4:19).

Baba wa Mbinguni alimtuma Yesu duniani ili awe mfano kwetu

Onyesha picha 1-3, Yesu Kristo. Elezea kwamba mojawapo ya sababu Yesu alikuja duniani ilikuwa ni kuwa mfano kwetu na kutuonyesha sisi jinsi ya kuishi. Yesu alikuwa mkamilifu. Hii inamaanisha Yeye alifanya kila kitu katika njia sahihi. Jinsi Yeye alivyoishi wakati alipokuwa duniani ndiyo njia tunayopaswa kujaribu kuishi.

Fungua Biblia na uwasomee watoto Yohana 13:15. Waambie watoto kwamba haya ni maneno ya Yesu. Sisitiza kwamba tunataka kuwa kama Yesu na kufuata mfano wake.

Wimbo

Wasaidie watoto kuimba au kusema maneno ya sehemu ya kwanza ya “I’m Trying to Be Like Jesus” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 78).

Mimi ninajaribu kuwa kama Yesu;

Mimi ninafuata njia zake.

Ninajaribu kupenda kama alivyopenda.

Katika yote ninayofanya na kusema.

(© 1980 na Janice Kapp Perry. Umetumika kwa ruhusa.)

  • Ni mambo ya aina gani tunapaswa kuyafanya kama tunajaribu kuwa kama Yesu?

Hadithi

Onyesha picha 1-63, Zakayo Juu Mti na usimulie hadithi ya Yesu na Zakayo, kama inavyopatikana katika Luka 19:1–10. Elezea kwamba Yesu alikuwa mfano mwema kwetu wakati alipokuwa mkarimu kwa Zakayo. Hata ingawa watu wengine hawakumpenda Zakayo, Yesu alitaka kwenda nyumbani kwake na kuwa rafiki yake.

  • Yesu alikuwaje mkarimu kwa Zakayo? (Ona Luka 19:5.)

  • Je, unafikiri Zakayo alijisikia vipi wakati Yesu alipokuwa mkarimu kwake?

Wimbo

Imbeni au mseme maneno ya “Jesus Said Love Everyone” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 61), mkitumia vitendo vinavyoelezwa hapa chini:

Yesu alisema mpende kila mtu (panua mikono wazi kabisa);

Watendee kwa ukarimu, pia (tikisa kichwa chini na juu),

Wakati moyo wako umejawa na upendo (weka mkono juu moyo),

Wengine watakupenda (jikumbatie [mwenyewe).

Hadithi

Onyesha picha 1-64, Yesu Akisali pamoja na Wanefi, na usimulie hadithi ya jinsi Yesu alivyosali pamoja na watoto wa Kinefi, kama inavyopatikana katika 3 Nefi 17:11–24. Elezea kwamba Yesu alionyesha kwa mfano wake kwamba tunapaswa kuwaombea wengine.

  • Yesu aliwaombea kina nani? (Ona 3 Nefi 17:21.)

  • Je, unafikiri watoto walijisikia vipi wakati Yesu alipowaombea?

  • Tunaweza kuwaombea kina nani?

Jadili watu ambao tunaweza kuwaombea, kama vile wana familia, watu walio wagonjwa, wamisionari, na viongozi wetu wa Kanisa.

Shughuli

Onyesha picha 1-63, Zakayo juu Mtini, na picha 1-64, Yesu Akisali Pamoja na Wanefi, upande wa pili wa chumba, na uweke nyayo za karatasi kwenye sakafu zikielekea kwenye kila picha. Acha watoto waimbe au waseme maneno ya sehemu ya kwanza ya “Mimi Najaribu kuwa kama Yesu” tena wanapofuata nyayo kwenda kwenye kila picha.

Simama kwenye kila picha na uwaache watoto wasimulie tena hadithi kadiri wanavyoweza. Wasaidie watoto kufikiria njia ambazo wao wanaweza kuwa mfano mwema kama vile Yesu alivyokuwa katika kila hali. Kwa mfano, wanaweza kushirilki na wengine wanasesere wao au kucheza na mtoto ambaye anahitaji rafiki (Zakayo), na wanaweza kusali kwa ajili ya mtu ambaye ni mgonjwa au anayehitaji msaada maalum (kama kuwaombea watoto wa Kinefi).

Wasaidie watoto kutambua kwamba wanapoonyesha upendo kwa wengine kwa kuwa wakarimu na kwa kuwaombea, wanafuata mfano wa Yesu. Pia wanaweka mfano mwema kwa watu wengine.

Wimbo

Imbeni au semeni maneno ya kibwagizo cha “I’m Trying to Be Like Jesus” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto uk. 78), ukitumia maneno yaliyoelezewa hapo chini:

Pendaneni; kama Yesu anavyowapenda (jikumbatie).

Jaribu kuonyesha ukarimu katika yote unayofanya (kumsalimia mtu mwengine kwa mikono).

Kuwa mpole na mwenye upendo kwa vitendo na kwa fikra (jifanye mkono mmoja ni kichwa cha mnyama na upapase na ule mkono mwingine),

Kwani haya ndiyo mambo Yesu alifundisha (weka mikono pamoja, viganja juu, kana vile kitabu cha maandiko).

(© 1980 na Janice Kapp Perry. Umetumika kwa ruhusa.)

Tunaweza kuwa mifano iliyo miema kwa wengine

Elezea kwamba kama tu vile watoto wanavyofuata mfano wa Yesu, watu wengine wanawatazama na kufuata mifano yao.

Shughuli

Acha mtoto aje mbele ya darasa na awe kiongozi. Acha mtoto awaongoze watoto wengine katika vitendo kama vile kupiga makofi, kuzunguka, au kuruka juu na chini. Rudia shughuli hii ili kuwaruhusu watoto wengine kuwa kiongozi.

Elezea kwamba kuna njia muhimu za kuwa mfano mzuri zaidi ya jinsi tunavyoweza kufanya na miili yetu. Waambie watoto wanaweza kuwa mifano iliyo miema kwa kufanya mambo mazuri, kama vile kusema ukweli, kuwatii mama na baba zao, kutoa wanasesere wao kwa wengine, kuwa na staha kanisani, na kusaidia katika familia zao.

  • Je, unaweza kufanya nini ili kuwa mfano mwema kwa wengine?

Acha kila mtoto afikirie njia anayoweza kuwa mfano mwema na aliambie darasa kile atakachofanya.

Ushuhuda

Simulia juu ya wakati ambao wewe ulifuata mfano mwema wa mtu fulani. Elezea hisia zako kuhusu umuhimu wa kufuata mfano wa Yesu. Wahimize watoto kuweka mifano iliyo miema kwa wengine kwa kufanya mambo ambayo Yesu angefanya.

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo.

  1. Tengeneza taji au kofia ya karatasi kwa kila mtoto. Kwenye kila taji au kofia, andika Naweza kuwa mfano mwema. Jadili njia ambazo watoto wanaweza kuwa mifano miema katikati ya wiki.

  2. Imba “Jesus Once Was a Little Child” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 55, “Jesus Wants Me for a Sunbeam” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 60), au “I Am Like a Star” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk,. 163).

  3. Onyesha tochi au kitu kingine kidogo. Iwashe na ujadili jinsi mwanga kutoka kwenye tochi ambavyo huwasaidia watu inapomulika. Soma kwa sauti fungu la kwanza la maneno katika 3 Nefi 12:16. Waelezee watoto kwamba wao ni kama mianga midogo wanapoweka mfano mwema, kwa sababu watu wengine wanawatazama na kuwafuata. Acha kila mtoto ashike tochi na kuwaongoza wengine chumbani. Rudia hivi mpaka kila mtoto ambaye anataka kuongoza amepata nafasi.

  4. Acha watoto wasimame na kufanya vitendo vya msitari shughuli ufuatao:

    Yesu Anawapenda Watoto Wadogo

    Baadhi ya watoto walikimbia kwenye mtaa wenye vumbi (kimbia katika sehemu hio),

    Wakiharakisha mbio kwa miguu yao midogo (onyesha miguu)

    Katikati ya umati wanapata sehemu (wajifanye wanapitapita katika umati)

    Karibu na Yesu, kuona uso wake (simamia vidole na tazama huko na kule).

    Baadhi ya watu wazima walisema, “Waondoeni” (fanya ishara kwa mkono kama unamaanisa “simameni”).

    “Yeye ana shughuli nyingi hataki watoto leo” (kunja na utikise kichwa).

    Lakini Yesu alisema, “Waacheni waje kwangu” (fanya ishara ya kuiita).

    “Wao ni muhimu na nawapenda” (jikumbatie)

    (Imetoholewa kutoka kwa Margaretta Harmon katika Bible Story Finger Plays and Action Rhymes [Cincinnati, Ohio: Standard Publishing Co., 1964], uk. 27.)

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Waombe watoto warudie neno mfano. Waambie kwamba mfano mwema ni mtu yule unayetaka kufanana naye utakapokuwa mkubwa. Wazazi wetu wanaweza kuwa mifano iliyo miema kwetu. Waombe watoto wataje mambo ambayo wazazi wao wanafanya ili kuwatunza wao au kuwafanya wawe na furaha.

  2. Acha watoto waunganishe mikono yao na wakienda katika duara huku wakiimba au kusema maneno ya “When We’re Helping” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 198). Rudia wimbo mara nyingi utakavyo, ukibadilisha mama na baba, kaka, dada, bibi, au babu.

  3. Cheza “Fuata Kiongozi” pamoja na watoto. Acha watoto wasimame katika mstari. Mtoto wa kwanza katika mstari akimbie, aruke, aruke kamba, au afanye kitendo upande mwingine wa chumba. Watoto wengine wamfuate mtoto wa kwanza, kwa kufanya kile anachofanya. Kisha mtoto wa kwanza aende mwisho wa mstari, na mtoto anayefuata anakuwa kiongozi mpya. Endelea mpaka kila mtoto apate zamu ya kuwa kiongozi.

Chapisha