Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 7: Roho Mtakatifu Hunisaidia Mimi


Somo la 7

Roho Mtakatifu Hunisaidia Mimi

Madhumuni

Kumsaidia kila mtoto kujua kuwa Yesu Kristo hutusaidia.

Maandalizi

  1. Jifunze kwa maombi Yohana 14:16–17; 2 Nefi 32:5; Moroni 10:4–5; na Mafundisho na Maagano 39:23; 130:22. Ona pia Kanuni za Injili (31110), sura ya 7.

  2. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Biblia, na nakala ya Mafundisho na Maagano.

    2. Kitu cha kawaida na mfuko wa kukiwekea ndani.

    3. Picha 1-3, Yesu Kristo (Picha za Sanaa za Injili 240; 62572); picha 1-4, Ono la Kwanza (Picha za Sanaa za Injili 403; 62470);

  3. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zozote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Shughuli za Kujifunza

Mwaalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Acha mtoto aje kwako. Mnong’onezee kitu fulani sikio mwake kuhusu Roho Mtakatifu, kama vile “ Roho Mtakatifu humsaidia Baba wa Mbinguni na Yesu.” Rudia kwa kila mtoto katika darasa (unaweza kusema kitu hicho hicho kwa kila mtoto). Waulize watoto kama wanajua yule wewe utazungumza kumhusu leo. Elezea kwamba utazungumza kuhusu Roho Mtakatifu msaidizi wa Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.

Onyesha picha 1-4, Ona la Kwanza. Onyesha Baba wa Mbinguni na Yesu na uelezee kwamba wao wana miili ambayo inafanana na yetu. Elezea kwamba Roho Mtakatifu yu kama Baba wa Mbinguni na Yesu katika njia nyingi. Yeye anatupenda, na hutusaidia, Lakini yeye hana mwili kama wa Baba wa Mbinguni na Yesu. Yeye ni roho kwa hiyo anaweza kuweka mawazo kimya kimya katika akili zetu na kutupa hisia za furaha na faraja.

Roho Mtakatifu hutupa faraja na msaada

  • Unapoumia au kuhuzunika, mama au baba yako hukupa faraja vipi na kukufanya ujisikie vyema?

Onyesha picha 1-3, Yesu Kristo. Waambie watoto kwamba Yesu alijua kwamba wafuasi wake, wasaidizi wake, wangekuwa na huzuni wakati atakufa, kwa hiyo aliwaambia kwamba angemwomba Baba wa Mbinguni awatumie mfariji wa kuwasaidia wasjisikie vibaya (ona Yohana 14:16–17).

Waambie watoto kwamba mfariji huyu ni Roho Mtakatifu, na anaweza kutufariji sisi pia. Elezea kwamba tunapokuwa na huzuni au kukasirika, Baba wa Mbinguni atatusaidia kwa kumtuma Roho Mtakatifu kutufariji.

Hadithi

Elezea kwamba Roho Mtakatifu anaweza pia kutuonya na kutuongoza tunapohitaji msaada. Simulia kwa maneno yako mwenyewe hadithi ifuatayo kuhusu Harold B. Lee, ambaye alikuwa Rais Kanisa wa kumi na moja.

“Labda nilikuwa karibu umri wa miaka minane, au chini ya hapo, wakati nilipelekwa na baba yangu kwenye shamba umbali fulani. Alipokuwa anafanya kazi nilijaribu kujipa shughuli na vitu vingi ambayo mvulana mdogo angejihusisha navyo. Mchana ulikuwa joto na wenye mavumbi na nilicheza mpaka nikachoka. Upande mwingine wa ua kulikuwa na banda lililobomoka ambalo linivutia. Katika akili yangu nilifikiria juu ya ili banda kama kasri ambayo ningependa kuivumbua, kwa hiyo nilienda kwenye ua na nikaanza kupanda ili niende kwenye lile banda. Kukaja sauti kwangu ambayo ilisema kitu cha nguvu sana, ‘Harold, usiende huko.’ Nikatazama huku na kule ili nione aliyekuwa anaita jina langu. Baba alikuwa mbali sana upande mwingine wa shamba. Angeweza kuona kile nilikuwa ninafanya. Hapakuwa na mtu yeyote karibu. Basi nikagundua kwamba mtu nisiyemwona alikuwa ananionya nisiende huko. Kilicho kuwa huko, kamwe sitakijua, lakini nilijifunza mapema kwamba kulikuwa na wale mbali na macho yetu ambao wangeweza kusema nasi” (katika Coference Report, Mexico City Area Conference 1972, uk. 48–49.).

Elezea kwamba wakati mwingine Roho Mtakatifu unong’ona kwa sauti kubwa, kama vile alifanya kwa Rais Lee, lakini mara nyingi hutupa hisia kuhusu kile tunapaswa kufanya au kile hatupaswi kufanya.

Roho Mtakatifu hutusaidia kujua kile kilicho sahihi

Elezea kwamba Roho Mtakatifu anatupenda na hutusaidia kuchagua kile kilicho sahihi. Acha watoto wafikirie vitu fulani ambavyo wamefanya ambavyo ni vyema, kama vile kuwatii wazazi, kuwasaidia wengine, na kusali.

  • Unahisi vipi unapofanya vitu ambavyo ni sahihi?

  • Unahisi vipi unapofanya vitu ambavyo ni makosa?

Elezea kwamba Roho Mtakatifu hutusaidia kujua tofauti kati uzuri na ubaya kwa kutupa hisia nzuri na za ukunjufu tunapofanya kitu sahihi na kuhisi huzuni tonapofanya kosa.

Acha watoto washiriki wakati walihisi hisia nzuri, za ukunjufu kwa sababu walifanya chaguo sahihi au walimsaidia mtu. Wasaidie kutambua ushawishi wa Roho Mtakatifu.

Wimbo

Pamoja na watoto imbeni au mseme maneno “Listen, Listen” (Kitabu cha Nyimbo cha Watoto, p. 107).

Sikiliza sauti ndogo tulivu!

Sikiliza! Sikiliza!

Wakati ambapo inakubidi ufanye maamuzi.

Yeye atatuongoza daima.

Roho Mtakatifu hutusaidia kujua kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo ni halisi

Elezea kwamba Roho Mtakatifu anaweza kutusaidia kutambua wakati jambo ni kweli au halisi. Waonyeshe watoto mfuko ulio na kitu ndani yake. Waambie watoto kwamba kuna kitu fulani ndani ya mfuko, lakini hauwaonyeshi kitu hicho.

  • Kuna kitu chochote katika mfuko huu?

Elezea kwamba ingawa watoto hawawezi kuona kitu ndani ya mfuko, wanajua kiko ndani kwa sababu uliwaambia kuwa kiko ndani hapo. Hata ingawa ni watu wachache ambao washamemwona Baba wa Mbinguni na Yesu, Roho Mtakatifu anaweza kutusaidia kujua kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu ni halisi na kwamba wanatupenda. Elezea kwamba ufahamu huu unaitwa ushuhuda. Wakati fulani watu hutoa ushuhuda wao katika mikutano ya Kanisa na kutuambia kwamba wanajua Yesu yu hai. Roho Mtakatifu amewasaidia kujua ukweli huu.

Tunaweza kupokea karama za Roho Mtakatifu

Zungumzia kuhusu uzoefu wako katika kubatizwa na kuthibitishwa. Zungumzia kuhusu jinsi wanaume wanaoshikilia ukuhani waliweka mikono yao juu ya kichwa chako na kukupa karama ya Roho Mtakatifu.

Wasomee watoto Mafundisho na Maagano 39:23 hadi Roho Mtakatifu. Elezea kwamba wakati watoto wanapofika miaka minane na kubatizwa na kuthibitishwa, wataweza kupokea karama ya Roho Mtakatifu. Karama ya Roho Mtakatifu itawasaidia kuweka ahadi walizofanya wakati walibatizwa.

Ushuhuda

Elezea shukrani zako kwa ajili ya Roho Mtakatifu na waambie watoto jinsi Roho Mtakatifu amekufariji na kukusaidia kujua kile kilicho sahihi.

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo hilo.

  1. Wasaidie watoto kuimba ua kusema maneno ya “The Still Small Voice” (Kitabu cha Nyimbo cha Watoto, uk. 106) au “The Holy Ghost” (Kitabu cha Nyimbo cha Watoto, uk.105).

  2. Onyesha picha za watoto wakifanya vitu vizuri, kama vile kushiriki na kusaidiana. Waulize watoto jinsi wanahisi wakati wamefanya vitu vizuri. Waelezee watoto baadhi ya mazingira ya watu wakifanya vitu vizuri na vitu vibaya, kama vile kuwasaidia mama zao, kupigana na kaka zao, kushiriki wanasesere, na kutowatii wazazi wao. Acha watoto wasimame wakati kitendo ni kizuri na kuketi chini wakati ni kitendo si kizuri

  3. Kwa sauti tulivu sema, “Mtu yeyote anayeweza kusikia sauti yangu, weka kidole chako kwenye pua lako. Mtu yeyote anayaweza kusikia sauti yangu, weka mikono yenu juu ya kichwa chako.” Endelea, ukitaja sehemu zingine za mwili, mpaka watoto wote wanaosikiliza sauti yako tulivu. Elezea kwamba hata ingawa wewe ulikuwa unasema kwa sauti ndogo, wakati watoto walisikiliza, wangeweza kusikia sauti yako na kutii maelekezo yako. Elezea kwamba Roho Mtakatifu wakati mwingine huzungumza nasi kwa sauti ndogo. Kama tutasikiliza kwa makini yeye atatwambia vitu muhimu.

  4. Simulia kwa maneno yako mwenyewe, hadithi ya Rais Wilford Woodruff, Rais wa nne wa Kanisa.

    Usiku mmoja Rais Woodruff, mkewe, na watoto wao wanne walipokuwa safarini, walisimama ili kulala katika nyumba ya rafiiki yao. Watatu kati ya watoto wao walilala katika nyumba hali Rais Woodruff, mkewe, na mtoto mmoja walilala nje katika gari. Rais Woodruff alisema: “Nilikuwa kitandani kwa muda mfupi niliposikia sauti ikiniambia: ‘amka na uondoe gari lako.’ Haikuwa radi, umeme au tetemeko la ardhi, lakini sauti tulivu, ndogo ya Roho wa Mungu—Roho Mtakatifu. … Niliamka na kusongeza gari langu … na kuliegesha kwenye upande wa nyumba. Nilipokuwa nikirudi kitandani Roho ile ile ikaniambia, ‘Nenda ukawaondoe nyumbu wako kutoka kwenye ule wa mti wa mwaloni.’ … Nikawaondoa hadi kwenye kijisitu cha migunga na kuwafunga hapo. Kisha nikaenda kulala. Katika mda wa dakika thelathini kimbunga kiliupiga ule mti ambao nilikuwa nimewafunga nyumbu wangu, kuung’oa kutoka mchangani na kuubeba yadi mia moja, kufagia ua mbili njiani mwake, na kuuangusha … karibu na pale gari langu lilipokuwa limesimama. … Kwa kutii ufunuo wa Roho wa Mungu kwangu niliokoa misha yangu na maisha ya mke wangu na mtoto, pia wanyama wangu” (“Leaves from My Journal,” Millennial Star, 12 Dec. 1881, pp. 790–91).

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Wiki kabla ya somo hili, waombe wazazi wa kila mtoto wamruhusu mtoto alete “kitu cha faraja” darasani. Hii inaweza kuwa blangeti maalum au mwanasesere au wimbo maalum wa kuimba. Lete vitu vichache zaidi ikiwa mmoja atasahau kuleta kitu.

    Darasani zungumza na watoto kuhusu jinsi vitu hivi huwafanya wahisi kuwa salama na kupendwa. Elezea kwamba mmoja wa wasaidizi wa Baba wa Mbinguni na Yesu anaweza kutufanya tuhisi kuwa salama na kupendwa. Mtu huyu wakati mwingine anaitwa Mfariji, kwa sababu Baba wa Mbinguni alimtuma kuwa nasi wakati tunahisi huzuni au hofu. Mtu huyu ni Roho Mtakatifu, rafiki wa ajabu!

  2. Imbeni au mseme maneno ya mstari wa mwisho wa “The Still Small Voice” (Kitabu cha Nyimbo cha Watoto, uk. 106) na uwasaidie watoto kufanya vitendo vinavyoelezewa.

    Sikiliza, sikiliza (kuja kiganja sikioni).

    Roho Mtakatifu atanong’oneza (weka kidole cha shahada kwenye midomo).

    Sikiliza, sikiliza (kuja kiganja sikioni).

    Ile sauti ndogo tulivu (weka mikono pamoja juu ya moyo),

Chapisha