Seminari
Kitengo cha 13: Siku ya 1, Mosia 18


Kitengo cha 13: Siku ya 1

Mosia 18

Utangulizi

Alma, ambaye alikuwa kuhani wa Mfalme Nuhu, aliamini maneno ya nabii Abinadi na kutubu dhambi zake. Baada ya kifo cha Abinadi, Alma kwa siri aliwafunza wengine kuhusu Yesu Kristo. Wale ambao walimwamini Alma walikuwa na hamu ya kuja katika zizi la Mungu. Waliingia katika agano la ubatizo mahali palipoitwa Maji ya Mormoni. Unapojifunza Mosia 18, tafuta kile Alma alifunza kuhusu ahadi unazofanya wakati unabatizwa na kile Bwana atakufanyia wewe unapoweka ahadi hizo.

Mosia 18:1–16

Alma anawafunza na kuwabatiza watu

Picha
Alma Anabatiza katika Maji ya Mormoni

Fikiria kuhusu ubatizo wako. Unakumbuka utondoti gani kuhusu tukio hili? Ulijitayarisha vipi kwa ubatizo wako? Unakumbuka hisia gani kuhusu ubatizo wako? Tafakari kile unaweza kuthamini hata zaidi kuhusu ubatizo wako sana kuliko ulivyofanya wakati ulibatizwa.

Mosia 18 hutusaidia kuelewa agano tunalofanya na Mungu wakati wa ubatizo. Agano ni “makubaliano kati ya Mungu na binadamu, lakini hawatendi kama walio sawa katika makubaliano haya. Mungu hutoa masharti ya agano, na watu wanakubali kufanya kile yeye anawataka wafanye. Kisha Mungu huahidi watu baraka fulani kwa utiifu wao” (Guide to the Scriptures, “Covenant,” scriptures.lds.org).

Ili kuona jinsi Mosia 18 hutusaidia kuelewa agano la ubatizo, angalia muhtasari ufuatao wa sura hii: Mosia 18:1–7, Kujitayarisha kwa Agano; Mosia 18:8–16, Kufanya Agano; na Mosiah 18:17–30, Kuishi Agano. Unaweza kutaka kuandika kila mada (kwa mfano, Kujitayarisha kwa Agano) karibu na aya sambamba katika maandiko yako.

Soma Mosia 18:1–2, 6–7, na utafute mafundisho na kanuni Alma aliwafundisha watu ili kuwatayarisha kwa ubatizo. Katika nafasi hapo chini, andika jinsi uelewa wa kile Alma aliwafunza watu wake kingesaidia mtu leo kujitayarisha kwa ubatizo.

Mosia 18:8–11 ameandikwa jinsi Alma alivyowasaidia watu wake kuelewa ahadi ambazo wangefanya na kupokea kupitia agano la ubatizo.

  1. Chora mchoro chini katika shajara yako ya maandiko. Pekua Mosia 18:8–11 kwa kile Alma alifunza kuhusu ahadi tunazofanya kwa Mungu (kile sisi “tu radhi” kufanya) na ahadi Mungu hutoa kwetu wakati tunapobatizwa. Andika kile ulichogundua katika safu inayofaa katika mchoro wako.

Mimi naahidi

Mungu Anaahidi

Mojawapo wa kanuni za injili iliyowazi katika Mosia 18:8–11 ni: Tunapokea Roho wa Bwana na ahadi ya uzima wa milele kwa kufanya na kuweka agano la ubatizo.

  1. Hapo chini ya mchoro katika shajara yako ya kujifunza maandiko, andika muhtasari wa kile ulichojifunza kuhusu umuhimu wa kufanya na kuweka agano la ubatizo.

Soma kauli ifuatayo ya Mzee Joseph B. Wirthlin wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili na uweke mstari chini ya baraka ambazo zinaweza kuja kwetu tunapoelewa ahadi tunazofanya na kupokea katika ubatizo: “Mimi nimeona kote katika maisha yangu kwamba watu wanapokuja kuelewa kikamilifu baraka na nguvu za agano lao la ubatizo, ikiwa ni mwongofu mpya au kama muumini wa siku nyingi katika Kanisa, shangwe kuu inayokuja katika maisha yao na wanavyoshughulikia wajibu wao katika ufalme kwa shauku za kuambukiza” (“Alma the Elder: A Role Model for Today,” in Heroes from the Book of Mormon [1995], 84).

  1. Andika katika shajara yako ya kujifunza maandiko kuhusu jinsi agano la ubatizo lako linaweza kuathiri njia unayoishi kila siku. (Kwa mfano, fikiria ahadi yako ya “kusimama kama shahidi wa Mungu wakati wote” vile inahusiana na njia unaingiliana na wengine, ikijumuisha jinsi unavyowatendea wana familia, mambo unayojadili na marafiki na jamaa, lugha unayotumia, aina ya sinema au vipindi vya televisheni unavyotazama, muziki unaosikiliza, uhusiano wa kijamii na miadi, na jinsi gani unajibu wale wanaokosoa imani yako.)

Kwa makini pekua Mosia 18:12–16, na utambue mifano ya jinsi Bwana alitimiza sehemu Yake ya agano na Alma na watu wake baada ya ubatizo wao. Unaweza kutaka kuweka alama kile umepata.

  1. Andika katika shajara yako ya kujifunza kuhusu wakati ulipohisi Bwana amekubariki wewe na Roho Yake kadri ulivyoweka ahadi uliyofanya katika ubatizo kumtumikia Yeye.

Mosia 18:17–30

Alma anaanzisha Kanisa la Yesu Kristo miongoni mwa watu

Ni mara ngapi unafikiria kuhusu maagano uliyofanya wakati wa ubatizo na kuyafanya upya unapopokea sakramenti? Unapaswa kufikiri kuyahusu mara ngapi? Ni wakati gani wewe unachukua muda kufikiria kuhusu maagano hayo?

Picha
Na Rais Henry B. Eyring

Rais Henry B. Eyring wa Urais wa Kwanza alifunza umuhimu wa kushika maagano yetu na Bwana: “Watakatifu wa Siku za Mwisho ni watu wa agano. Kutoka siku ya ubatizo kupitia mambo muhimu ya kiroho ya maisha yetu, tunafanya ahadi na Mungu na Yeye anafanya ahadi za sisi. Yeye daima huweka ahadi Zake zinatolewa kupitia watumishi Wake walioidhinishwa, lakini ni mtihani muhimu kwa maisha yetu ili kuona kama tutafanya na kuweka maagano na Yeye” (”Witnesses for God,” Ensign, Nov. 1996, 30).

Soma Mosia 18:17–18, 20–23, 27–29, ukitafuta jinsi washiriki wa Kanisa katika siku za Alma waliweka maagano yao ya ubatizo. Unaweza kutaka kuweka alama maneno na vishazi mahususi katika Mosia 18:22, 26, 30 ambavyo vinaonyesha kwamba baraka kuu huja kwa wale ambao wanashika maagano yao ya ubatizo.

  1. Jibu maswali yafuatayo katika shajara yako ya kujifunza maandiko: Ni kitu gani kimoja unachoweza kufanya vyema kuweka maagano uliyofanya katika ubatizo? Utaweka vipi sharti hili?

Mosia 18:31–35

Wale ambao ni wa Kanisa wanatoroka kutoka kwa mateso ya Mfalme Nuhu

Jifunze Mosia 18:31–33 ili kujifunza kile Mfalme Nuhu alikuwa anafanya katika mji wa Lehi-Nefi wakati Alma na watu wake walikuwa wanafurahia baraka kuu karibu na Maji ya Mormoni. Soma Mosia 18:34 na kisha Mosia 23:1–2 utafute jinsi Alma alikuwa “ameonywa” juu ya hatari zilizowakabili watu wake.

Fikiria kuandika ukweli huu karibu na Mosia 18:34: Bwana anaweza kuwaonya watu wema wakati wakiwa katika hatari

Soma uzoefu ufuatao ulioshirikiwa na Mzee Neil L. Andersen wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili ambao unaonyesha ukweli huu:

Picha
Mzee Neil L. Andersen

Akifanya kazi kama askari maalum wa FBI, rafiki yangu alichunguza makundi ya jinai yaliyojipanga yakisafirisha madawa haramu kuingia nchini Marekani.

Wakati mmoja, yeye na askari mwingine walienda kwenye nyumba moja ambako waliamini muuza madawa anayejulikana alikuwa anasambaza kokeni. Rafiki yangu anaelezea kile kilitokea:

Tulibisha mlango wa muuza madawa. Mshukiwa alifungua mlango, na alipotuona sisi, alijaribu kuzuia tusione. Lakini alikuwa amechelewa; tungeweza kuona kokeni kwenye meza yake.

Mwanaume na mwanamke ambao walikuwa kwenye meza mara moja walianza kuondoa kokeni. Ilitubidi kuwazuia wasiharibu ushahidi, kwa hivyo kwa upesi nilimsukuma mshukiwa wa madawa ambaye alikuwa anazuia mlango upande mmoja. Nilipomsukuma, macho yangu yalikutana na yake. Cha kushangaza, hakuonekana kukasirika au kuogopa. Alikuwa anatabasamu kwangu.

Macho yake na tabasamu ya kuzima ilinipatia wazo kwamba yeye hangeweza kudhuru, kwa hiyo kwa upesi nilimuacha na nikaanza kwenda mbele kwenye meza. Mshukiwa sasa alikuwa nyuma yangu. Ghafula, nikapata wazo dhahiri, lenye nguvu lilikuja kwenye akili zangu: “Jihadhari na uovu nyuma ya macho ya tabasamu.”

Mara moja nikageuka nyuma kumtazama mshukiwa. Mkono wake ulikuwa ndani ya mfuko wake mkubwa wa mbele. Bila kufikiria nilikamata mkono wake na kuutoa mfukoni mwake. Ndiyo basi niliona, kilichoshikiliwa mkononi mwake, bastola nusu otomatiki tayari kufyatuliwa. Mapambano yalifuata, na nikampokonya silaha mtu huyu.’ …

 Roho Mtakatifu alimwonya rafiki yangu hatari ya kimwili, Roho Mtakatifu pia atakuonya dhidi ya hatari za kiroho” (“Beware of the Evil behind the Smiling Eyes,” Ensign or Liahona, May 2005, 46–47).

  1. Andika katika shajara yako ya kujifunza maandiko kuhusu hisia umeshapata kutoka kwa Roho Mtakatifu au uzoefu unaokumbuka ambapo umewahi kuonywa juu ya au kulindwa kutokana na hatari za kimwili au kiroho, au andika kuhusu uzoefu wa mtu unayemjua au uliyemsoma au kumsikia.

  2. Andika yafuatayo katika sehemu ya mwisho ya kazi za leo katika shajara yako ya kujifunza maandiko:

    Nimejifunza Mosia 18 na kukamilisha somo hili mnamo (tarehe).

    Maswali ya ziada, mawazo, na umaizi ningependa kushiriki na mwalimu wangu:

Chapisha