Seminari
Kitengo cha 9: Siku 1, 2 Nefi 32


Kitengo 9: Siku ya 1

2 Nefi 32

Utangulizi

Baada ya kufundisha juu ya “njia nyembamba na iliyosonga”inayoelekea kwenye uzima wa milele” (2 Nefi 31:18), Nefi aliona kwamba watu wake walihangaika juu ya kile wangefanya baada ya kuanza kwenye njia hiyo. Yeye akajibu maswali yao kwa kuwahimiza “kushiriki maneno ya Kristo” na “kusali kila wakati” (2 Nefi 32:3, 9). Aliwahakikishia kwamba kama wangefanya mambo haya, Roho Mtakatifu angewasaidia kujua cha kufanya.

2 Nefi 32:1–7

Nefi anatushauri tutafute mwelekeo mtakatifu kupitia maneno ya Yesu Kristo

Fikiria wakati mtu alipokupatia maelekezo ya kutoka sehemu moja hadi nyingine. Je! Ilikuwa rahisi au vigumu kuelewa maelekezo hayo? Kwa nini ni muhimu kuwa mtu kutoa maelekezo wazi?

Katika somo lililopita ulijifunza maelekezo fulani Nefi alitoa kwa watu wake. Baada ya kushiriki maalekezo hayo, alisema, “Hii ndiyo njia” (2 Nefi 31:21). Pekua kwa upesi 2 Nefi 31:17–18, na rejelea jinsi mtu huanza katika njia ya uzima wa milele. Kisha soma 2 Nefi 32:1, na utafute swali ambalo lilikuwa katika mioyo ya watu kuhusu kile Nefi alikuwa amewafunza wao. Elezea maswali ya watu kwa maneno yako mwenyewe:

Soma 2 Nefi 32:2–3, na utafute kile Nefi alisema tunahitaji kufanya baada ya kuingia katika njia hiyo. Inaweza kusaidia kujua kwamba kuongea na ndimi za malaika, kulingana na Rais Boyd K. Packer, Rais wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili, “kwa urahisi humaanisha kwamba wewe unaweza kuongea kwa uwezo wa Roho Mtakatifu” (“The Gift of the Holy Ghost: What Every Member Should Know,” Ensign, Aug. 2006, 50).

Unaweza kutaka kuweka alama kishazi “shiriki maneno ya Kristo” katika 2 Nefi 32:3 (aya hii ni kifungu cha umahiri wa maandiko). Nefi alitumia kishazi “maneno ya Kristo” ili kuelezea mafundisho yenye maongozi ya Roho Mtakatifu. Orodhesha baadhi ya njia au sehemu unaweza kusoma, kusikia, au kupokea mafundisho yenye maongozi ya Roho Mtakatifu.

Maneno ya Kristo yanajumuisha maandiko na maneno ya manabii wa kisasa. Ili kukusaidia kutafakari maana ya “shiriki maneno ya Kristo,” soma dondoo zifuatazo:

Picha
Mzee Russell M. Nelson

Mzee Russell M. Nelson wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili alifundisha: “Kushiriki inamaanisha zaidi ya kuonja. Kushiriki inamaanisha kufaidi Tunafaidi maandiko kwa kujifunza katika moyo wa ugunduzi mwema na utii aminifu. Tunaposhiriki maneno ya Kristo, yana … kuwa sehemu muhimu ya asili yetu” (“Living by Scriptural Guidance,” Ensign, Nov. 2000, 17).

Mzee Robert D. Hales, pia wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili, alisema, “Kama mimi na wewe tungeshiriki maneno ya Kristo, ni lazima tusome maandiko na kuelewa maneno yake kwa njia ya kuyatafakari na kuyafanya sehemu ya kila fikira na vitendo”(“Healing Soul and Body,” Ensign, Nov. 1998, 15).

  1. Katika shajara yako ya kujifunza maandiko, andika kwa maneno yako mwenyewe kile unafikiria inamaanisha kushiriki maneno ya Kristo.

Tafakari tofauti kati ya maneno mlo, asusa, na kuona njaa. Fikiria kwa dakika kuhusu jinsi baadhi ya njia zisizo na ufanisi za kujifunza maneno ya Kristo zinaweza kufananishwa na kula asusa au hata kuona njaa.

Jaza katika salio la kanuni ifuatayo kulingana na 2 Nefi 32:3: Wakati tunashiriki maneno ya Kristo, maneno ya Kristo yata.

  1. Katika shajara yako ya kujifunza maandiko, aidha uandike kuhusu wakati uliposhiriki maneno ya Kristo kulikusaidia wewe kujua kile cha kufanya katika maisha yako au kuelezea hali unayokabiliana nayo sasa ambapo kushiriki maneno ya Kristo kungekusaidia.

Jaza mapengo hapo chini ili kutathimini jinsi wewe unavyoshiriki vyema maneno ya Kristo na jinsi unavyoweza kujiboresha. Katika kila mfano hapo chini, andika neno—mlo, onja, au kuona njaa—ambayo inaelezea jinsi wewe unatafuta vyema kujua maneno ya Kristo katika mazingira hayo. Kwa mfano, unaweza kushiriki maandiko katika kujifunza kwako kibinafsi lakini tu onja maneno ya Kristo katika mkutano mkuu.

Masomo ya maandiko ya kibinafsi:

Mkutano wa Sakramenti:

Mkutano mkuu:

Masomo ya Maandiko Kifamilia:

Seminari:

Jioni ya familia nyumbani:

Mkutano wa Akidi ya Ukuhani wa Haruni au darasa la Wasichana:

Shule ya Jumapili:

Maombi ya kibinafsi:

  1. Chukua dakika ili uchague mojawapo wa shughuli ambazo kwazo wewe uliandika kwamba kwa sasa “unaonja” au “kuona njaa.” Katika shajara yako ya kujifunza maandiko, andika jinsi wewe utakavyoshiriki vyema maneno ya Kristo katika mazingira hayo. Kisha fuata kabisa na ufanye hivyo.

Soma 2 Nefi 32:4–7, na utafakari majibu ya maswali yafuatayo (utakuwa unaandika jibu lako kwa mojawapo wa maswali ya kazi ya 4):

  • Katika mstari wa 4, unafikiri inamaanisha nini “kuuliza” au “kubisha”? Maombi yanaweza kuwa mfano mzuri vipi wa kuuliza na kubisha?

  • Pia katika mstari wa 4, Nefi alisema nini ndiyo matokeo ya wale ambao hawatauliza au kubisha?

  • Katika mstari wa 5, ni baraka gani ambayo Nefi anaahidi kuwa tunaweza kupata tunapompokea Roho Mtakatifu?

  • Katika mstari wa 7, ni mitazamo gani watu wa Nefi walikuwa nayo ambayo ilimpelekea yeye kuomboleza kwa sababu yao? Kwa nini unafikiri mitazamo hii inawazuia watu kupekua na kuelewa “elimu kuu”?

  1. Andika katika shajara yako ya kujifunza maandiko ukweli mmoja umejifunza kutoka kwa 2 Nefi 32:4–7, na uelezee kwa nini ukweli huu ni muhimu katika maisha yako.

Picha
ikoni ya umahiri wa maandiko
Umahiri wa Maandiko—2 Nefi 32:3

  1. Unafikiria itakuchukua muda gani wewe kukariri 2 Nefi 32:3 kama unatongoa kila wakati unapokula chakula? Andika aya kwenye kadi au karatasi dogo, na uibebe pamoja nawe. Katika siku chache zijazo, shiriki maneno ya Kristo kwa kutafuta kukariri 2 Nefi 32:3 kabla na baada ya kila mlo unaokula. Katika shajara yako ya kujifunza maandiko, ripoti juu ya milo mingapi ilikuchukua kukariri maandiko hayo.

2 Nefi 32:8–9

Nefi anatushauri kuomba kila siku

Watu wengi wanasema kwamba baada ya wao kutenda dhambi hawataki kuomba kwa Baba wa Mbinguni. Fikiria kwa dakika kuhusu kwa nini hii inaweza kuwa hivi. Ni nani hangependa wewe uombe wakati wowote, hususani baada ya kutenda dhambi? Kwa nini?” Angalia katika 2 Nefi 32:8 kile Roho Mtakatifu hutufunza tufanye kuhusu maombi. Tafakari maswali yafuatayo: Kwa nini unafikiria Bwana anakutaka uombe? Kwa nini unafikiri Shetani hataki wewe uombe?

Soma 2 Nefi 32:9, na utafute ni mara ngapi tunafaa kuomba na baraka gani Bwana hutuahidi kama tutaomba. Unaposoma mstari huu, inaweza kusaidia kujua kwamba kuweka wakfu humaanisha kujitolea kwa huduma ya Mungu au kufanya kuwa takatifu.

Kutoka 2 Nefi 32:9 tunajifunza kanuni hii: tunapoomba kila wakati, tutaweza kufanya yale yote Bwana angetaka sisi tufanye kwa ustawi wa nafsi zetu. (Kumbuka kwamba 2 Nefi 32:8–9 ni kifungu cha umahiri wa maandiko. Unaweza kutaka kukiweka alama kwa njia ya kipekee ili uweze kupata katika siku za usoni.)

Picha
msichana anaomba

Tafakari inamaanisha nini kuomba kila mara. Unaposoma kauli ifuatayo ya Mzee David A. Bednar wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili, weka mstari njia moja au zaidi ambazo tunaweza kutimiza amri ya “kuomba daima”:

Picha
Mzee David A. Bednar

“Kunaweza kuwa na vitu katika hulka zetu, katika tabia zetu, au kuhusu ukuaji wetu wa kiroho ambacho kwacho tunahitaji kushaurina na Baba yetu wa Mbinguni katika sala ya asubuhi. Baada ya kuonyesha shukrani ipasavyo kwa baraka zilizopokelewa, tunasihi kwa ajili ya kuelewa mwelekeo, na usaidizi wa kufanya mambo ambayo hatuwezi kufanya kwa nguvu zetu wenyewe tukiwa peke yake. …

“Wakati wa mkondo wa siku, tunaweka maombi katika mioyo yetu kwa ajili ya misaada endelevu na uongozi. …

“Tunatambua wakati wa siku hii hasa kwamba kuna matukio ambapo kwa kawaida tunataka kuwa na tabia ya kuzungumza kwa ukali, na hatufanyi; au tunaweza kuelekea kuwa na hasira, lakini hatukubali. Tunahisi msaada wa mbinguni na nguvu na kutambua kwa unyenyekevu majibu ya maombi yetu. Hata katika huo wakati wa kutambua, tunatoa maombi ya kimya ya shukrani.

“Kufikia mwisho wa siku yetu, tunapiga magoti tena na kutoa ripoti kwa Baba yetu. Tunatathmini matukio ya siku na kutoa shukrani za dhati kwa ajili ya baraka na msaada tuliopokea. Tunatubu na, kwa msaada wa Roho wa Bwana, kubaini njia tunazoweza kufanya na kuwa bora kesho. Hivyo sala yetu ya jioni hujenga juu ya na ni mwendelezo wa sala yetu ya asubuhi. Na sala yetu ya jioni pia ni maandalizi kwa sala ya maana ya asubuhi.

“Sala za asubuhi na jioni —na sala zote zilizo katikati ya —si matukio yaliyotengana, bali yameunganishwa pamoja kila siku na katika siku, wiki, miezi na hata miaka. Hii ni kwa sehemu jinsi tunavyokamilisha marudio ya maandiko ya ‘kusali kila wakati’(Luka 21:36; 3 Nefi 18:15, 18; M&M 31:12). Sala za maana kama hizo ni muhimu katika kupata baraka kubwa Mungu anazohifadhi katika ghala kwa watoto Wake waaminifu” (“Pray Always,” Ensign or Liahona, Nov. 2008, 41–42).

  1. Andika katika shajara yako ya kujifunza maandiko jinsi unafikiria kufuatia maelekezo ya Mzee Bednar juu ya jinsi “kusali daima” yanaweza kukusaidia katika maisha yako.

Ili kukamilisha somo hili, soma ushuhuda ufuatao kutoka kwa Mzee Spencer J. Condie, ambaye alikuwa wakati huo anahudumu kama Sabini, kuhusu kushiriki maneno ya Kristo: “Unaweza kuwa unakabiliwa na maamuzi ya kuhusu misheni, ajira yako ya siku za usoni, na, hatimaye, ndoa. Unaposoma maandiko na kuomba kwa maelekezo, unaweza hasa usione majibu katika umbo la maneno yaliyopigwa chapa kwenye ukurasa, lakini unaposoma utapokea msukumo wa kipekee, na minong’ono, na, kama ilivyoahidiwa, Roho Mtakatifu ‘atakuonyesha vitu vyote mnastahili kutenda’ [2 Nefi 32:5]” (“Becoming a Great Benefit to Our Fellow Beings,” Ensign, May 2002, 45).

Picha
ikoni ya umahiri wa maandiko
Umahiri wa maandiko—2 Nefi 32:8–9

  1. Katika masaa 24 yafuatayo, jaribu kujumuisha kile umejifunza kuhusu jinsi ya “kusali kila mara” katika maisha yako. Hapo mwanzoni wa somo lifuatalo, utaalikwa kuripoti mawazo na hisia zako kuhusu uzoefu huu. Andika katika shajara yako ya kujifunza maandiko jinsi kujitahidi “kusali kila mara” kunaweza kuleta tofauti katika maombi yako.

  2. Andika yafuatayo katika sehemu ya chini ya kazi za leo katika shajara yako ya kujifunza maandiko:

    Nimejifunza 2 Nefi 32na kukamilisha somo hili mnamo (tarehe).

    Maswali ya ziada, mawazo, na umaizi ningependa kushiriki na mwalimu wangu:

Chapisha