Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 4: Mimi Ninaweza Kuomba kwa Baba wa Mbinguni


Somo la 4

Mimi Ninaweza Kuomba kwa Baba wa Mbinguni

Madhumuni

Ni kumsaidia kila mtoto kujifunza jinsi ya kuomba kwa Baba wa Mbinguni na kujua kwamba Yeye atasikiliza.

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze Danieli 6. Ona pia Kanuni za Injili (31110), sura ya 8.

  2. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Biblia.

    2. Picha 1-9, Maombi ya Asubuhi (62310); picha 1-10, Maombi ya Familia; picha 1-14, Danieli katika Tundu la Simba (Picha za Sanaa za Injili 117; 62096); picha 1-15, Kubariki Chakula.

  3. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zozote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Shughuli za Kujifunza

Mwalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Acha mtoto ambaye alitoa maombi ya kufungua asimame mbele ya darasa. Wakumbushe watoto kwamba somo la mwisho walijifunza kwamba tuliishi na Baba wa Mbinguni kabla ya kuzaliwa. Baba yetu wa Mbinguni ametutuma huku duniani.

  • Tunaweza kuzungumza na Baba wa Mbinguni tukiwa hapa duniani.

  • (Jina la mtoto aliyetoa maombi) alikuwa anazungumza na nani alipokuwa akiomba?

Wasaidie watoto kutambua kwamba wakati tunaomba kwa kweli tunazungumza na Baba wa Mbinguni.

Sisi tunaweza kuomba kwa Baba wa Mbinguni

Toa ushuhuda wako kwamba hata ingawa hatuwezi kumwona yeye, tunaweza kuomba kwa Baba wa mbinguni na Yeye atasikiliza maombi yetu.

Onyesha picha 1-9, Maombi ya Asubuhi.

  • Msichana huyu anafanya nini?

  • Anazungumza na nani?

  • Unafikiri anaweza kuwa anasema nini na Baba wa Mbinguni?

Tumia picha 1-9, Maombi ya Asubuhi; picha 1-10, Maombi ya Familia; picha 1-15, Kubariki Chakula, unapojadiliana na watoto nyakati ambazo tunaomba. Elezea kwamba tunaweza kuomba kwa Baba wa Mbinguni wakati wo wote tunapotaka; nyakati za kawaida sana ni wakati tunapoamka, tunapoenda kulala, wakati wa chakula, pamoja na familia zetu, na wakati tunapokuwa na mahitaji maalum. Acha watoto waonyeshe picha ifaayo unapojadiliana nao.

Yesu Kristo alitufundisha kuomba kwa Baba wa Mbinguni

Elezea kwamba Yesu ametufundisha kufanya mambo fulani wakati tunapoomba. Tunapojiandaa kuomba, tunafikiria juu ya Baba wa Mbinguni.

  • Tunafanya nini na mikono yetu wakati tunaomba?

  • Tunafanya nini na vichwa na macho yetu wakati tunapoomba?

Shughuli

Acha watoto waige vitendo vyako unapoonyesha jinsi tunavyojiandaa kuomba kwa kukunja mikono yetu, kuinamisha vichwa, na kufunga macho yetu. Unaweza kisha kumwomba mtoto asimame mbele ya darasa, na uache watoto wengine wafuatie vitendo vyake anapoonyesha jinsi ya kujiandaa kuomba.

Wimbo

Pamoja na watoto imbeni au semeni maneno “A Prayer Song” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 22) mara kadhaa. Fanya vitendo vinavyopendekezwa na maneno ya wimbo.

Tunainamisha vichwa vyetu wakati wa maombi.

Tunakunja mikono yetu pamoja.

Kisha tunafunga macho yetu, na huku tukiomba.

Sisi tunazungumza na Baba wa Mbinguni.

  • Tunaweza kufanya nini kingine?

Elezea kwamba nyumbani, tunapotoa maombi yetu wenyewe au ya familia, sio tu tunakunja mikono yetu, kuinamisha vichwa vyetu, na kufunga macho yetu, bali kila mara pia tunapiga magoti.

Wimbo

Elezea kwamba kuna mambo maalum tunayosema tunapoomba. Imbeni au semeni maneno ya mstari wa pili wa “I Pray in Faith” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 14) mara kadhaa. Acha watoto wanyoshe kidole kimoja kwa mojawapo ya mambo manne maalum tunayosema wakati tunaomba.

Mimi huanza kwa kusema “Mpendwa Baba wa Mbinguni;

Namshukuru kwa ajili ya baraka anazotoa;

Kisha kwa unyenyekevu naomba vitu ambavyo ninahitaji,

Katika jina la Yesu Kristo, amina.

(© 1987 by Janice Kapp Perry. Imetumika kwa Idhini.)

  • Tunaanzaje maombi yetu ?

  • Tunaweza kumshukuru Baba wa Mbinguni kwa vitu gani?

  • Tunaweza kumwomba nini Baba wa Mbinguni?

  • Tunamaliziaje maombi yetu ?

Baba wa Mbinguni husikiliza wakati tunaomba

Hadithi

Onyesha picha 1-14, Danieli katika Tundu la Simba. Simulia hadithi kutoka katika Danieli 6. Soma kwa sauti sehemu ya kwanza ya mstari wa 22 ili kuelezea kwa nini Danieli hakuumizwa wakati akiwa katika tundu la simba.

Elezea kwamba Danieli alitaka kuomba kwa sababu ilikuwa ni amri kutoka kwa Baba wa Mbinguni na pia kwa sababu alikuwa anataka kumshukuru Baba wa Mbinguni kwa ajili ya baraka zake.

  • Mfalme alifanya nini kwa sababu Danieli aliomba? (Ona Danieli 6:16.)

  • Ni nini kilimtokea Daniel ndani ya pango la simba? (Ona Danieli 6:22.)

  • Unawezaje kujua kwamba Baba wa Mbinguni alisikia maombi ya Danieli? (Ona Danieli 6:23.)

Ushuhuda

Zungumzia juu wakati ambapo Baba wa Mbinguni amesikia maombi yako. Waombe watoto waelezee uzoefu wo wote waliopata kwa sababu ya maombi.

Waambie watoto jinsi ulivyo na shukrani kwamba tunaweza kuomba kwa Baba wa Mbinguni, na uwahakikishie kwamba Baba wa Mbinguni hutusikia tunapoomba.

Unapomuomba mtoto atoe maombi ya kufunga, rejea jinsi tunavyojiandaa kuomba.

  • Tunafanya nini ili kujiandaa kuomba? (Tunakunja mikono yetu, tunaimisha vichwa vyetu na kufumba macho.)

  • Ni kitu gani cha kwanza (jina la mtoto) anapaswa kusema katika maombi?

  • (Jina la mtoto) angeweza kumshukuru Baba wa Mbinguni kwa ajili ya kitu gani?

  • (Jina la mtoto) angeweza kumwomba nini Baba wa Mbinguni ?

  • (Jina la mtoto) anapaswa kumaliza vipi maombi ?

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo.

  1. Rusha kitu laini kama vile kijifuko cha maharagwe au mpira kwa watoto. Baada ya kila mtoto kushika kitu hicho, mwambie akamilishe sentensi hii “Ninapoomba, mimi humshukuru Baba wa Mbinguni kwa ajili ya.” Mtoto aweza kujibu, “Familia yangu.” Baada ya kila mtoto kupata zamu, rudia shughuli hii, watoto wakitaja vitu wanavyoweza kumwomba Baba wa Mbinguni wakati wanapoomba. Unaweza kuonyesha picha ili kuwasaidia wao kufikiri juu ya mawazo.

  2. Imbeni au semeni maneno ya “A Song of Thanks” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 20), mkifanya vitendo vinavyoelezwa hapa chini:

    Tunakushukuru kwa ajili ya duniani nzuri (fanya umbo la duara kuashiria dunia);

    Tunakushukuru kwa ajili ya chakula tunachokula (jifanye unaweka chakula mdomoni);

    Tunakushukuru kwa ajili ya ndege waimbao (lete vidole na dole gumba pamoja mfano wa mdomo wa ndege.

    Tunakushukuru, Mungu, kwa ajili ya kila kitu (nyoosha mikono kabisa)!

    (Kutoka kwa First Year Music na Hollis and Dann. (© 1957 na D. C. Heath and Company. Imechapishwa tena kwa Idhini.)

  3. Karirini mstari “Ninashukuru kwa ajili ya Macho Yangy,” mkiota kila sehemu ya mwili mnapoitaja:

    Ninashukuru kwa ajili ya macho yangu,

    Masikio yangu, mdomo wangu na pua;

    Ninashukuru kwa ajili ya viganja vyangu na mikono yangu.

    Miguu yangu na vidole vyangu

    (Imetoholewa kutoka kwenye mstari wa Beverly Spencer.)

  4. Acha watoto wafanye igizo la hadithi ya Danieli katika pango la simba. Unaweza kuleta mavazi ya kawadia. Kama hautaki kuigiza hadithi yote, acha watoto wajifanye simba wangurumao, na kisha waache wafunge midomo yao kana vile malaika wamefunga vinywa wao.

  5. Imbeni au semeni maneno ya “Thanks to Our Father” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 20) au “We Bow Our Heads” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk.25).

  6. Acha watoto wachore picha za vitu wanavyoweza kumshukuru Baba wa Mbinguni wakati wanapoomba. Andika Ninapoomba, naweza kumshukuru Baba wa Mbinguni kwa ajili ya kile kilicho katika kila picha.

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Wakumbushe watoto kwamba tunapoomba tunazungumza na Baba wa Mbinguni, ambaye anatupenda na hutusikia. Wasaidie watoto kusema mstari ufuatao:

    Nampenda Baba yangu wa Mbinguni.

    Mimi humshukuru ninapoomba.

    Baba yangu wa Mbinguni ananipenda;

    Yeye husikia mambo nisemayo.

  2. Wasaidie watoto kusema mmoja au yote kati ya mistari ifuatayo, wakionyesha vitendo sahihi:

    Mikono yetu tunakunja, vichwa vyetu tunainamisha.

    Macho yetu twayafunga, tu tayari sasa.

    Twakunja mikono yetu na twainamisha vichwa vyetu.

    Na twasikiliza maombi yatolewapo.

  3. Chora mikono ya kila mtoto kwenye kipande cha karatasi kwa kugandamizia mkono. Sema kuhusu kile tunachopaswa kufanya na mikono tunapoomba. Waache watoto wapake rangi michoro ya picha za kugandamiza mikono yao. Andika kila picha jina la mtoto.

Chapisha