Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 38 :Naweza kuwa na Staha


Somo la 38

Naweza kuwa na Staha

Madhumuni

Ni kumtia moyo kila mtoto kuonyesha upendo kwa Baba wa Mbinguni na Yesu kwa kuwa na staha.

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze Kutoka 3:1–10.

  2. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Biblia.

    2. Picha 1-19, Kristo na Watoto (Sanaa ya Picha za Injili 216; 62467); Picha 1-66, Musa na Kichaka Kinachoteketea kwa Moto (Sanaa ya Picha za Injili 107; 62239);Picha 1-67, Darasa lenye Staha.

  3. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zo zote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Shughuli za Kujifunza

Mwalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Waombe watoto wakunje mikono yao na wakae kwa utulivu huku wakiimba au kusema maneno ya “Reverently, Quietly” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 26), kwa sauti nyororo. Ikiwa watoto wanajua wimbo huu, wanaweza kuimba pamoja nawe.

Kwa staha, kwa utulivu, kwa upendo tunakufikiria wewe;

Kwa staha, kwa utulivu, kwa ulaini tunaimba tuni yetu,

Kwa staha, kwa utulivu, kwa unyenyekevu sasa tunasali,

Acha Roho wako Mtakatifu akae ndani ya mioyo yetu leo.

Mkimaliza, washukuru watoto kwa kuketi kwa utulivu.

Tunaweza kuwa na staha kanisani.

Onyesha picha 1-67, Darasa Lenye Staha.

  • Watoto hawa wako wapi?

  • Wanafanya nini?

  • Unafikiri wanafikiria kuhusu nini?

  • Utafanya nini unapokuja katika Msingi?

Eleza kuwa tunapokuja kanisani tunapaswa kutenda kwa njia fulani. Hii inaitwa kuwa na staha.

Acha watoto warudie neno staha mara kadhaa.

  • Unafikiri inamaanisha nini kuwa na staha?

Elezea kwamba kuwa na staha ni kufanya mambo ambayo yanaonyesha upendo wetu na heshima yetu kwa Baba wa Mbinguni na Yesu. Tunaweza kuonyesha upendo wetu kwao katika njia zifuatazo (acha watoto waonyeshe baadhi ya njia hizo unapozungumza juu yake):

  • Kutembea kwa utulivu na kuongee kwa sauti ndogo.

  • Kukaa kwa utulivu na kusikiliza sala na masomo.

  • Kunyosha mikono yetu wakati tunapotaka kusema kitu.

  • Kukunja mikono yetu

  • Kuliweka safi jumba letu la mikutano.

Elezea kwamba tunapofanya mambo haya, Baba wa Mbinguni na Yesu wanajua kwamba tunawapenda na kwamba tunafurahia kuwa kanisani.

Wimbo

Pamoja na watoto imbeni au semeni maneno “I Want to Be Reverent” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 28). Rudia kama ukipenda.

Nataka kuwa na staha.

Nionyeshe upendo wangu kwao.

Nitasikiliza kwa utulivu,

Kwani staha inaanza nami.

  • Kwa nini tunapaswa kuwa na staha katika darasa la Msingi?

Wakumbushe watoto kwamba tunapokuwa na staha, tunaweza kuwasikiliza walimu wetu na kujifunza kuhusu Baba wa Mbinguni na Yesu. Tunapokuwa na staha, tunawasaidia wengine kuwa na staha pia.

  • Tuko ndani ya jengo gani sasa?

  • Hii ni nyumba ya nani?

Elezea kwamba jumba la mikutano ni la Baba wa Mbinguni na Yesu. Ni mahali ambapo tunakuja kujifunza kuhusu wao na kile wanachotaka sisi tufanye.

Shughuli

Cheza mchezo wa vidole ufuatao pamoja na watoto: Fanya matendo kwa mikono ili kuonyesha sehemu za jumba la mikutano.

Jumba la Mikutano

Hizi ni kuta za nyumba maridadi sana;

Huu ni mnara mrefu sana.

Haya ni madirisha ambayo huingiza mwanga ndani.

Na milango ifungukayo kwa ajili wote.

Nyumba hii imejengwa na mikono ya upendo.

Kama mahali pa kuimba na kusali.

Acha tukunje mikono yetu, kuinamisha vichwa vyetu (kunja mikono na inamisha vichwa).

Na tutoe shukrani kwa ajili ya nyumba hii leo.

  • Ni baadhi ya vitu gani unapaswa kufanya katika hili jumba la mikutano?

  • Ni baadhi ya mambo gani hatupaswi kufanya katika hili jumba la mikutano?

Wasaidie watoto kuelewa kwamba kuna sehemu na nyakati katika jumba la mikutano kwa ajili ya kukimbia na kucheza michezo, lakini katika sehemu nyingi za jengo na katika siku ya Jumapili tunapaswa kuwa na staha. Taja kwamba licha na kuketi kwa staha katika darasa la Msingi na ndani ya kanisa, tunatembea na kuongea kwa sauti ndogo tuwapo katika kumbi hizo.

Hadithi

Simulia hadithi kuhusu watoto katika darasa lako wakija katika darasa la Msingi. Jumuisha vile wanavyosisimka wakimbiapo na kurukaruka wakielekea katika jengo, jinsi wanavyotembea kwa utulivu wakiingia ndani, na kile wanachofanya wakati wa mkutano wa sakramenti na katika darasa la Msingi na baadaye katika ukumbi. Sisitiza jinsi watoto wanavyokuwa na staha wanapokuja kanisani.

Wimbo

Imba au sema maneno ya “Two Happy Feet” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 270 watoto wakitembea chumbani kwa utulivu na kwa makini ili viatu vyao visipige kelele yoyote.

Mimi nina miguu miwili midogo yenye furaha.

Hunipeleka pale ninapoenda.

Huruka na kuruka kamba pamoja nami.

Na hufanya kelele, najua.

Lakini katika nyumba ya Baba wa Mbinguni.

Pole pole sana hukanyaga.

Kwani, licha ya kuwa natembea, hauwezi kusikia.

Kabisa miguu yangu midogo

  • Je, unafanya nini kwa miguu yako katika kumbi za kanisani? Katika darasa?

  • Je, unafanya nini na mikono yako?

  • Je, unafanya nini na sauti yako?

Tunaweza kuwa na hisia za kuwa na staha

Onyesha picha 1-19, Kristo na Watoto, na uelezee jinsi unavyojisikia unapofikiria kuhusu Yesu Kristo na jinsi Yeye anavyotupenda. Elezea kwamba hizi ni hisia za staha. Waalike watoto waonyeshe hisia zao kuhusu Yesu.

Hadithi

Onyesha picha 1-66, Musa na Kichaka Kinachoteketea kwa Moto, na usimulie hadithi hii kama inavyopatikana katika Kutoka 3:1-10. Sisitizia hisia za staha Musa alizojisikia wakati Bwana aliposema naye katika kichaka kilichokuwa kinateketea kwa moto na kumwita awaongoze wana wa Israeli ili waondoke kutoka Misri. Soma kwa sauti kutoka katika Biblia na uelezee sehemu ya mstari wa 5: “Vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni ardhi takatifu.”

  • Kwa nini Musa alivua viatu vyake?

Elezea kwamba hii ilikuwa ni njia ya kuwa na staha. Hakikisha watoto wanaelewa kwamba hatuhitaji kuvua viatu vyetu ili tuwe na staha. Tuna njia zingine nyingi za kuwa na staha.

  • Je, unawezaje kuwa na staha?

Tunaweza kuwa na staha nyumbani

Waambie watoto kwamba jumba la mikutano si mahali pekee tunapopaswa kuwa na staha.

  • Je, wewe hufanya nini wakati mtu anasali?

  • Je, wewe hufanya nini wakati wa jioni ya familia nyumbani?

Elezea kwamba wakati tunaposikiliza kwa utulivu wakati wa maombi na masomo nyumbani, pia tunakuwa wenye staha. Hii humwonyesha Baba wa Mbinguni na Yesu kwamba tunawapenda.

Ushuhuda

Onyesha upendo wako kwa Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo na shukrani zako kwamba unaweza kuonyesha upendo huu kwa kuwa na staha. Wahimize watoto waonyeshe upendo wao kwa Baba wa Mbinguni na Yesu kwa kuwa na staha katika Msingi, katika mkutano wa sakramenti, na wakati wa sala na jioni ya familia nyumbani.

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie wakati wa somo.

  1. Wapeleke watoto matembezi ya staha katika kumbi za jumba la mikutano. Kama inawezekana, nendeni katika kanisa. Mnaporudi darasani, wapongeze watoto kwa kuwa na tabia ya staha na jadili jinsi staha yao ilivyowasaidia watu wengine katika jengo kuwa na staha katika madarasa yao.

  2. Imba au useme maneno ya “I Will Try to Be Reverent” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 28, “Father, I Will Reverent Be” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 29), au “Our Chapel Is a Sacred Place” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 30).

  3. Chora nyayo za kila mtoto kwenye karatasi ambayo ina mstari “Two Happy Feet” ulioandikwa juu yake (ona uk 126). Acha kila mtoto apake rangi mchoro wa mguu wake na kuuchukua nyumbani.

  4. Acha kila mtoto achukue zamu kuonyesha njia anayoweza kuwa na staha darasani, kama vile kuketi kwa utulivu, kukunja mikono, na kunyosha mkono anapotaka kusema kitu. Zungumzia kuhusu kwa nini tunapaswa kuwa na staha katika nyumba ya Baba wa Mbinguni.

  5. Wasaidie watoto kusema maneno ya mstari mmoja au yote miwili katika mistari ifuatayo. Buni vitendo kama inavyopendezwa na maneno.

    Ifungue, Ifunge [Mikono]

    Ifungue, Ifunge;

    Ifungue, Ifunge;

    Piga makofi kidogo.

    Ifungue, Ifunge;

    Ifungue, Ifunge;

    Iweke kwenye mapaja yako.

    Mimi natikisa mikono yangu.

    Mimi natikisa mikono yangu.

    Mimi nabingirisha mikono yangu.

    Mimi napiga makofi.

    Mimi nainua mikono yangu,

    Kisha naishusha chini.

    Na naikunja mapajani.

    Mimi naituliza miguu yangu.

    Mimi naipumzisha miguu yangu.

    Mimi naketi wima kwenye kiti changu.

    Mimi nainamisha kichwa changu.

    Mimi nafunga macho yangu.

    Mimi ni tayari kusali.

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Imbeni au semeni maneno ya “The Chapel Doors” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto uk. 156). Acha watoto waweke kidole kwenye midomo yao kila mara kifungu cha maneno “Sh, tulia kimya” kinaposemwa.

  2. Acha watoto wafunge macho yao. Waambie wao wanyoshe mikono yao kama wanaweza kukusikia ukiangusha sarafu au kifungo. Angusha sarafu au kifungo sakafuni au mezani. Kisha funga kifungo au sarafu na kitambaa cha mkono au kipande cha nguo. Waombe watoto wafunge macho yao, na wanyoshe mikono yao kama wakisikia sarafu au kifungo wakati huu. Angusha kifungo au sarafu iliyofungwa katika kitambaa sakafuni au mezani. Wasaidie watoto kuelewa kwamba kuna mengi ya kusikia kama watasikiliza kwa makini.

Chapisha