Seminari
Kitengo 22: Siku ya 2, Helamani 3–4


Kitengo cha 22: Siku ya 2

Helamani 3–4

Utangulizi

Katika wakati ulioelezwa katika sura za mwanzo za Helamani, Wanefi walifurahia nyakati za amani na kuvumilia nyakati za ubishi. Malaki ya Wanefi walijiunga na Kanisa wakati wa amani. Kufuatia mafanikio haya makubwa, washiriki wengi zaidi wanyenyekevu wa Kanisa walikua katika imani yao licha ya kuteswa na wale waliokuwa na kiburi. Sababu Wanefi wengi walikuwa waovu, walipoteza ardhi zao zote za kusini kwa Walamani.

Helamani 3

Wanefi wengi wahama upande wa kaskazini, wakati Kanisa likistawi katikati ya uovu na mateso.

SomaHelamani 3:1–2, na utambue kwamba kwa miaka kadhaa “hapakuwa na ubishi” miongoni mwa watu wa Wanefi. Sasa soma Helamani 3:3, 19, na utambue maneno au vishazi vinavyoonyesha kuwa mambo yalikuwa yamebadilika miongoni mwa Wanefi.

Helamani 3:4–16 inaelezea kwamba vile ubishi ulivyokuwa kati ya Wanefi, watu wengi walihamia kaskazini. Wanefi wengi wakawa waovu na kujiunga na Walamani.

Licha ya ubishi na uovu, Helamani alichagua kuishi tofauti. Helamani alikuwa anatumikia kama jaji mkuu wa Wanefi na pia kama nabii kati yao. Soma Helamani 3:20, na ubaini jinsi Helamani alivyoelezwa. (Neno usawa lina maana ya haki au bila unyanyasaji au upendeleo.)

Nini kinachokuvutia kuhusu Helamani? Kwa nini unafikiri alibakia imara katika kipindi hiki cha ubishi na uovu? Unaweza kutaka kuwekea alama neno daima katika Helamani 3:20.

Soma Helamani 3:22–26, na uweke alama jinsi Nephites alianza mabadiliko kwa bora. Watu wangapi walijiunga na Kanisa?

Mormoni mara nyingi alitumia vishazi “hivyo tunaweza kuona,” na “tunaona” ili kuonyesha kweli alizotaka tujifunze. Katika Helamani 3:27–30 vishazi hizi zinatumiwa mara kadha, kuonyesha kuwa Mormoni alitaka tujifunze baadhi ya masomo muhimu. Soma Helamani 3:27–30, na uweke alama misemo muhimu na utambue masomo ambazo Mormoni alitaka tujifunze.

  1. Kukamilisha kazi zifuatazo katika shajara yako ya kujifunza maandiko:

    1. Andika kile Mormoni alitaka ujue kutoka Helamani 3:27–30 kuhusu neno la Mungu.

    2. Andika jinsi masomo yako ya maandiko imekusaidia kuepuka uovu na kukuweka kwenye njia ya kuelekea kwa mbele ya Mungu.

Soma Helamani 3:32–34, na utambue kwamba baadhi ya washiriki wa Kanisa walianza kuwatesa washiriki wengine wa Kanisa. Watesaji walikuwa watu ambao walisema kuwa wao ni wa Kanisa, lakini kwa kweli walikuwa wamejazwa na kiburi na hawakuamini katika mafundisho ya Kanisa. Matendo yao yalisababisha umini wanyenyekevu wa Kanisa kuteseka taabu nyingi. Fikiria jinsi vigumu itakavyokuwa kwenda Kanisani na kuteswa na washiriki wengine wa Kanisa kwa sababu ulichagua kufuata manabii wa Mungu na amri.

Soma Helamani 3:35 ili kujifunza jinsi washiriki waaminifu wa Kanisa walitenda wakati wa muda wao wa mateso na taabu.

  1. Kulingana na masomo yako ya Helamani 3:35, jibu maswali yafuatayo katika shajara yako ya kujifunza maandiko:

    1. Je, imani ya washiriki wanyenyekevu wa Kanisa iliongezeka au kudidimia wakati wa muda wao wa taabu?

    2. Ni nini washiriki wanyenyekevu wa Kanisa walifanya ambayo iliimarisha imani zao?

    3. Ni baraka gani washiriki hawa wa Kanisa walipokea?

Kwa kujifunza Helamani 3:33–35, tunaweza kujifunza kwamba kila mtu huamua jinsi mateso na dhiki itamwathiri. Kamilisha taarifa hii kulingana na kile ulichojifunza kutoka mistari hizi: Licha ya mateso na majaribio, imani yetu katika Yesu Kristo inaweza kuongezeka tunapo . (Kuna njia kadha ya kukamilisha sentensi hii.) Unaweza kutaka kuandika sentensi yako katika maandiko yako karibu naHelamani 3:33–35.

  1. Ili kukusaidia kuelewa vyema mafundisho ya mistari hizi, jibu mbili au yote ya maswali yafuatayo katika shajara yako ya kujifunza maandiko:

    1. Jinsi gani maombi au kufunga imekusaidia katika wakati wa mateso au majaribio?

    2. Unafikiri ina maanisha nini kutoa moyo wako kwa Mungu?

    3. Ni wakati gani imani yako katika Yesu Kristo iliongezeka wakati wa mateso au majaribio?

Soma Helamani 3:36–37, na ubaini hali ya kiroho ya wengi wa Wanefi wakati Helamani alipokufa.

Helamani 4

Roho wa Bwana hujiondoa kutoka kwa Wanefi, na Walamani wanashinda nchi yote ya kusini mwa Nefi.

Kama ilivyoandikwa katika Helamani 4, baada ya Helamani kufariki, kiburi na ubishi miongoni mwa Wanefi ulisababisha Wanefi wengi kujiunga na Walamani. Walamani walipigana vita dhidi ya Wanefi. Soma Helamani 4:4–8, na uweke alama kwenye ramani nchi ambayo unafikiri Walamani walishinda.

Picha
Territory Map
  1. Gawanya kurasa katika shajara yako ya kujifunza maandiko kwa nusu kwa kuchora mstari wima chini katikati ya ukurasa. Juu ya upande mmoja wa ukurasa andika: Vishazi vinavyoonyesha mtazamo wa Wanefi na matendo. Kwenye upande mwingine wa ukurasa andika: Vishazi vinavyoonyesha kile kilichotokea kwa sababu ya matendo haya. Soma Helamani 4:11–13, 21–26, na uandike angalau vishazi vitatu chini ya kila kichwa.

Moja wapo wa kanuni muhimu tuyojifunza kutoka Helamani 4 ni hii: Kiburi na uovu hututenga na Roho wa Bwana na kutuacha kwa nguvu zetu wenyewe. Unaweza kutaka kuandika kanuni hii katika shajara yako ya kujifunza maandiko karibu naHelamani 4:23–25.

Katika uzoefu wa Wanefi, kuachwa kwa nguvu zao wenyewe kawaida ilimaanisha kupoteza vita na nchi zao (ona Helamani 4:25–26). Katika maisha yetu, kuachwa kwa nguvu zetu wenyewe ina maanisha kupoteza urafiki wa Roho.

  1. Fikiri kuhusu aina ya “vita” unayopitia katika maisha yako, na uandike kuhusu moja au zaidi yao katika shajara yako ya kujifunza maandiko. Andika angalau jambo moja unaweza kufanya ili kudumisha urafiki wa Roho katika maisha yako. Pia andika hisia zako juu ya umuhimu wa kuwa na Roho katika maisha yako ili kukusaidia kukabiliana na vita vya maisha yako kwa nguvu ya Bwana.

  2. Andika yafuatayo katika sehemu ya mwisho ya kazi ya leo katika shajara yako ya kujifunza maandiko:

    Nimejifunza Helamani 3–4 na kukamilisha somo hili mnamo (tarehe).

    Maswali ya ziada, mawazo, na umaizi ninaotaka kushiriki na mwalimu wangu:

Chapisha