Seminari
Kitengo3: Siku 1, Nefi 7


Kitengo 3: Siku ya 1

1 Nefi 7

Utangulizi

Kujitolea kikamilifu kwa Nefi kwa Bwana inaonyeshwa katika 1 Nefi 7. Pamoja na ndugu zake, alitii amri ya Bwana ya kurudi Yerusalemu na kumleta Ishmaeli na familia yake pamoja nao kwenda nyikani. Kwenye safari ya kurudi nyikani, Lamani, Lemueli, na wengine wa familia ya Ishmaeli waliasi dhidi ya Nefi na walitaka kurudi Yerusalemu. Walipomfunga na kutaka kumuua Nefi, aliomba kwa imani, akakombolewa na Bwana, na kuwasamehe kikamilifu wale waliomtesa. Unapojifunza somo hili, tafakari jinsi unaweza kufanya kitakatifu kwa amri na hali ngumu kama vile Nefi alivyofanya.

1 Nefi 7:1–5

Bwana alimwamuru wana wa Lefi kurudi Yerusalemu kwa Ishmaeli na familia yake.

Fikiria juu ya familia yako, na utafakari kwa nini familia ni muhimu katika mpango wa Mungu.

Soma 1 Nefi 7:1–2, na utambue kile Bwana alimwamuru Lehi ili wanawe wafanye na kwa nini Yeye aliwataka kuitenda. (Itakuwa muhimu kujua kwamba neno mbegu katika 1 Nefi 7:1 inamaanisha watoto na uzao.)

Mojawapo wa kweli tunazojifunza kutokana na vifungu hivi ni kuwa Bwana anatuamuru kuoa na kulea watoto Kwake. Unapoendelea masomo yako ya 1 Nefi 7, jiulize kwa nini ndoa na familia ni muhimu kiasi kwamba Bwana angeamuru Nefi na ndugu zake kuvumilia siku nyingi za safari ngumu kupitia nyikani ili kurudi Yerusalemu.

Soma taarifa ifuatayo kutoka katika “Familia: Tangazo kwa Ulimwengu,” na utambue kile manabii wa siku hizi wametangaza kuhusu umuhimu wa ndoa: “Sisi, Urais wa Kwanza na Baraza la Mitume Kumi na Wawili wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, tunatangaza kwa heshima kwamba ndoa kati ya mwanaume na mwanamke imetakaswa na Mungu, na kwamba familia ni ya muhimu katika mpango wa Muumba kwa maisha ya milele ya watoto Wake. (Ensign auLiahona, Nov. 2010, 129).

Unaweza kuzungushia kishazi “kwa Bwana” katika1 Nefi 7:1. Fikiria juu ya maana ya kishazi katika siku zetu.

Tafuta mawazo ya ziada katika kulea watoto kwa Bwana unaposoma mafundisho yafuatayo kutoka kwa “Familia: Tangazo kwa Ulimwengu”:

“Tunatangaza kwamba amri ya Mungu kwa watoto Wake wa kuzaana na kujaza dunia imebaki ikizingatiwa. …

“… Wazazi wana jukumu takatifu la kulea watoto wao katika upendo na utakatifu, kukimu mahitaji yao ya kimwili na kiroho, na kuwafundisha kupendana na kutumikiana mmoja na mwingine, kutii amri za Mungu, na kuwa wanainchi wenye kutii sheria popote wanapoishi. Wanaume na wanawake—kina mama na kina baba—watawajibika mbele za Mungu kwa kufanya majukumu haya” (Ensign or Liahona, Nov. 2010, 129).

Picha
Familia ya Ishmaeli

Nefi na ndugu zake wanaongea na familia ya Ishmaeli

Soma 1 Nefi 7:3–5 na utambue jinsi Bwana alisaidia wana wa Lehi kutimiza amri Zake. Bwana alisaidia vipi Ishmaeli na familia yake kukubali mwaliko wa kuungana na familia ya Lehi nyikani?

  1. Uliza wazazi wako, kiongozi wa Kanisa, au mwalimu kupendekeza njia tatu ambazo vijana siku hizi wanaweza kujiandaa kwa ndoa na kulea watoto “kwa Bwana.” Nakili ushauri wao katika shajara yako ya kujifunza maandiko.

1 Nefi 7:6–15

Nefi anajaribu kuwashawishi nduguze kuendelea na safari yao nyikani

Soma 1 Nefi 7:6–7, na utambue ni kwa nini Lamani na Lemueli, na baadhi ya familia ya Ishmaeli waliasi wakati wa safari yao nyikani. Fikiria vile itakavyokuwa kuwa kama Nefi katika hali hii. Fikiria kile ungemwambia Lamani na Lemueli na familia ya Ishmaeli ili kujaribu kuwashawishi kuendelea na safari yao kuelekea nchi ya ahadi.

Soma 1 Nefi 7:8–12, na utambue maswali ambazo Nefi aliuliza nduguze ili kujaribu kuwashawishi wasirudi Yerusalemu. Ni kweli gani tatu ambazo Nefi alisema ndugu zake walisahau?

Jibu yafuatayo katika shajara yako ya kujifunza maandiko:

  1. Jinsi gani kukumbuka kweli hizo tatu kungewasaidia Lamani na Lemueli kuwa waaminifu kwa Bwana?

  2. Orodhesha baraka 4–5 ambazo umepokea kutoka kwa Bwana. Jinsi gani kukumbuka kile Bwana amekufanyia kutakusaidia kuwa mwaminifu katika kuchagua kumfuata Yeye?

Soma 1 Nefi 7:13–15, na utambue kile Nefi alisema kitafanyika kwa Lamani, Lemueli, na wana waasi wa familia ya Ishmaeli ikiwa watarudi Yerusalemu.

  1. Andika kifungu katika shajara yako ya kujifunza maandiko kuhusu kwa nini ni muhimu kukumbuka kile Bwana amekutendea na kufuata mwongozo Wake.

1 Nefi 7:16–22

Bwana anamkomboa Nefi

Endelea kufikiria ingekuwa namna gani kuwa katika hali ya Nefi unaposoma 1 Nefi 7:16. Ungefanya nini?

Nefi aliomba. Soma maombi yake katika 1 Nefi 7:17–18, na utambue kile Nefi alichoomba.

Tambua kwamba Nefi aliomba kukombolewa “kulingana na imani [yake].” Mojawapo ya masomo tunayojifunza kutoka kwa mistari hii ni kwamba Mungu hujibu maombi kulingana na imani yetu. Kuomba kwa imani inamaanisha kwamba tuombe kwa imani katika Bwana na kwa hiyari ya kutenda.

Soma taarifa ifuatayo kutoka kwa Mzee David A. Bednar wa Akidi ya Wale Mitume Kumi na Wawili kuhusu maombi ya Nefi katika 1 Nefi 7:17 na uwezo wa Upatanisho wa kubadilisha mioyo yetu. Piga mstari chini ya maneno ambayo yatakusaidia kuelewa umuhimu wa kuwa tayari kutenda tunapoomba kwa imani.

Picha
Mzee David A. Bednar

“Unajua kile ningeweza kuomba ikiwa ningefungwa na ndugu zangu? Maombi yangu yangejumuisha ombi la kitu kibaya kifanyike kwa ndugu zangu na yangekamilika kwa maneno ‘unikomboe kutoka mikononi mwa ndugu zangu’ au, kwa njia nyingine, ‘Tafadhali nikomboe kutokana na tatizo hili, sasa!’ Inapendeza hasa kwangu kwamba Nefi hakuomba kama vile mimi ningeomba, ili hali yake ibadilishwe. Badala yake, aliomba apate nguvu za kubadilisha hali yake. Acha nishauri kwamba aliomba kwa njia hii kwa sababu alijua na kuelewa na kupata uzoefu wa uwezo wa kuwezesha wa Upatanisho wa Mwokozi. …

“Ndugu zangu na dada zangu, matokeo ya tukio hili kwa kila mmoja wetu ni wazi kabisa. Wewe na Mimi tunapokuja kuelewa na kutumia uwezo wa kuwezesha wa Upatanisho katika maisha yetu ya binafsi, tutaomba na kutafuta nguvu ili kubadilisha hali zetu badala ya kuomba kwa mabadiliko ya hali zetu. Tutakuwa wakala wa ‘kutenda’ badala ya vitu ‘vinavyotendewa’(2 Nephi 2:14)” (“‘In the Strength of the Lord’ (Words of Mormon 1:14; Mosiah 9:17; Mosiah 10:10; Alma 20:4),” in Brigham Young University 2001–2002 Speeches [2002], 124).

  1. Jibu moja ya maswali yafuatayo katika shajara yako ya kujifunza maandiko:

    1. Ni wakati katika maisha yako umewahi kuomba kwa imani na kutambua jibu la Bwana kwa maombi yako?

    2. .Unawezaje kufuata mfano wa Nefi wa kuomba na kutafuta uwezo wa kubadilisha hali zako badala ya kuomba kwa mabadiliko ya hali zako?

Baada ya Nefi kukombolewa kutoka kwa kamba zake, ndugu zake walitaka tena kumshambulia. Soma 1 Nefi 7:19–21, na utambue kinachokuvutia kuhusu mtazamo wa Nefi. Fikiria juu ya hali katika familia yako ambayo ilihitaji msamaha. Fikiria kwa nini ni muhimu sana kwamba wanafamilia waweze kusameheana mmoja na mwingine.

  1. Andika yafuatayo mwisho wa kazi ya leo katika shajara yako ya kujifunza maandiko:

    Nimejifunza1 Nefi 7 na kukamilisha somo hili mnamo (tarehe).

    Maswali ya ziada, mawazo, na umaizi ninaotaka kushiriki na mwalimu wangu:

Chapisha