Miitaala kwa ajili ya Msingi na Wakati wa Kushiriki
Somo la 14: Adamu na Hawa Waliumbwa katika Mfano wa Baba wa Mbinguni


Somo la 14

Adamu na Hawa Waliumbwa katika Mfano wa Baba wa Mbinguni

Madhumuni

Ni kumsaidia kila mtoto kuelewa kwamba Adamu na Hawa waliumbwa katika mfano wa Baba wa Mbinguni.

Maandalizi

  1. Kwa maombi jifunze Mwanzo 1; 2:15–25; na 3. Ona pia Kanuni za Injili (31110), sura ya 5 na 6.

  2. Vifaa vinavyohitajika:

    1. Biblia.

    2. Mikato 1-1 hadi 1-25 (mikato inayofanana na hiyo pia inaweza kupatikana katika Mikato ya Vielelezo vya Picha vya Msingi seti ya 3, 4, na 5).

    3. Picha 1-33, Adamu na Hawa (Picha za Sanaa za Injili 101; 62461); picha 1-34, Adamu na Hawa Wakifundisha Watoto Wao.

  3. Fanya maandalizi yanayohitajika kwa Shughuli zo zote za Kuboresha unazotaka kutumia.

Shughuli za Kujifunza

Mwalike mtoto atoe maombi ya kufungua.

Shughuli ya Usikivu

Waombe wale wote ambao ni watoto wa Baba wa Mbinguni wasimame. Wakumbushe watoto kwamba sisi wote ni watoto wa Baba wa Mbinguni, kwa hivyo kila mmoja anapaswa kusimama.

Wimbo

Imba “I Am a Child of God” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, uk. 2), pamoja na watoto. Onyesha kwamba wimbo huu unasema Baba wa Mbinguni ametupa makao duniani.

Mimi ni mtoto wa Mungu,

Kanileta hapa,

Kanipa makao duniani

Na wazazi wema

Niongoze, kaa nami,

Unifundishe.

Unionyeshe njia

Ya kujia kwako.

Dunia iliumbwa kulingana na mpango wa Baba wa Mbinguni

Shughuli

Weka maumbo ya mikato ikiangalia chini mezani au kwenye paja.

  • Ni baadhi ya vitu gani ambavyo Yesu aliviumba kwa ajili ya dunia?

Mtoto atajapo kila kiumbe, acha yeye aonyeshe mkato husika.

  • Wewe unashukuru kwa ajili ya viumbe gani?

Wasaidie watoto kuelewa kwamba dunia na kila kitu kilichomo ndani yake kiliumbwa kwa ajili yetu kwa matumizi na kufurahiwa. Wakumbushe watoto kwamba dunia na kila kitu kilichomo ndani yake ni sehemu ya mpango wa Baba wa Mbinguni.

Wimbo

Imba “I Am a Child of God” tena pamoja na watoto.

Adamu na Hawa walikuwa sehemu ya mpango wa Baba wa Mbinguni

Acha watoto watazame maumbo ya mikato uliyoyabandika.

  • Ni kitu gani kingine kinachohitajika kuwa duniani?

Onyesha picha 1-33, Adamu na Hawa. Elezea kwamba baada ya vitu vingine kuumbwa, ndipo Adamu na Hawa waliumbwa. Simulia hadithi ya uumbaji wa watu, kama inavyopatikana katika Kutoka 1:26–28. Elezea kwamba Adamu na Hawa walikuwa watu wawili wa kwanza kuishi duniani. Walikuwa na miili ya nyama na mifupa ambayo ilifanana na mwili wa Baba wa Mbinguni.

  • Ni nani alikuwa mwanaume wa kwanza kuumbwa hapa duniani?

  • Ni nani aliyekuwa mwanamke wa kwanza?

  • Adamu na Hawa walikuwa na miili ya aina gani?

Acha watoto waguse mikono yao, na uwakumbushe kwamba miili yao inafanana na miili ya Adamu na Hawa.

Hadithi

Rejea picha 1-33, Adamu na Hawa, simulia hadithi ya Adamu na Hawa kwa maneno yako mwenyewe, taja mambo yafuatayo wazi (ona Mwanzo 2:15–25; 3):

  1. Baada ya Adamu na Hawa kupokea mwili waliishi mahali maridadi palipoitwa Bustani ya Edeni.

  2. Adamu na Hawa waliozwa kwa milele na Baba wa Mbinguni.

  3. Matunda na maua yalikua kwa urahisi katika Bustani ya Edeni, wanyama wote walikuwa ni wa kufugwa.

  4. Adamu na Hawa hawakujua tofauti kati ya mema na mabaya.

  5. Adamu na Hawa hawangeweza kupata watoto.

  6. Adamu na Hawa wangeweza kula matunda ya miti yote isipokuwa mti mmoja.

  7. Adamu na Hawa walikula tunda la ule mti.

  8. Adamu na Hawa walitakiwa kuondoka kwenye Bustani ya Edeni.

  9. Ulimwengu wote ukabadilika: Adamu na Hawa iliwabidi wafanye kazi ili wapate chakula, magugu yalianza kukua, wanyama wakawa wakali.

  10. Adamu na Hawa kisha wakaanza kupata watoto.

Onyesha picha 1-34, Adamu na Hawa Wakiwafundisha Watoto Wao. Elezea kwamba Adamu na Hawa walibarikiwa kupata watoto wengi. Wao walikuwa wazazi wa kwanza duniani. Waliwafundisha watoto wao kuhusu Baba wa Mbinguni na Yesu. Familia yao ilikua na kutapakaa kote ulimwenguni.

  • Adamu na Hawa walifanya nini baada ya kuondoka kutoka Bustani ya Edeni?

Elezea kwamba Adamu na Hawa na watoto wao walitumia na kufurahia mimea na wanyama ambao walikuwa wameumbwa kwa ajili ya dunia.

Shughuli

Wasaidie watoto kufanya mchezo wa vidole ufuatao:

Adamu na Hawa

Adamu na Hawa waliishi duniani (weka mikono kama bakuli kuashiria dunia).

Ilipokuwa mpya sana.

Waliwatunza wanyama wengi (tumia mkono mmoja kupapasa ule mwingine).

Na chakula pia waliotesha (weka vidole mdomoni, kana vile kula).

Adamu na Hawa walikuwa na watoto (weka vidole viwili karibu pamoja).

Ambao nao walipata watoto wao wenyewe (ongeza vidole viwili zaidi).

Sasa watoto wengi wamezaliwa (chezesha vidole vyote kumi).

Tazama jinsi ulimwengu ulivyokua (tumia mikono kutengeneza duara kubwa, uipanue kwenye kila upande)!

Wasaidie watoto kuelewa kwamba kwa sababu Adamu na Hawa walikuwa wazazi wa kwanza duniani, sisi wote ni sehemu ya familia yao.

Baba wa Mbinguni na Yesu Walisema dunia ilikuwa mzuri

Soma sentensi ya kwanza ya Mwanzo 1:31 kwa sauti. Acha watoto warudie sentensi hii pamoja na wewe. Elezea kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu wanatutaka tuvione viumbe vyote kuwa ni vizuri. Cha muhimu sana, wao wanatuona sisi ni wazuri, na wanampenda sana kila mmoja wetu.

Ushuhuda

Toa ushuhuda wako kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu wanampenda kila mmoja wetu. Eleza kwamba ulimwengu na kila kitu kicho ndani yake kipo kwa ajili yetu kutumia na kufurahia. Wakati tunapoona ua, nyota, na kiumbe kingine, sharti tunakumbushwa kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu wanatupenda. Elezea shukrani zako kwa ajili upendo wao na kwa ajili ya dunia.

Shughuli za Kuboresha

Chagua baadhi ya shughuli hizi ili uzitumie katika somo.

  1. Chagua shughuli kadhaa kutoka somo la 8 hadi 13 kama vile “Uumbaji wa Mungu,” au “Nuhu,” ili uzifanye pamoja na watoto.

  2. Rejea kile kilichotendeka kila siku ya Uumbaji wakati watoto wakihesabu siku kwa vidole vyao.

  3. Imba au sema maneno ya “My Heavenly Father Loves Me” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto , 228) pamoja na watoto.

  4. Acha watoto wachore au wapake rangi picha ya kitu ambacho ni sehemu ya mpango wa Baba wa Mbinguni, kama vile ua, mti, au jua. Andika juu ya karatasi ya kila mtoto Mimi nashukuru kwa ajili ya dunia.

Shughuli za Ziada Kwa Watoto Wadogo

  1. Imbeni au semeni maneno ya “The World Is So Big” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto uk. 235). Wasaidie watoto kufanya vitendo vilivyoandikwa hapo chini:.

    Dunia ni kubwa sana, ee, duara sana (tengenezeni duara kubwa kwa mikono),

    Na ndani yake viumbe vya Mungu hupatikana;

    Milima (weka kwa umbo la mlima juu ya kichwa)

    Mabonde (weka viganja mbele ya mwili)

    Na miti mirefu (nyoosha mikono kwa urefu)

    Wanyama wakubwa (ishara ya ukubwa)

    Na wanyama wadogo (ishara ya udogo)

    Nyota zing’aazo usiku kucha (nyosha na uchezeshe vidole),

    Jua mchana lina joto na linaangaza sana (tengenezeni duara kubwa kwa mikono),

    Dunia ni kubwa sana, ee, duara sana.

    Mungu anatupenda sisi wote; baraka zetu ni nyingi (kunja mikono na ujikumbatie).

  2. Wasaidie watoto kufanya vitendo kwa mstari wa shughuli ufuatao huku ukisema maneno:

    Uumbaji wa Mungu

    Mungu aliumba mwezi (fanya duara kwa mikono).

    Na nyota za kumetameta (fungua na ufunge mikono)

    Na aliziweke hewani (fikia juu)

    Aliumba jua (tengeneza duara kubwa juu ya kichwa)

    Na miti (nyoosha mikono kwa urefu)

    Na maua (weka mikono kama bakuli)

    Na ndege wadogo ambao huruka (punga mikono).

    (Kutoka Fascinating Finger Fun na Eleanor Doan. © 1951. Imetumika kwa Idhini.)

Chapisha