Seminari
Kitengo cha 6: Siku ya 3, 2 Nefi 9


Kitengo cha 6: Siku ya 3

2 Nefi 9

Utangulizi

Mafunzo yako ya mahubiri ya Yakobo, yaliyoanzia katika 2 Nefi 6–8, yanaendelea katika 2 Nefi 9. Katika 2 Nefi 6–8 ulijifunza mafundisho ya Yakobo kuhusu rehema na nguvu za Mwokozi za kukomboa nyumba ya Israeli kutokana na hali yao ya kupotea na kutawanyika. Katika sura ya 9 utajifunza juu ya ushuhuda wa Yakobo wa nguvu za Upatanisho wa Mwokozi wa kutukomboa sisi kutokana na athari za Anguko, ikijumuisha kifo cha kimwili na kiroho pamoja na matokeo ya dhambi zetu. Rais Joseph Fielding Smith alifundisha kwamba2 Nefi 9 ni “moja ya mahubiri ya kuelimisha zaidi yaliowahi kutolewa kuhusiana na upatanisho.” Inapaswa kusomwa kwa makini na kila mtu anayetafuta wokovu”(Answers to Gospel Questions, comp. Joseph Fielding Smith Jr., 5 vols. [1957–66], 4:57).

2 Nefi 9:1–9

Yakobo anafundisha kwamba Kuanguka kulileta kifo cha kimwili na kiroho kwa wanadamu wote.

Ni nini kinachokuja akilini unapofikiria neno jinamizi?

Neno jinamizi kwa kawaida humaanisha kitu ambacho kinatisha na kinaweza kuleta madhara makubwa sana. Ingawa watu wengi wanafikiria tu juu ya viumbe vya kufikirika wanapofikiria jinamizi, fikiria kama kuna kitu ambacho hasa kinaweza kuleta madhara ya kudumu kwako na, kwa kweli kinatisha. Yakobo alitumia picha ya jinamizi kuashiria hali ya kutisha ambayo sisi sote tunakabiliana nayo katika maisha ya mauti. Soma 2 Nefi 9:10, na utambue sifa mbili za jinamizi ambazo Yakobo alizielezea. Kisha jaza mapengo katika chati hapo chini.

Jinamizi Ovu

D

H

“d ya b

“d ya s

Ni muhimu kuelewa kwamba wakati Yakobo alifundisha kuhusu “kifo cha kiroho” yeye hakumaanisha kwamba roho zetu hasa zitakufa, bali ni kwamba sisi tumetenganishwa kiroho au kukatiliwa mbali kutoka kwenye uwepo wa Mungu (ona 2 Nefi 9:6). Utengano huu mara nyingi hutajwa kama kifo cha kiroho katika maandiko. Unaweza kupenda kuandika kishazi kukatiliwa mbali kutoka uwepo wa Mungu katika pambizo ya maandiko yako karibu na “kifo cha roho” katika 2 Nephi 9:10.

Soma 2 Nefi 9:6, na utambue kwamba Yakobo alianza kwa kuzungumza kuhusu kifo cha mwili na akamalizia kwa kujadili kukatiliwa mbali kutoka uwepo wa Mungu. Pekua mstari huu kwa makini. Ni tukio gani ambalo lilileta vyote kifo cha kimwili na cha kiroho kwa wanadamu?

Soma 2 Nefi 9:7–9, na utambue kile Yakobo alifundisha kingetokea kwa miili na roho zetu kama hakungekuwa na Upatanisho, na kifo cha kimwili na cha kiroho kingebakia milele. Kabla ya kusoma, inaweza kukusaidia kuja maana ya maneno yafuatayo ambayo Yakobo anatumia katika mstari wa 7: Kishazi “hukumu ya kwanza iliyompata mwanadamu”(2 Nefi 9:7) hulenga matokeo ya Kuanguka kwa Adamu na Hawa. Neno uharibifu linalenga miili ya maisha ya muda kwa sababu si kamili na hatimaye itakufa. Neno kutoharibika linalenga mwili iliofufuka, ambao utaishi milele.

  1. Katika shajara yako ya kujifunza maandiko, orodhesha vishazi vichache ulivyotambua katika 2 Nefi 9:7–9 ambavyo vinaelezea kile kingetokea kwa miili yetu na roho zetu kama kungekuwa hakuna Upatanisho.

Picha
Yesu akiomba katika Gethsemane

Soma kauli ifuatayo ya Mzee D. Todd Christofferson wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili ili kufafanua kile hatma yetu ingekuwa bila Upatanisho wa Yesu Kristo: “Kama utengano wetu kutoka kwa Mungu na kifo chetu cha kimwili kingekuwa cha kudumu, wakala wa maadili haungekuwa na maana. Ndiyo, tungekuwa huru kuchagua, lakini ingekuwa na maana gani? Matokeo ya mwisho yangekuwa sawa daima bila kujali matendo yetu: kifo bila matumaini ya ufufuo na hakuna matumaini ya mbinguni. Kama vizuri au vibaya tunavyoweza kuchagua kuwa, sote tungeishia kuwa ‘malaika kwa ibilisi’” (“Moral Agency,” Ensign, June 2009, 50).

  1. Andika sentensi katika shajara yako ya kujifunza maandiko ukielezea kwa maneno yako mwenyewe kile unafikiria Mzee Christofferson alikuwa anasema kuhusu hali ya kuanguka kwetu. Ongeza maelezo mafupi ya kwa nini unafikiria Yakobo angelinganisha kifo cha kimwili na kutenganishwa kutoka kwa Mungu kuwa “mnyama mwovu.”

2 Nefi 9:10–27

Yakobo anafundisha jinsi mateso ya Mwokozi hutukomboa kutoka kwa madhara ya anguko na matokeo ya dhambi.

Mungu hakutuacha sisi tuteseke madhara yote ya “yule mnyama mwovu, kifo na jehanamu.” Soma 2 Nefi 9:10, na uweke alama kile Mungu ametutayarishia sisi.

Soma analogia ifuatayo kutoka kwa Rais Joseph Fielding Smith ambayo inaonyesha haja yetu ya Mwokozi:

“Mtu anaetembea barabarani inatokea anatumbukia katika shimo lenye kina kirefu na giza hata kwamba hawezi kujitoa nje na kupata uhuru wake tena. Je! Anaweza kujiokoa vipi kutoka kwenye janga lake? Sio kwa bidii yoyote yake, kwani hamna njia ya kuokoka kutoka katika shimo hili. Anapiga kelele apate usaidizi na nafsi iliyo karimu, inasikia kilio chake cha msaada, inaharakisha kutoa msaada kwake na kwa kuteremsha ngazi, na kumpatia ambayo kwayo anaweza kutoka tena kufikia nje ardhini.

“Hii kwa kweli ndiyo ilikuwa hali ambayo Adamu alijiweka mwenyewe na uzao wake, wakati alikula tunda lililokatazwa. Wote wakiwa pamoja katika shimo, hakuna angeweza kutoka nje na kuwaokoa wengine. Shimo liliondolewa kutoka uwepo wa Bwana na kifo cha muda, kuharibika kwa mwili. Na wote wakiwa chini ya mauti, hakuna ambaye angeweza kutoa njia ya kutoroka.

“Kwa hivyo, katika rehema yake isiyo na mwisho, Baba alisikia kilio cha watoto wake na akamtuma Mwanawe wa Pekee, ambaye hakuwa chini ya mauti wala dhambi, ili atoe njia ya kuepuka. Hii alifanya kupitia upatanisho wake usio na mwisho na injili ya milele” (Doctrines of Salvation, ed. Bruce R. McConkie, 3 vols. [1954–56], 1:126–27).

Sehemu kubwa ya ujumbe wa Yakobo katika sura ya 9 inalenga juu ya njia ambayo Bwana alitutayarishia ya kutoroka kutoka kwa fumbato la kifo cha kimwili na kifo cha kiroho, na inatuhakikishia sisi kwamba tunaweza kukombolewa.

  1. Pekua 2 Nefi 9:5, 19–21, na ujibu maswali yafuatayo katika shajara yako ya kujifunza maandiko:

    1. Kulingana na 2 Nefi 9:5, 21, Mwokozi alipitia nini ili kwamba sisi tuweze kukombolewa kutoka kwa kifo na jehanamu?

    2. Mwokozi aliteseka kwa ajili ya nani, kulingana na 2 Nefi 9:21?

Fikiria kuhusu ni watu wangapi “wa jamii ya Adamu” (2 Nefi 9:21). Hii inajumuisha wale wote ambao waliishi, wanaoishi sasa, na wale bado wataishi katika ulimwengu huu—ikijumuisha wewe. Unaweza kutaka kuandika jina lako karibu na 2 Nefi 9:21 ili kukumbuka dhabihu ya Mwokozi iliyotolewa kwa ajili yako.

Picha
Usulubisho

Yakobo alifunza kwamba kuteseka kwa Mwokozi kungetusaidia kutoroka kutoka kwa jinamizi—kifo cha kimwili na kukatiliwa mbali kutoka kwenye uwepo wa Mungu milele. Soma 2 Nefi 9:22, na utambue kishazi ambacho kinasema tutaweza kushinda kifo cha kimwili na kishazi ambacho kinaonyesha tutakuwa katika uwepo wa Mungu tena. Andika kile unatambua katika sentensi hapo chini:

Kwa sababu ya Kuanguka, miili yetu itakufa, lakini kwa sababu ya kuteseka kwa Kristo, miili yetu itakuwa .

Kwa sababu ya Kuanguka, sisi tutakatiliwa mbali kutoka uwepo wa Mungu, lakini kwa sababu ya kuteseka kwa Kristo, wote watasimama tena .

Kutoka kwa mafundisho ya Yakobo tunajifunza fundisho: Upatanisho wa Yesu Kristo hukomboa wanadamu wote kutokana na kifo cha kimwili na kifo cha kiroho kilicholetwa na Kuanguka.

Kama ziada kwa ujumbe huu wa matumaini, Yakobo alifundisha kwamba kuteseka kwa Mwokozi kunaweza pia kutukomboa kutoka kwenye kifo cha kiroho kilichosababishwa na dhambi zetu wenyewe. Soma 2 Nefi 9:27, na utambue jinsi Yakobo alivyoelezea hali ya wale ambao watavunja amri au kufanya dhambi. Soma 2 Nefi 9:15–16, na uweke alama maumivu au mateso ya kiroho ambayo dhambi zetu zitaleta juu yetu kama sisi hatutatubu.

Kwa kuongezea mateso haya, tazama kishazi “watatupwa kwenye” katika 2 Nefi 9:16. Kwa sababu ya Upatanisho, wanadamu wote watarudi kwenye uwepo wa Mungu kuhukumiwa. Hata hivyo, kama hatujatubu dhambi zetu, tutatenganishwa tena na uwepo wa Mungu. Ilhali ukombozi kutoka kwa Kuanguka ni kipawa cha wanadamu wote, ukombozi wetu kutoka kwa matokeo ya dhambi zetu binafsi hutegemea hamu na matendo yetu. Soma 2 Nefi 9:21, 23–24. Kwa sababu ya Upatanisho, tunaweza kufanya nini ili tuokolewe kutokana na matokeo ya milele ya dhambi zetu?

Baada ya kusoma maneno ya Yakobo, kamilisha kanuni ifuatayo: Kupitia Upatanisho wa Yesu Kristo, tunaweza kushinda matokeo ya dhambi zetu ikiwa sisi.

Tutachukua muda na kutafakari juu ya kile unachoweza kufanya ili kuhisi zaidi nguvu za kusafisha za Upatanisho wa Mwokozi. Je! Kuna mambo Bwana angependa wewe utubu? Tafakari jinsi unaweza kutubu mambo haya. Je! Unaweza kusikia vyema sauti Yake vipi?

  1. Andika aya fupi katika shajara yako ya kujifunza maandiko ukionyesha jinsi unavyohisi kuhusu dhabihu ya upatanisho wa Mwokozi kwa ajili yako.

  2. Andika yafuatayo chini ya kazi za leo katika shajara yako ya kujifunza maandiko:

    Nimejifunza 2 Nefi 9na kukamilisha somo hili mnamo (tarehe).

    Maswali ya ziada, mawazo, na umaizi ningependa kushiriki na mwalimu wangu:

Chapisha